• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Septemba 28-Oktoba 4)

    (GMT+08:00) 2019-10-04 16:54:53

    George Weah afuta mpango wa kuuunda Mahakama maalum

    Rais wa Liberia George Weah amekataa wito na shinikizo za Kimataifa, kuunda Mahakama maalum kuchunguza mauaji ya zaidi ya watu 250,000 wakati wa machafuko ya wenyewe kwa wenyewe katika taifa hilo la Afrika Magharibi.

    Rais Weah amebainisha hilo, baada ya kurejea nyumbani akitokea kwenye mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Marekani.

    Weah amesema haelewi, wanaharakati wanachokitaka, kwa sababu tangu alipoingia madarakani, hajawahi kusema kuwa ataunda Mahakama hiyo.

    Akishangiliwa na wafuasi wake, mchezaji huyo wa zamani wa mchezo wa soka amesema kuwa kazi kubwa aliyonayo ni kuinua uchumi wa taifa hilo miongoni mwa masuala mengine muhimu.

    Msimamo wa rais Weah, umewasikitisha wanaharakati wa haki za binadamu ambao walikuwa na matumaini makubwa kuwa angeamuru kuundwa kwa Mahakama hiyo.

    Rais Weah ni rais wa pili kuchaguliwa kidemokrasia katika historia ya nchi hiyo,baada ya kumalizika kwa vita vya muda mrefu kati ya mwaka 1989 hadi 1997.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako