• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Julai 18-Julai 24)

    (GMT+08:00) 2020-07-24 17:08:53

    Uchaguzi mkuu wa Tanzania kufanyika Oktoba 28

    Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania jumatano (NEC) ilitangaza kuwa, uchaguzi mkuu nchini humo utafanyika tarehe 28, mwezi Oktoba mwaka huu.

    Taarifa iliyotolewa na mwenykiti wa NEC BW. Semistoeles Kaijage imesema, Agosti 25, Tume hiyo itapitisha wagombea wa urais, wabunge na madiwani walioteuliwa na vyama vyao.

    Taarifa hiyo pia imesema, kampeni za uchaguzi zitaanza tarehe 26, mwezi ujao hadi tarehe 27, mwezi Oktoba, siku moja kabla ya uchaguzi.

    Tume hiyo imesema, Watanzania milioni 29 wamejiandikisha kushiriki uchaguzi wa mwaka huu, ikilinganishwa na Watanzania milioni 23 waliojiandikishwa mwaka 2015.


    1  2  3  4  5  6  7  8  9  10  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako