Nchi za Afrika Mashariki zatangaza bajeti ya mwaka 2016-2017
Nchi za Afrika Mashariki Kenya, Tanzania na Uganda wiki hii zimetangaza bajeti zao za mwaka 2016-2017.
Bajeti ya Kenya imeongezeka hadi dola za kimarekani bilioni 23 kutoka bilioni 20 za mwaka 2015-2016, ambayo itaongeza kodi ili kuwanufaisha watu wenye mapato chini.
Wizara ya fedha ya Tanzania nayo imetangaza bajeti ya mwaka 2016-2017 yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 14.7.
Waziri wa fedha wa nchi hiyo Bw. Philip Mpango amesema dola za kimarekani bilioni 8.9 katika bajeti hiyo itatolewa nchini, na nyingine bilioni 1.8 zitatokana na misaada kutoka nje.
Na nchini Uganda, bajeti yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 7.8 imetangazwa, ambayo walimu na wahadhiri wapata nyongeza ya mshahara, huku bajeti ikiongezeka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |