Wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya CRI
China Radio International
China
Dunia
(GMT+08:00) 2004-03-19 21:26:41    
Reli kati ya Qinghai na Tibet

cri

    Habari zinasema kuwa baada ya ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet kukamilika, inleta nafasi nyingi kwa maendeleo ya sekta za rasilimali ya madini, wanyama na mimea adimu ya uwanda wa juu, utengenezaji wa vinywaji visivyo na uchafuzi, tiba na madawa ya kitibet, mazao ya kilimo na mifugo na vitu vya kazi za mikono vya kabila la kitibet. Bidhaa mbali mbali zenye umaalumu wa uwanda wa juu pia zitaweza kusafirishwa kwa sehemu mbali mbali kwa njia hiyo ya reli ambapo kupungua kwa gharama ya usafirishaji kutaweza kukuza nguvu ya ushindani ya rasilimali za Tibet katika masoko ya nchini na ulimwenguni, na kuvutia uwekezaji vitega uchumi kutoka nchi za nje. Pamoja na kukuzwa kwa uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya Tibet na sehemu za nje, utandawazi wa masoko ya Tibet pia utaweza kuendelezwa, na uchumi wa sehemu hiyo utahimizwa zaidi.

    Reli kati ya Qinghai na Tibet itafanya mawasiliano yawe rahisi na salama, ya raha na ya gharama ndogo zaidi kwa watalii, hali ambayo italeta ongezeko kubwa la watalii na kuendeleza mambo ya utalii ya Tibet. Profesa Li Zhu-qing wa taasisi ya uchumi wa makabila madogo madogo ya chuo kikuu cha makabila cha China alifafanua zaidi, "sehemu ya Tibet ni sehemu isiyofaa kwa uendelezaji wa viwanda vya kijadi, bali ni mwafaka kwa kukuza mambo ya utalii. Tibet ina rasilimali nyingi za kiasili za utalii na mandhari nzuri yenye kivutio kikubwa. Pili, Tiber ina utamaduni wenye umaalumu wa kijadi, hivyo utalii unaweza kuwa nguzo ya uchumi wake."

    Kujengwa reli kati ya Qinghai na Tibet kutachangia maendeleo ya sekta ya huduma ya Tibet, pamoja na ujenzi wa reli na vituo vya treni, miji mingi itaanzishwa ambayo itatoa ajira nyingi mpya.

    Katika taarafa ya Liuwu iliyoko katika kiunga cha kaskazini mwa mji wa Lhasa, kijana aitwaya Dawa, baada ya kusikia kwamba kituo cha treni kitajengwa karibu na nyumba yake, alisema kuwa atajenga hoteli moja karibu na huko ili kupata pesa nyingi zaidi na kuishi maisha ya kama wakazi wa mjini. Mzee mmoja wa kabila la watibet alisema kuwa anataka kupanda treni kutembelea Beijing, kwani angeweza kuburudishwa na mandhari ya kando kando ya reli.

    Ukweli ni kwamba hata kabla ya ujenzi wa reli kukamilika, sehemu za ujenzi wa reli zilikuwa zimeleta manufaa kwa wakazi wa huko. Habari zinasema kuwa wenyeji wa huko wanauza vifaa vya ujenzi na vyakula kwa makampuni ya ujenzi, wakulima na wafugaji wengi wa huko waliajiriwa katika ujenzi wa reli, inakadiriwa kwamba mwaka 2003 Tibet itaweza kuwa na pato la Yuan zaidi ya milioni 300. Bw. Xu Ping kutoka taasisi ya utafiti wa jamii na uchumi ya kituo cha utafiti wa elimu ya Tibet cha China alisema, "Ujenzi wa reli kati ya Qinghai na Tibet umechangia moja kwa moja maendeleo ya uchumi wa Tibet na kuleta ajira nyingi kwa wakulima na wafugaji wa huko. Hadi hivi sasa kiasi cha wakulima na wafugaji elfu 6 hadi elfu 10 wanashiriki katika ujenzi wa reli hiyo. Inakadiriwa kwamba toka mwaka 2002 hadi mwaka 2003, wenyeji wa huko wameongezewa pato la Yuan zaidi ya milioni 100 kutokana na vibarua.

Idhaa ya Kiswahili 2004-03-19


1  2