• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Oktoba 1-Oktoba 7)

    (GMT+08:00) 2016-10-08 17:18:59

    Antonio Guterres ateuliwa kuchukua wadhfa wa Ban Ki-moon

    Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwa wingi wa kura limemteua aliyekuwa waziri mkuu wa Ureno Antonio Guterres kuwa katibu mkuu mpya wa umoja huo.

    Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa unatarajiwa kufanyika wiki ijayo kuidhinisha uchaguzi wake kwa muhula wa miaka mitano.

    Bwana Guterres ,mwenye umri wa miaka 67,ambaye aliongoza kitengo cha wakimbizi katika Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha miaka 10 atachukua mahala pake Ban Ki-moon mapema mwaka ujao.

    Bwana Ban mwenye umri wa miaka 72,alimtaja bwana Guterres kama 'chaguo zuri' la kumrithi.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako