Wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya CRI
China Radio International
China
Dunia
(GMT+08:00) 2004-03-19 21:26:41    
Reli kati ya Qinghai na Tibet

cri

    Sasa ni miaka miwili na nusu tangu reli kati ya mikoa ya Qinghai na Tibet kuanza kujengwa. Hivi sasa reli kati ya Qinghai na Tibet imeshapita kwenye mlango wa mlima wa Tanggula wenye urefu wa zaidi ya mita 5,000 kutoka usawa wa bahari na kuingia mkoani Tibet. Reli kati ya Qinghai na Tibet ni mojawapo miongoni mwa miradi mikubwa inayojengwa katika miaka ya karibuni nchini China kwa ajili ya kustawisha uchumi wa sehemu ya magharibi. Reli hiyo itachangia sana maendeleo ya uchumi wa sehemu ya Tibet na kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya Tibet na mikoa mingine ya China.

    Reli kati ya Qinghai na Tibet iliyoko katika sehemu ya magharibi ya China, inaanzia mji wa Xining, mkoani Qinghai, hadi mji wa Lhasa, mkoani Tibet. Toka miaka ya 50 ya karne iliyopita, China ilinuia kujenga reli moja kutoka sehemu ya China bara iendayo Tibet. Ujenzi wa kipindi cha kwanza cha reli hiyo ambacho ni reli kati ya miji ya Xining na Geermu, mkoani Qinghai ulizinduliwa rasmi mwaka 1974 na ulikamilika mwaka 1984 ambapo ujenzi wa kipindi cha pili cha reli yenye urefu wa kilomita 1,118 kati ya miji ya Geermu na Lhasa ulianza rasmi mwezi Juni mwaka 2001.

 

    Ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet ni hatua muhimu inayochukuliwa na China ya kustawisha sehemu ya magharibi na kusawazisha maendeleo ya uchumi ya sehemu mbali mbali. Mtafiti wa idara ya utafiti wa uchumi na jamii ya taasisi ya utafiti wa elimu ya Tibet ya China, Bw. Xu Ping anasema kuwa ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet utaleta athari kubwa kwa maendeleo ya Tibet, alisema, "Ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet ni jambo kubwa katika harakati za ustawishaji wa sehemu ya magharibi ambalo litaleta athari kubwa kwa maendeleo ya Tibet. Kimsingi, itatatua kabisa tatizo la mawasiliano ambapo vikwazo vya mawasiliano kati ya Tibet na mikoa mingine ya China bara vitaondolewa kabisa."

    Mkoa ujiendeshao wa Tibet uko katika sehemu ya mpakani, kusini magharibi ya China ambao ni mkoa pekee usio na njia ya reli hapa nchini. Mawasiliano finyu na miundo mbinu hafifu vilikwamisha maendeleo ya uchumi wa Tibet. Katika muda mrefu uliopita, rasilimali za madini na mazao ya kilimo na mifugo ya Tibet havikuweza kusafirishwa kwa sehemu nyingine, na gharama ya usafirishaji wa bidhaa za viwanda na vitu vinavyohitajiwa katika maisha ya watu ilikuwa kubwa, hali ambayo ilisababisha maendeleo ya uchumi wa Tibet kuwa nyuma yakilinganishwa na mikoa mingine ya China.

    Hivi sasa vitu vyote vinavyohitajiwa na Tibet vinasafirishwa huko kwa magari, ingawa kuna barabara 4 ziendazo Tibet katika China bara, lakini iko barabara moja tu kati ya Qinghai na Tibet inayoweza kusafirisha mizigo bila kuathiriwa na hali ya hewa na vikwazo vingi vya ardhini, hivyo kazi za uchukuzi za barabara hiyo zimekuwa nyingi siku hata siku ambapo hivi sasa, zaidi ya 80% ya mizigo inasafirishwa huko kwa njia ya barabara. Hivyo ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet utaleta ufanisi mkubwa wa kiuchumi na kijamii kwa kuimarisha uwezo wa uchukuzi na marekebisho ya mfumo wa uzalishaji mali.


1  2