Hillary Clinton akubali uteuzi wa chama cha Democratic
Mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Democratic, Hillary Clinton, amekubali uteuzi wake kuwania kinyang'anyiro cha urais katika uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika Novemba 8 mwaka huu nchini Marekani.
Kwenye hotuba yake mjini Philadelphia Ijumaa Clinton alisema wakati wa kupambana na mpinzani wake sasa umeanza rasmi.
Alitoa wito kwa wanachama wote wa Democratic kuungana naye huku akimkebehi mpinzani wake Trump, katika madai yake kuwa ni yeye pekee anayeweza kuyasuluhisha matatizo ya Marekani.
Alisema kuwa Wamarekani hufanya kazi kwa pamoja kuyatatua yote yanayonufaisha taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |