• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Mei 25-Mei 31)

    (GMT+08:00) 2019-05-31 18:04:40

    Jeshi la Nigeria layalaumu mashirika ya kibinadamu kwa kulisaidia kundi la Boko Haram

    Jeshi la Nigeria limeyatuhumu mashirika ya kibinadamu katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kwa kulisaidia kundi la Boko Haram, na kuonya kuwa linapinga kitendo hicho.

    Katika taarifa yake, msemaji wa jeshi hilo Sagir Musa amekataa kutoa majina ya mashirika ya kibinadamu yanayoshukiwa kulipatia kundi hilo misaada kama vile chakula. Hata hivyo, Bw. Musa amethibitisha kuwa mpiganaji wa ngazi ya juu wa kundi hilo amekamatwa wakati akipokea msaada wa chakula kutoka shirika moja la misaada ya kibinadamu lililoko eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ambapo kuna mapambano makali dhidi ya magaidi.

    Amesema mpiganaji huyo wa Boko Haram aliyetambuliwa kuwa ni Muhammed Modu, alikamatwa na askari jumapili iliyopita.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako