• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (9 Julai-15 Julai)

    (GMT+08:00) 2016-07-15 17:46:07

    Carter atangaza kupelekwa Iraq mamia ya askari wa ziada

    Mkuu wa Pentagon Ashton Carter ametangaza Jumatatu hii mjini Baghdad, kutuma mamia ya askari wa ziada nchini Iraq ili kusaidia vikosi vya serikali kupambana dhidi ya wanajihadi wa kundi la Islamic State (IS) na hasa kuuteka mji wa Mosul.

    Katika ziara yake ya nne nchini Iraq tangu kuteuliwa kwenye nafasi hiyo mwezi Februari 2015, Bw Carter amekutana na Waziri Mkuu Haider al-Abadi na mwenzake Khaled al-Obeidi, wakati ambapo Marekani inaongoza muungano mpana wa kimataifa unaopambana dhidi ya kundi la IS.

    Idadi hii ya askari wa ziada itapelekea idadi ya wanajeshi wa Marekani nchini Iraq kuongezeka na kufikia askari 4,600, hasa kwa ajili ya ujumbe wa mafunzo kwa askari wa Iraq.

    1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako