Riek Machar apokea matibabu Sudan
Aliyekuwa makamu wa rais wa Sudan Kusini Riek Machar anapokea matibabu ya macho nchini Sudan katika mji mkuu Khartoum, imesema serikali ya Sudan.
Hali ya afya ya Dk Machar sasa imeimarika na atakuwa chini ya uangalizi wa matibabu mpaka atakapoondoka kwenda katika nchi ambayo ni chaguo lake kwa mujibu wa taarifa ya serikali.
Baada ya kufutwa kwenye wadhifa wa Makamu wa rais mwezi Julai, Riek Machar alitangazwa kukimbilia katika nchi salama ya ukanda wa Afrika ya Mashariki wiki iliyopita na msemaji wake, James Gatdet Diak.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |