• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Moyo wa mageuzi kuleta ajabu kubwa zaidi ya China 2018-10-26

    Katika miaka 40 iliyopita tangu China itekeleze sera ya mageuzi na ufunguaji mlango, uchumi wa nchi hiyo umeinuliwa hadi nafasi ya pili duniani, ambapo ukubwa wa viwanda vya utengenezaji umeshika nafasi ya kwanza duniani, na watu zaidi ya milioni 700 wamefanikiwa kuondokana na umaskini. Mabadiliko hayo yanaitwa "Ajabu ya China" na wasomi wa nchi za magharibi. Kwa kukabiliana na hali ya kimataifa inayobadilika na changamoto ya mabadiliko ya mtindo wa maendeleo ya ndani, China itaweza kutimiza ajabu mpya au la? Ukaguzi wa rais Xi Jinping wa China mkoani Guangdong umetupa jibu thabiti kuwa mageuzi ya China hayatasimamishwa, ufunguaji mlango pia utazidishwa, na China itakuwa na ajabu mpya itakayoshangaza dunia.

    • Kipengele cha 301 chaonesha jaribio la Marekani la kuzuia maendeleo halali ya China 2018-10-25

    Hivi karibuni Kituo cha Kusini kilichoundwa na nchi 50 zinazoendelea kimetoa ripoti inayoitwa "Kipengele cha 301 cha Marekani: Kwa nini ni haramu na kinapotosha?". Ripoti hiyo imevutia tena ufuatiliaji wa jumuiya ya kimataifa katika kipengele hicho chenye utata.

    • Marekani kujitoa katika mkataba wa silaha za masafa ya kati za nyuklia kutaharibu msingi wa amani wa dunia 2018-10-24

    Rais Vladimir Putin wa Russia amekutana na msaidizi wa rais wa Marekani anayeshughulikia mambo ya usalama wa taifa Bw. John Bolton ambaye yuko ziarani nchini Russia. Mkutano huo umefanyika chini ya uamuzi wa rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kujitoa katika Mkataba wa Silaha za Masafa ya Kati za Nyuklia. Rais Putin amekosoa madai ya Marekani kuhusu Russia kutofuata mkataba huo, na Bw. Bolton amejibu kuwa hajakwenda Russia kwa nia ya kumaliza suala hilo. Pande zote mbili hazijapata makubaliano yoyote juu ya mkataba huo ndani ya mkutano wa dakika 90.

    • Waziri wa mambo ya nje wa China ahudhuria mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za BRICS 2018-09-28

    Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi jana huko New York alihudhuria mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za BRICS, na kukubaliana na wenzake kuhusu kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kwenye mkutano wa viongozi wa BRICS uliofanyika mjini Jorhannesburg, Afrika Kusini, kuimarisha mawasiliano ya kimkakati, kuzidisha ushirikiano, kuongeza maingiliano kati ya watu na watu, kuleta manufaa kwa pande zote, na kutekeleza ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa.

    • Bw. Guterres asema ushiriki wa pande nyingi upo hatarini wakati unapohitajika zaidi 2018-09-26

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonya kuwa ushiriki wa pande nyingi upo hatarini wakati ambao unahitajika zaidi duniani. Akiongea na viongozi mbalimbali duniani waliohudhuria mjadala wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Guterres ameeleza kuwa hivi sasa kuna tatizo kubwa la kutoaminiana katika taasisi za kitaifa, baina ya nchi na hata kwenye sheria za kimataifa.

    • Katibu mkuu wa UN asema kati ya dola trilioni 5 na trilioni  7 zinahitajika kila mwaka kutekeleza malengo ya maendeleo ya milenia 2018-09-25

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amesema kati ya dola za kimarekani trilioni 5 na trilioni 7 zinahitaji kuwekezwa kila mwaka ili kutimiza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2030.

    • UAE yakanusha shutuma za Iran kuhusu shambulizi la kigaidi 2018-09-24
    Waziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE Bw. Anwar Gargash amekanusha shutuma zilizotolewa na Iran kuwa washirika wa Marekani wa nchi za ghuba wanahusika na shambulizi lililotokea nchini Iran.
    • Korea Kaskazini na Korea Kusini zasaini makubaliano ya Pyongyang 2018-09-19

    Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un na Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini wamesaini makubaliano ya Pyongyang yanayolenga kuondoa tishio la silaha za nyuklia katika peninsula ya Korea.

    • Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wafungwa 2018-09-18

    Mkutano wa 72 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefungwa leo huko New York, ambapo Bibi Maria Fernanda Espinosa kutoka Ecuador ameapishwa kuwa rais wa awamu ya 73 ya baraza hilo.

    • Ikulu ya Korea Kusini yaeleza mambo yatakayojadiliwa kati ya viongozi Korea Kusini na Kaskazini 2018-09-17

    Msemaji wa ikulu ya Korea Kusini Bw. Im Jong-seok amesema, mazungumzo yajayo kati ya viongozi wa rais wa nchi hiyo na kiongozi wa Korea Kaskazini yatazingatia uhusiano kati ya nchi hizo mbili, kuhimiza mazungumzo kati ya Korea kaskazini na Marekani na kutuliza hali ya wasiwasi ya kijeshi katika peninsula ya Korea.

    • Marais wa China na Russia watumaini vijana wa nchi hizo mbili wataenzi urafiki kizazi baada ya kizazi 2018-09-13
    Rais Xi Jinping wa China na mwenzake Vladimir Putin wa Russia jana kabla ya kurejea Beijing walitembelea Kituo cha watoto wa Russia cha "Bahari" huko Vladivostok, Russia. Viongozi hao wawili wana matumaini kuwa vijana wa nchi hizo mbili wataimarisha mawasiliano, na kuenzi urafiki kati ya pande hizo mbili kizazi baada ya kizazi.
    • China imekuwa msukumo mpya katika kuhimiza ujenzi wa umoja wa uchumi wa Asia Kaskazini Mashariki 2018-09-12

    Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba katika mkutano wa Baraza la 4 la uchumi la Mashariki uliofanyika mjini Vladivostok, Russia.

    • Rais wa Ufaransa ajitahidi kuondoa hali ngumu ya Umoja wa Ulaya 2018-09-05

    Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, ambaye ni mmoja wa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, mwishoni mwa mwezi Agosti, alihutubia mkutano wa mabalozi wa Ufaransa katika nchi za nje, akitetea msimamo wa pande nyingi, na kuonyesha kuwa Ufaransa inajitahidi kuongoza Umoja wa Ulaya kujiondoa kwenye hali ngumu.

    • Rais wa Ukraine awasilisha rasimu wa sheria bungeni kuhusu matarajio ya kujiunga na Shirika la NATO na Umoja wa Ulaya 2018-09-04
    Rais Petro Poroshenko wa Ukraine amewasilisha rasimu ya sheria bungeni itakayowekwa kwenye katiba kuhusu matarajio ya nchi hiyo kujiunga na Shirika la NATO na Umoja wa Ulaya.
    • Russia kuchukua hatua za kukabiliana na vikwazo vilivyowekwa na Marekani 2018-08-23

    Rais Vladmir Putin wa Russia amesema vikwazo vipya vilivyowekwa na Marekani dhidi ya Russia havina maana, na vinakwenda kinyume na matarajiao ya Marekani. Tangu Marekani ilipotangaza kuweka vikwazo dhidi ya Russia mwanzoni mwa mwezi huu, Russia imechukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na hali hiyo.

    • Marekani yaendelea kuinua kigezo cha uwekezaji wa kigeni nchini humo 2018-08-15

    Hivi karibuni, Marekani imetoa muswada wa sheria wa mageuzi ya ukaguzi wa usalama wa taifa dhidi ya uwekezaji wa kigeni. Hii ni mara ya kwanza kwa Marekani kurekebisha na kuimarisha uwezo wa kamati ya uwekezaji wa kigeni katika miaka karibu kumi iliyopita. Kamati hii itafanya ukaguzi mkali zaidi kwa uwekezaji wa kigeni unaotaka kuingia nchini Marekani.

    • Rais wa zamani wa Chile ateuliwa kuwa kamishna mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa mataifa 2018-08-09

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amemteua rais wa zamani wa Chile Bi. Michelle Bachelet kuwa Kamishna mkuu wa haki za binadamu wa Umoja huo akichukua nafasi ya Bw. Zeid Ra'ad Zeid Al-Hussein atakayemaliza muda wake mwishoni mwa mwezi huu.

    • Mchumi mkuu wa IMF asema ni kosa kwa Marekani kujaribu kupunguza urari wa biashara kwa njia ya kuongeza ushuru 2018-08-08

    Mchumi mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF Bw. Maurice Obstfeld amesema ni kosa kwa Marekani kujaribu kupunguza urari wa biashara kwa njia ya kuongeza ushuru wa forodha.

    • Uchunguzi kuhusu uingiliaji wa Russia kwenye uchaguzi wa Marekani huenda utasababisha pigo kubwa rais Trump 2018-08-07
    Jumapili iliyopita rais Donald Trump wa Marekani alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa ripoti kuhusu mtoto wake Donald Trump Jr. zote ni "habari feki", na pia amekiri kuwa mwaka 2016 mtoto wake huyo alikutana na mwanasheria wa Russia kwa ajili ya kupata taarifa za kiintelijinsia kuhusu mpinzani wake wa kisiasa, na kukitaja kitendo hicho kuwa ni "halali kikamilifu na ni mazoea ya kawaida kwenye duru za kisiasa".
    • Kauli ya Lawrence Kudlow inakanganya Marekani 2018-08-04

    Mkurugenzi wa kamati ya uchumi ya Marekani Lawrence Kudlowameongea na baadhi ya vyombo vya habari na kuonya CHina kutopuuza uwezo wa rais Trump wa kutimiza ahadi yake, na kusema Marekani itaunda muungano kwa haraka kukabiliana na kitendo kisicho cha haki cha biashara ya China.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako