• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Julai 18-Julai 24)

    (GMT+08:00) 2020-07-24 17:08:53

    Eneo la Biashara Huria barani Afrika kuleta fursa mpya kwa ushirikiano wa China na Afrika

    Mtaalam wa Ethiopia Gedio Jalata amesema, Eneo la Biashara Huria barani Afrika (AfCFTA) litaleta fursa mpya kwa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika

    Akizungumza na Shirika la Habari la China Xinhua, Jalata amesema AfCFTA inataka mawasiliano imara ya miundombinu katika bara la Afrika, na msaada wa China utahitajika sana. Amesema kasi ya ujenzi wa miundombinu barani Afrika ni ndogo, na nchi kama China ina uzoefu mkubwa katika ujenzi wa miundombinu, na inaweza kuzisaidia nchi za Afrika kujenga barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege.

    Jalata amesema hivi sasa thamani ya biashara kati ya nchi za Afrika inachukua asilimia 17 tu ya thamani ya jumla ya biashara ya bara hiyo, na sababu kuu ni hali duni ya mawasiliano ya miundombinu kati ya nchi za Afrika.


    1  2  3  4  5  6  7  8  9  10  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako