Umoja wa Afrika wafuatilia hali ya Sudan Kusini
Wiki hii mkutano wa 27 wa Umoja wa Afrika umefunguliwa mjiniKigali Rwanda.
Mwenyekiti anayeondoka wa tume ya Umoja huo Bibi Nkosazana Dlamini-Zuma alisema, Umoja huo unafuatilia kwa karibu mapigano mapya yaliyotokea hivi karibuni nchini Sudan Kusini.
Bibi Zuma amesema serikali na viongozi wa nchi wanapaswa kuwalinda na kuwahudumia wananchi wao, siyo kuwaletea madhara.
Pia amesema bara la Afrika linapaswa kuheshimu maisha ya watu, na serikali isiyojali maisha ya watu haivumiliki kamwe.
Maudhui ya mkutano huu ni kulindwa kwa haki za kibinadam na hasa haki za wanawake, na pia paspoti mpya ya Afrika inatarajiwa kuzinduliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |