• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (4 Julai-8 Julai)

    (GMT+08:00) 2016-07-08 19:12:25

    Wayahudi 6,000 kuhamishiwa israel

    Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametangaza kwamba Serikali yake imeanzisha mpango wa kuwahamishia Wayahudi wa Ethiopia nchini Israel.

    Takriban Waethiopia 9,000 wanaodai kuwa Wayahudi wanasubiri kuhamia Israel, na wamesubiri kwa miaka kadhaa.

    Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu wa Israel amebaini kuwa shughuli hiyo itaanzishwa hivi karibuni.

    Amesema serikali yake itahakikisha Wayahudi walioko nchini Ethiopia wanapelekwa nchini Israel kujiunga na jamaa zao ambao tayari wamefika Israel.

    Inaarifiwa kuwa Wayahudi Waethiopia 130,000 wanaishi Israel kwa sasa, tangu shughuli ya kuwahamisha ianze 1984.

    Waziri Mkuu wa Israel amekamilisha ziara yake barani Afrika nchini Ethiopia, baada ya kuzuru Uganda, Kenya na Rwanda


    1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako