• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Mei 25-Mei 31)

    (GMT+08:00) 2019-05-31 18:04:40

    Rais wa Afrika Kusini atangaza baraza dogo la mawaziri

    Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametangaza baraza jipya la mawaziri mjini Pretoria, akipunguza idadi ya mawaziri kutoka 36 hadi 28.

    Rais Ramaphosa amesema ni muhimu kuwa mfumo na ukubwa wa serikali uendane na mahitaji ya watu na kuhakikisha rasilimali za umma zinagawiwa kwa ufanisi.

    Rais Ramaphosa ameunganisha wizara kadhaa ikiwemo wizara ya biashara na viwanda imeunganishwa na wizara ya maendeleo ya uchumi, wizara ya masuala ya mazingira pia imeunganishwa na wizara ya misitu na uvuvi.

    Wataalam walimtaka rais huyo kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, wakisema linaweka shinikizo kubwa kwa sheria ya mishahara ya watumishi.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako