• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (4 Julai-8 Julai)

    (GMT+08:00) 2016-07-08 19:12:25

    Katumbi asema atarudi nyumbani hivi karibuni kuongoza maandamano

    Mwanasiasa wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi Chapwe ambaye amekuwa nchini Uingereza kupata matibabu amesema atarudi nyumbani kuongoza maandamano ya amani dhidi ya rais Joseph Kabila.

    Mwezi uliopita, Katumbi alikuhumiwa jela kwa makosa ya kuhusika na uuzaji wa nyumba kwa njia ya ulaghai kwa raia mmoja wa Ugiriki.

    Mahakama mjini Lubumbashi ilimhukumu jela miaka 3.

    Hata hivyo, Katumbi hajasema ni lini atarajea nyumbani lakini amesema tu kuwa atafika jijini Kinshasa hivi karibuni.

    Tayari Katumbi amesema atawania urais dhidi ya Jospeh Kabila ikiwa ataamua kuwania tena.

    Thomas Dakin Mwenyekiti wa Mashirika ya kiraia Mashariki katika jimbo la Kivu Kaskazini amesema ni haki ya Katumbi kuandaa maandamano nchini humo ikiwa atarejea.

    Katumbi ameendelea kuilaani serikali ya Kinshasa kwa kumlenga kisiasa, ili asiwanie urais.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako