• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 9-March 15)

    (GMT+08:00) 2019-03-15 18:54:14

    Wabunge Uingereza wapinga mpango wa kujiondoa EU

    Mpango wa Theresa May wa Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya umepingwa na wabunge kwa mara ya pili huku zikiwa zimesalia siku 17 hadi muda wa taifa hilo kujitoa katika EU.

    Wabunge walipiga kura kupinga mpango wa waziri mkuu huyo kwa kura 149 - kiwango kidogo ikilinganishwa na kura zilizopigwa Januari.

    Bi May amesema wabunge sasa watapiga kura iwapo Uingereza iondoke katika EU bila ya mpango na iwapo hatua hiyo itashindwa, kura ya iwapo mpango mzima wa kujiondoa - Brexit uahirishwe.

    Waziri mkuu aliwasilisha ombi la dakika ya mwisho kwa wabunge waunge mkono mpango wake baada ya kupata hakikisho kisheria kuhusu msimamo wa Ireland kuhusu kujitoa katika EU.

    Lakini licha ya kuwashawishi wabunge 40 wa chama cha Conservative, haikutosha kikamilifu kubadili pigo la kura ya ushindi wa kihistoria dhidi ya mpango wake mnamo Januari.

    Katika taarifa yake baada ya kupata pigo hilo, May amesema: "Naendelea kuamini kwamba kwa kiasi kikubwa matokeo mazuri ni Uingereza kuondoka katika Umoja wa Ulaya katika namna nzuri na kwa mpango.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako