FBI kutomfungulia mashitaka Bibi Hillary Clinton
Shirika la upelelezi la Marekani FBI halitamfungulia mashtaka bibi Hillary Clinton kwa tuhuma ya kuvujisha siri za taifa. Mkurugenzi wa shirika hilo Bw James Comey akifafanua uamuzi huo amesema Bibi Clinton alipokuwa waziri wa mambo ya nje alitumia email binafsi kushughulikia mambo ya kiofisi, kitendo ambacho kinaonesha kuwa yeye na msaidizi wake hawakuwa makini katika kushughulikia siri za taifa, lakini hakuna ushahidi wowote unaoonesha kuwa walikiuka sheria kwa makusudi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |