Nchini Kenya afisa mmoja wa polisi amewauwa wenzake 6 kwa kuwamiminia risasi katika kituo cha polisi cha Kapengunria.
Awali iliripotiwa kuwa aliyewapiga risasi polisi hao alikuwa mshukiwa wa kundi la kigaidi la al- Shabab aliyekuwa anazuiliwa katika kituo hicho.
Afisa huyo wa polisi aliyeuwa wenzake kwa jina Abdihakim Maslah alikuwa amewasilisha ombi la kutaka kujiuzulu kazi yake lakini halikukubaliwa.
Mienendo yake imekuwa ikichunguzwa na polisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |