• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Baadhi ya wanasiasa wa Marekani hawatafanikiwa katika suala la Taiwan kujiunga na mkutano wa afya wa dunia

    • Rais wa Marekani apuuza sayansi katika michezo yake ya kisiasa

    Kampeni ya urais ya Donald Trump ya mwaka 2016 ilivutia vyama vingi kutokana na chuki yake ya wazi dhidi ya sayansi, ikiwemo nadhari ya kuwa na mashaka juu ya chanjo, na madai yake kuwa mabadiliko ya hali ya hewa ni mzaha ulioanzishwa na China.

    • China yaimarisha imani ya jumuiya ya kimataifa katika kukabiliana na COVID-19

    Rais Xi Jinping wa China jana alipohutubia ufunguzi wa mkutano wa 73 wa Afya wa Dunia, alijulisha uzoefu wa China katika kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona, kutoa mapendekezo sita ya kuimarisha juhudi za kupambana na virusi hivyo, na kutangaza hatua tano za kusukuma mbele ushirikiano wa kimataifa. Hotuba hiyo itaimarisha imani ya dunia kushinda virusi hivyo, na kukamilisha mfumo wa usimamizi wa mambo ya kimataifa.

    • Wanasiasa wa Marekani wafanya ubaguzi wa rangi wakati wa janga la COVID-19

    • Marekani yafanya umwamba katika chanjo dhidi ya COVID-19

    Zaidi ya viongozi 140 wa nchi mbalimbali wakiwemo rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, waziri mkuu wa Pakistan Bw. Imran Khan na waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Gordon Brown wameandika barua ya pamoja, wakitaka nchi zote zipate chanjo dhidi ya virusi vya Corona kwa usawa, kama ikitafitiwa na kutengenezwa kwa mafanikio.

    • Viongozi wa Marekani wapaswa kuwajibika na kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Corona duniani
    Hivi karibuni, msomi maarufu wa Marekani Bw. Noam Chomsky ameilaani serikali ya nchi hiyo akieleza kuwa ili kuficha makosa waliyoyafanya kwa Wamarekani, viongozi wa Marekani wametafuta njia ya kuhamisha uwajibikaji wao.
    • Marekani yachukulia mapambano dhidi ya COVID-19 kama ni michezo ya kisiasa

    Gazeti la The Sydney Morning Herald la Australia limetoa ripoti likisema, waraka wenye kurasa 15 uliotolewa tarehe 2 na Gazeti la The Daily Telegraph na kudai chanzo cha virusi vya Corona ni Maabara ya Utafiti wa Virusi ya Wuhan, China, unatokana na habari mbalimbali zisizo sahihi, na kuaminiwa kuwa umetolewa na mwanadiplomasia wa Marekani nchini Australia. Shirika Kuu la Utangazaji la China limetoa tahariri, na kusema Marekani inachukulia mapambano dhidi ya COVID-19 kama ni michezo ya kisiasa.

    • Wanasiasa wa Marekani wanawachukua wananchi kama chombo cha kufanyiwa majaribio

    Mkurugenzi wa zamani wa Idara ya utafiti na maendeleo ya matibabu ya kiikolojia ya Marekani Bw. Rick Bright ameilaani serikali ya Marekani kwa kulazimishwa kutii amri mbele ya mambo ya kisiasa na kuacha kufuata mapendekezo ya wataalamu hodari wa sayansi kwenye serikali wakati inapotoa maamuzi kuhusu mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

    • Mashambulizi yanayofanywa na baadhi ya wanasiasa wa Marekani yatawaharibia wenyewe

    Wakati hali ya maambukizi ya virusi vya Corona ikionesha mwelekeo mzuri huku maisha ya kawaida ya watu yakirejea hatua kwa hatua katika nchi nyingi duniani, Marekani ikiwa nchi pekee inayoongoza duniani inadumisha ongezeko la idadi ya watu walioambukizwa zaidi ya elfu 20 kwa siku, hali ambayo inasikitisha watu.

    • Sekta ya utalii stawi yaonesha kufufuka kwa uchumi wa China

    Takwimu zilizotolewa na Wizara ya Utamaduni na Utalii ya China zinaonesha kuwa, katika siku tano za mapumziko ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Wachina zaidi ya milioni 115 walifanya utalii. Hali hii inaonesha kuwa athari ya mlipuko wa virusi vya Corona ni ya muda mfupi, na uchumi wa China unafufuka kwa haraka.

    • Wanasiasa wanapaswa kuwaacha wanayansi wafanye kazi yao kutafuta chanzo cha virusi

    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw Mike Pompeo, jana, alirudia kauli yake kuhusu "kuwepo kwa ushahidi mwingi unaoonyesha virusi vya Corona vilitoka katika maabara mjini Wuhan", akifumbia macho maelezo ya ofisi ya mkurugenzi wa upelelezi ya Marekani kwamba, "virusi vya Corona havikutengenezwa na bidanamu, wala havitokani na kubadilisha jeni"

    • Wachina bilioni 1.4 wamepambana kishujaa katika kukabiliana na COVID-19

    Leo ni Siku ya Wafanyakazi Duniani. Kutokana na vita dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona, siku hii ina maana tofauti nchini China kwa mwaka huu. Rais Xi Jinping alisema vita hiyo ni ya kiraia, na kusisitiza kuwa kushinda vita hiyo kunategemea wananchi wote wa China. Toka madaktari waliopambana na virusi kwenye mstari wa mbele zaidi, hadi wafanyakazi wanaosambaza vifurushi, mamilioni ya watu wametoa mchango wao kwa ajili ya kushinda vita hiyo, na hao ni mashujaa kweli.

    • Uzoefu wa China kwenye mapambano dhidi ya COVID-19 waonesha sifa nzuri za utamaduni wa taifa la China

    • Mshikamano na ushirikiano ni silaha zenye nguvu zaidi katika kupambana na virusi vya Corona nchini China

    Mlipuko wa virusi vya Corona ulianza ghafla bila kutarajiwa nchini China mwanzoni mwa mwaka 2020, lakini kutokana na uongozi wa rais Xi Jinping wa China, wachina bilioni 1.4 wameshikamana na kusaidiana, na kupata mafanikio muhimu katika kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo mjini Wuhan na nchini China kwa ujumla.

    • Mfumo wa kisiasa umechangia mfanikio ya China katika kudhibiti virusi vya Corona

    Wakati nchi mbalimbali zinajitahidi kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona, China imepata mafanikio muhimu katika kudhibiti maambukizi ya virusi hivyo, ambavyo katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amevielezea kuwa ni utatanishi mkubwa zaidi duniani baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Akieleza maoni yake juu ya mafanikio hayo, mwenyekiti wa Mfuko wa The Kuhn wa Marekani Bw. Robert Lawrance Kuhn amesema, ni kutokana na uongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China CPC, mfumo wa kisiasa wa China na serikali yenye nguvu, China imeweza kukabiliana na ugonjwa huo kwa nguvu, ufanisi na kwa haraka.

    • China yatoa kipaumbele kwa wananchi wakati wa mapambano dhidi ya COVID-19

    Tokea idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona iongezeke kwa zaidi ya elfu 13 kwa siku, hadi kufikia leo tarehe 26 wagonjwa waliotibiwa hospitali mjini Wuhan wote wamepata nafuu, imeonesha ushindi katika vita vya kulinda mji wa Wuhan, vilevile inamaanisha kuwa baada ya juhudi kubwa, wananchi wa China wamepata mafanikio makubwa katika kuzuia na kudhibiti virusi vya Corona kwa ushirikiano.

    • Marekani kushtaki China ni kitendo cha kukwepa wajibu

    Wakati maambukizi ya virusi vya Corona yanaongezeka nchini Marekani, baadhi ya wanasiasa wa nchi hiyo wameishtaki China kwa kisingizio cha kutozuia virusi hivyo kuenea nchi za nje. Shirika Kuu la Utangazaji la China limetoa tahariri na kusema hiki ni kitendo cha kuibebesha China wajibu.

    • Ziara ya rais Xi Jinping mkoani Shaanxi yaonesha nia ya China ya kutimiza lengo la kutokomeza umaskini

    Rais Xi Jinping wa China hivi karibuni alifanya ziara ya ukaguzi mkoani Shaanxi, na kueleza imani yake ya kutimiza lengo la kuondoa umaskini mwaka huu. Kutokana na mpango kazi, China itatokomeza umaskini uliokithiri na kumaliza ujenzi wa jamii yenye maisha bora mwaka huu.

    • Je, kwa nini kampuni za Marekani zinaongeza uwekezaji nchini China wakati wa janga la COVID-19

    Ujenzi wa mradi wa Kampuni ya ExxonMobil ya Marekani nchini China wenye thamani ya dola bilioni 10 za Kimarekani ulizinduliwa rasmi jana. Kabla ya hapo, Kampuni ya Walmart ya Marekani ilitangaza kuongeza uwekezaji wa dola milioni 420 za Kimarekani mjini Wuhan, China. Shirika Kuu la Utangazaji la China (CMG) limetoa tahariri inayosema "Je, kwa nini kampuni za Marekani zinaongeza uwekezaji nchini China wakati wa janga la COVID-19".

    • Uchochezi hautaweza kutingisha uhusiano kati ya China na Afrika

    Hivi karibuni baadhi ya Wamarekani walitunga na kueneza uongo kwamba "Waafrika wanabaguliwa mkoani Guangzhou, China", ili kuchochea uhasama kati ya Afrika na China.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako