Jeshi la Nigeria latangaza kumjeruhi kiongozi wa Boko Haram
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa kiongozi wa Boko Haram amejeruhiwa vibaya.
Abubakar Shekau inaaminika kuwa amelengwa na mashambulizi ambayo yamesababisha vifo vingi na jeshi la Nigeria limeeleza kuwa mashambulizi hayo ya anga ni ya aina yake.
Jeshi la Nigeria limetangaza Jumanne kwenye akaunti yake ya Twitter kwamba maafisa wengi wa kundi la Boko Haram wameuawa katika mashambulizi ya anga na kiongozi wa kundi la kigaidi, Abubakar Shekau, amejeruhiwa vikali.
Jeshi la Nigeria linasema kuwa mashambulizi hayo yalifanyika Ijumaa ya wiki iliyopita wakati wa sala katika kijiji cha jimbo la Borno, karibu na msitu maarufu wa Sambisa unaotumiwa na kundi la Boko Haram kama ngome yao kuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |