Kikosi cha usalama cha Afghanistan chamwua kamanda mwandamizi wa kundi la Taliban
Gavana wa mkoa wa Helmand kusini mwa Afghanistan Bw. Hayatullah Yaht amesema vikosi vya usalama vya Afghanistan vimemuua kamanda mwandamizi wa kundi la Taliban Mullah Eqdam, wakati alipowaongoza wapiganaji wa kundi hilo kwenye shambulizi dhidi Lashkar Gah, mji mkuu wa mkoa wa Helmand. Bw. Yaht amesema Eqdam ndiye aliyepanga mashambulizi mkoani humo katika miaka iliyopita, na kifo chake kitaleta pigo kubwa kwa kundi hilo mkoani humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |