Wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya CRI
China Radio International
China
Dunia
(GMT+08:00) 2004-07-20 13:47:09    
Radio China hongera

cri
    Msikilizaji wetu Noel E Mashauri wa S.L.P 42 Kiomboi-Iramba Singida Tanzania ametuletea barua akisema kuwa, kwanza anapenda kutoa salamu kwa watangazaji na watayarishaji wa vipindi wa Radio China kimataifa. Anasema yeye ni mzima wa afya anaendelea vizuri na shughuli za ujenzi wa taifa bila kusahau kusikiliza matangazo ya Radio China Kimataifa. Sisi hapa Radio China hatujambo, na tunashukuru sana kwa salamu zako.

    Bwana Noel anasema pia anapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa uongozi wa Redio China kimataifa kwa yote wanayowafanyia wasikilizaji. Pamoja na juhudi za watangazaji wote kwa umahiri wao mkubwa wa kutangaza. Anasema juhudi hizo ni kubwa na zinahitaji ushirikiano wa dhati ili kuzidumisha, kwa upande wake yuko bega kwa bega na radio yake pendwa, kwa namna moja ama nyingine kudumisha hayo ambayo redio China inayafanya kuleta urafiki, amani na ushirikiano katika sehemu zote duniani.

    Anasema kwa kuthibidisha hilo ametuletea shairi la pongezi, shairi hilo linasema hivi:

    Redio China hongera, kutangazia dunia

    Kwa habari zako bora, wasikilizaji ringia

    Na mafunzo yalofaulu, kwetu sisi twasifia

    Waitangaza dunia, redio China hongera

    Radio China pongezi,kwa huo uwepo wako

    Hutakosa njema enzi, kwa wote rafiki zako

    Jinsi ulivyo mjenzi, shikana huko na huko

    Redio China hongera,waitangaza dunia

    Redio China waleta, mshikamano ulo mwema

    Waunganisha kupata ,dunia isiyovuma

    Kwa vurugu na kufuta, tofauti na lawama

    Amani waitafuta, kwa shime isiyokoma

    Waitangaza dunia,redio China hongera

    Anasema anavyodhani hayo yote yasingefanikiwa kama kusingekuwa na mshikamano mzuri kati ya wafanyakazi wote wa redio China .Utangazaji bora na uhariri makini ndiyo unaofanya mafanikio yaongezeke na kukua siku hadi siku hivyo. Shairi lake linaendelea kusema:

    Kwa sasa najibarizi, kwa uzalendo pomoni

    Kwa wale wafanyakazi, Han mei mama chen

    Fadhili Mpunji kazi, kwao bidii si duni

    Na wahariri wajuzi, kwa mpangilio makini

    Nawapongeza wote, redio China hongera

    Bwana Noel Mashauri anasema, anapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa kumtumia bahasha ambazo zimeshalipiwa stempu, hali ambayo inamrahisishia si yeye tu bali na wasikilizaji wenzake wote katika kutuma majibu na taarifa nyingine. Hivyo ni njia ambayo itakuza uhusiano wetu sisi wasikilizaji na redio China na wananchi wake kwa ujumla, na pia hapa chini ni salamu zake:

    Wapenzi twajivunia, kwa mapendo madhubuti

    Ni bure wahudumu,hata wale mahutihuti

    Daraja unganisha, usumbufu hatupati

    Wananchi wote Asia, Afrika na Djibuti

    Ulaya na amerika, marafiki ni bahati

    Asante kwa kurahisisha mawasiliano

     Ni redio hiyo hiyo ,imeunga urafiki

     Bila kinyongo cha moyo, tena taharuki

     Kuonyesha nia inayo, inadumishwa mashabiki

     Kwa kukudhi itakayo, klabu za salamu lukuki

     Asante kwa kurahisisha mawasiliano

     Bwana Mashauri anasema, asingependa kuendelea zaidi ila tudumishe urafiki wetu, umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, vile vile kidole kimoja hakivunji chawa

    Angependa kukumbusha kuwa wasikilizaji wa Radio China kimataifa wanawapenda sana wafanyakazi wa redio yao wakiwakilishwa na Han mei, mama Chen, Fadhili Mpunji na wengine.

Idhaa ya Kiswahili 2004-07-20