• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Oktoba 1-Oktoba 7)

    (GMT+08:00) 2016-10-08 17:18:59

    Wananchi wa Colombia wapinga makubaliano ya amani na FARC

    Baada ya kura ya maoni , matokeo yanaonyesha kuwa wananchi wa Colombia wamepinga makubaliano ya amani na kundi la waasi la FARC, makubaliano yaliyoafikiwa hivi karibuni kati ya serikali na kundi hili la waasi.

    Kwa mujibu wa matokeo rasmi ya kura ya maoni, kura ya "hapana" imeshinda kwa 50.21% dhidi ya 49.78% kwa kura ya "ndiyo."

    Zaidi ya watu milioni kumi na tatu wamepiga kura, lakini wanaopinga makubaliano hayo wameshinda kwa kura zisizozidi elfu sitini.

    Wakazi wa miji mbalimbali ndio wameonekana kupinga makubaliano haya kwa kiasi kikubwa. Katika mji wa Medellin, kwa mfano, kura ya "hapana" imeshinda kwa zaidi ya 60%. Magari yalizunguka kila sehemu yakiliza mahoni, huku raia wakifurahia ushindi katika mji mkuu huo wa jimbo la Antioquia, ngome kuu ya rais wa zamani Alvaro Uribe ambaye ambaye aliwataka wakazi wa jimbo hilo kupiga kura ya "hapana."


    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako