• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (23 Julai-29 Julai)

    (GMT+08:00) 2016-07-29 18:56:28

    Wafanyakazi wa UN washambuliwa Nigeria

    Washambuliaji wasiojulikana wameshambulia msafara wa Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, katika jimbo la Borno nchini Nigeria.

    Wafanyakazi kutoka katika mashirika hayo ya Umoja wa Mataifa UNICEF, IOM na UNFPA walikuwa wakitokea Bama kwenda Maiduguri katika jimbo hilo la Borno, ambako waligawa misaada ya kibinadamu

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF, mfanyakazi mmoja wa shirika hilo na mwingine kutoka IOM walijeruhiwa katika shambulio na kukimbizwa hospitali.

    Msafara huo ulikuwa katika maeneo ya mashambani kaskazini mashariki mwa Nigeria, ambako mizozo ya wenyewe kwa wenyewe imesababisha kuwepo kwa tatizo la utapiamlo.

    Kwa mujibu wa UNICEF shambulio hilo sio tu limewagusa wafanyakazi hao wa kutoa misaada, bali pia watu wote wanaohitaji misaada na usaidizi unaoletwa na watu hao.

    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako