Wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya CRI
China Radio International
China
Dunia
(GMT+08:00) 2003-11-29 01:28:08    
Chanjo ya ugonjwa wa SARS

cri
    Majaribio ya chanjo ya ugonjwa wa SARS mwilini yamemalizika hivi karibuni, hivi sasa yanasubiri kibali cha kufanywa mwilini mwa binadamu, hatua ambayoinaashiria mafanikio makubwa waliyopata wataalamu wa China katika utafiti wa Chanjo ya aina hiyo.

    Tangu yalipozuka maambukizi ya ugonjwa wa SARS mkoani Guangdong, Chian, Mwezi Novemba mwaka uliopita, kwa muda wa miezi michache tu ugonjwa huo ulienea sehemu kubwa ya China, hali ambayo inabainisha kuwa ukosefu wa chanjo ya ugonjwa huo ulichangia kuenea kwa maambukizi ya SARS.

    Mwezi Aprili mwaka huu, maambukizi ya SARS yalipokuwa yakienea kwa kasi sana, Uongozi wa udhibiti wa SARS ya China ulizindua kwa dharura ?Mradi wa utafiti wa chanjo ya SARS? ambao umeorodheshwa katika suala la maendeleo ya teknolojia ya kiwango cha juu ya taifa. Chanjo ya SARS ni virusi vya ugonjwa wa SARS viliyokwisha uawa ambayo binadamu akipandikizwa virusi vya aina hiyo, basi mwilini mwake zitajitokeza chembechembe za upinzani ambazo zitamlinda dhidi ya virusi vya aina hiyo.

    Baada ya kujitahidi kwa zaidi ya miezi sita, hivi sasa China imemaliza kwa ujumla utafiti wa kuondoa uhai wa virusi vya SARS vitakavyotumiwa kwenye mwili wa binadamu, inakadiriwa kwamba chanjo ya SARS itaweza kutumiwa kwa binadamu kwa majaribio kabla ya mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.

    Habari zinasema kuwa chanjo hiyo ya SARS imeshatumiwa kwenye mwili wa kima kwa majaribio, na matokeo yake yameonesha kwamba baada ya kima kupewa chanjo hiyo, hali yake ilionekana kama ya zamani. Na siku ya 10 baada ya kupewa chanjo hiyo, miilini ya kima waliofanyiwa majaribio ilikuwa na chembechembe zinazokinga virusi vya SARS, hali ambayo imekuwa na uhakika juu ya usalama wa matumizi ya chanjo ya aina hiyo. Mafanikio hayuo ya utafiti wa chanjo ya SARS ya China yamethibitishwa na shirika la afya ulimwenguni, WHO.