• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Septemba 28-Oktoba 4)

    (GMT+08:00) 2019-10-04 16:54:53

    Wakimbizi wa Burundi 600 warejea nyumbani

    Wakimbizi wa Burundi 600 waliokimbilia nchini Tanzania wamerudishwa makwao "kwa hiari yao" tangu Alhamisi, Oktoba 3, kwa mujibu wa serikali ya tanzania.

    Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi, UNHCR, lilikuwa limemepanga katika siku za hivi karibuni kuwarudisha nchini Burundi wakimbizi takribani 400, wote kwa hiari yao.

    Hata hivyo, wakimbizi 588 ndio walisafirishwa hadi katika kambi ya muda ya Nyabitare katika mkoa wa Ruyigi, mashariki mwa Burundi. UNHCR imehakikisha kwamba imechunguza kuwa "wale ambao waliongezwa katika kundi hilo la watu 400 wamerudishwa kwa hiari yao".

    Tangu mwaka 2017, wakimbizi zaidi ya 78,000 kutoka Burundi wamerudishwa kutoka Tanzania.

    Baada ya mkutano na mwenzake wa Burundi mwishoni mwa mwezi Agosti, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania alitangaza kwamba serikali yake itawarudisha kwa hiari yao au kwa nguvu wakimbizi wote wa Burundi kuanzia tarehe mosi Oktoba mwaka huu. Uamuzi ambao ulikosolewa na jamii ya kimataifa.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako