Wiki hii Chansela wa Ujerumani Bibi Angela Merkel amelaani vikali mashambulizi yaliyotokea hivi karibuni nchini, na kutangaza mpango unaolenga kuimarisha usalama nchini Ujerumani.
Hatua zinazotajwa kwenye mpango huo ni pamoja na kutoa urahisi wa kuruhusu kuwarudisha wakimbizi nyumbani, kuweka mfumo wa kutambua wakimbizi wenye siasa kali na kufanya luteka za kupambana na ugaidi.
Hivi karibuni Ujerumani imekuwa ikikumbwa na mashambulizi, na raia wengi wamekuwa wanakosoa sera ya serikali kuhusu wakimbizi wakisema wasiwasi wao hausikilizwi vya kutosha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |