• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Makampuni ya China yaendelea vizuri huku yakikabiliwa na changamoto

    Hivi karibuni China ilitoa orodha ya mwaka 2019 ya makampuni yake 500 makubwa zaidi. Ikilinganishwa na mwaka jana, makampuni hayo ya mwaka huu yamepata maendeleo ya kasi zaidi, wakati huo huo, yamepanda juu katika mnyororo wa uzalishaji duniani na kuongeza ushawishi wa kimataifa. Kutokana na utatanishi wa hali ya uchumi nchini China na duniani, ni vigumu kwa makampuni ya China kupata mafanikio hayo.

    • China yabeba wajibu wa usalama wa nyukilia duniani

    Kwa mara ya kwanza, serikali ya China leo imetoa waraka kuhusu shughuli za kuhakikisha usalama wa nyukilia, ambapo imejulisha maendeleo ya shughuli hizo, kanuni na sera za kimsingi, mawazo ya usimamizi na uzoefu wake katika kudumisha usalama wa nyukilia, na kufafanua nia na hatua yake ya kuongeza ushirikiano wa kimataifa na kujenga jumuiya yenye hatma ya pamoja katika usalama wa nyukilia.

    • Uchambuzi: jaribio la Marekani kulihusisha suala la Hong Kong kwenye mazungumzo ya kibiashara kati yake na China litashindikana

    Kwa mara nyingine tena, baadhi ya wamarekani Ijumaa walidai kuwa mazungumzo ya kibiashara kati ya Marekani na China yanahusiana na suala la Hong Kong, lakini mwezi mmoja uliopita, ni watu hawa walisema wazi kuwa "Hong Kong ni sehemu ya China, na wanaweza kushughulikia wenyewe na hawahitaji ushauri."

    • Kupanda ngazi ya mikwaruzano ya kibiashara kutoweza kutatua masuala
    Hivi karibuni baadhi ya wamarekani wametangaza tena kuongeza ushuru dhidi ya bidhaa za China zinazouzwa nchini humo na kusababisha kupamba moto kwa hatari ya mikwaruzano ya kibiashara. Hatua hiyo imeenda kinyume na njia sahihi, na kutosaidia kutatua masuala, na haitasaidia maslahi ya China na Marekani wala maslahi ya watu wa dunia nzima.
    • Makampuni ya Marekani hayataki kuachana na China inayosifiwa kama "Kiwanda cha Dunia"

    Ili kujibu Marekani kutangaza kuongeza ushuru kwa asilimia 10 dhidi ya bidhaa za China zenye thamani ya dola bilioni 300 za kimarekani zinazouzwa nchini Marekani, hivi karibuni China imechukua hatua za kulipiza kisasi. Baadhi ya wamarekani sio tu wamedai kuzidisha hatua za ushuru, bali pia kuyaamrisha makampuni ya Marekani kuondoka nchini China na kutafuta mpango mbadala. Madai hayo yameshangaza wadau wa sekta ya uchumi wa Marekani, na wameyapinga. Nguvu bora ya kipekee ya China inayosifiwa kama "Kiwanda cha Dunia" haiwezi kuachwa na makampuni ya kimataifa yakiwemo ya Marekani.

    • Fimbo ya ushuru ni tishio kubwa kwa ukuaji wa uchumi wa dunia
    • China yaendelea kuwa injini ya mafungamano ya kiuchumi duniani
    China imetangaza orodha mpya kuhusu maeneo ya majaribio ya biashara huria ambayo linahusisha mikoa ya Shandong, Jiangsu, Guangxi, Hebei, Yunnan na Heilongjiang, na hadi sasa idadi ya maeneo ya majaribio ya biashara huria nchini China yamefikia 18. Kwa mara nyingine tena, China imeonesha kwa vitendo halisi kwamba, itasukuma mbele mageuzi na ufunguaji mlango kwa hatua madhubuti, kuelekeza uchumi kupata maendeleo yenye sifa bora, na kuingiza msukumo kwa ajili ya mafungamano ya kiuchumi duniani.
    • Marekani kujiumiza kwa kuiuzia silaha Taiwan

    Wizara ya ulinzi ya Marekani jana iliarifu rasmi bunge kuwa, nchi hiyo inapanga kuiuzia Taiwan ndege 66 za kisasa za kivita aina ya F-16 pamoja na zana nyingine na huduma husika, zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 8. Kitendo hiki kinachokiuka sheria ya kimataifa na kanuni ya kimsingi ya uhusiano wa kimataifa, kuingilia mambo ya ndani ya China, na kukiuka mamlaka na usalama wa China, kinapingwa vikali na China, ambayo itachukua hatua yoyote ya lazima kulinda maslahi yake, ikiwemo kuyawekea vikwazo makampuni ya Marekani yanayoshiriki kwenye mauzo haya ya silaha kwa Taiwan.

    • Uchambuzi: wamarekani kadhaa kukiona cha mtemakuni kwa kauli na vitendo vyao vya kiburi kuhusu Hong Kong

    Tume ya Masuala ya Sheria iliyo chini ya Kamati Kuu ya Bunge la Umma la China leo imesema baadhi ya wabunge wa Marekani wametoa kauli zisizowajibika na kupotosha ukweli wa mambo na kuunga mkono vitendo vya uhalifu vya watu wenye msimamo mkali mkoani Hong Kong, hatua hii ya kuwachanganya watu mioyoni, inalenga kupinga serikali ya China na kuvugura jamii ya Hong Kong.

    • Hila ya kulifanya suala la kibiashara liwe la kisiasa litashindwa

    Makamu wa rais wa Marekani Michael Pence jana alihutubia klabu ya uchumi la Detroit akisema, Marekani inawaheshimu sana watu wa China, na haipendi soko la China lipate hasara. Lakini kama nchi hizo zikifikia makubaliano kuhusu suala la uchumi na biashara, China inatakiwa kufuata ahadi zote, ikiwa ni pamoja na kuheshimu ukamilifu wa sheria za Hong Kong kufutia "taarifa ya pamoja ya China na Uingereza" iliyosainiwa mwaka 1984. Hii ni hila ya Marekani ya kulifanya suala la biashara liwe la kisiasa, na kujaribu kuongeza shinikizo kwa China.

    • China kulinda kithabiti maslahi yake
    • Msukumo mpya wahimiza uchumi wa China kupata maendeleo yenye sifa bora
    Takwimu mpya zilizotolewa na Idara ya Takwimu ya China zimeonesha kuwa, katika miezi saba ya mwanzo mwaka huu, thamani ya nyongeza ya viwanda vya utengenezaji wa teknolojia ya hali ya juu imeongezeka kwa asilimia 8.7 kuliko mmwaka jana wakati kama huu. Pia uwekezaji katika viwanda vya utengenezaji na utoaji wa huduma za teknolojia hiyo umeongezeka kwa asilimia 11.1 na 11.9, hali inayoonesha kuwa msukumo mpya wa uchumi wa China umezidi kuongezeka, imekuwa nguvu muhimu ya kukabiliana na changamoto, na kuhimiza maendeleo ya uchumi yenye sifa bora katika siku za baadaye.
    • Uchumi wa China una uwezo wa kutosha wa kukabiliana na changamoto

    Takwimu zilizotolewa leo na Idara Kuu ya Takwimu ya China zinaonesha kuwa, mwezi Julai uchumi wa China umeendelea kukua kwa kasi inayofaa.

    • Marekani kuiorodhesha China kuwa nchi inayodhibiti kiwango cha safaru yake ni siasa ya kujichukulia maamuzi ya upande mmoja

    Wizara ya Fedha ya Marekani imeiorodhesha China kuwa inadhibiti kiwango cha sarafu yake. Hii sio tu hailingani na vigezo vilivyowekwa na Wizara hiyo vya "nchi inayodhibiti kiwango cha sarafu", bali pia ni siasa ya kujichukulia maamuzi ya upande mmoja na kitendo cha kujilinda kibiashara. Hatua ambayo itaharibu vibaya kanuni za kimataifa na kuleta athari kubwa kwa shughuli za uchumi na fedha duniani.

    • Uchambuzi: Marekani inapaswa kubeba lawama ya kukwama kwa biashara ya mazao ya kilimo kati yake na China

    Tume ya Ushuru wa Forodha ya Baraza la Serikali la China imetangaza kuwa, kuna uwezekano wa kuongeza ushuru kwa mazao ya kilimo ya Marekani yaliyonunuliwa baada ya tarehe 3, Agosti, na kuzitaka kampuni husika za China zisimamishe kununua bidhaa hizo kutoka Marekani. Hatua hiyo imekuja baada ya Marekani kutishia kuongeza ushuru wa asilimia 10 dhidi ya bidhaa za China zinazouzwa nchini Marekani zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 3000 kuanzia tarehe mosi, Septemba.

    • Uchambuzi: China na Marekani hazitafikia makubaliano kama Marekani haitekelezi ahadi zake mara kwa mara
    • Shinikizo halitatatua suala lolote

    Mara baada ya kumalizika kwa duru ya 12 ya mazungumzo ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani, Marekani imeinua tena fimbo ya ushuru kutishia kuongeza asilimia 10 ya ushuru dhidi ya bidhaa za China zenye thamani ya dola bilioni 300 za kimarekani zinazouzwa nchini Marekani. Kitendo hicho kimekiuka vibaya makubaliano ya pamoja yaliyofikiwa katika mkutano wa marais wa nchi hizo mbili huko Osaka, Japan,na hakitasaidia kutatua masuala. China inapinga kithabiti na itachukua hatua ya lazima ili kulinda kithabiti maslahi yake.

    • Kuvunjika kwa Mkataba wa makombora ya masafa ya kati kutaleta tishio la usalama duniani
    Muda wa miezi sita wa utaratibu wa kilichodaiwa na Marekani kujitoa kutoka kwenye Mkataba wa Marekani na Russia kuondoa makombora ya masafa mafupi na ya kati (INF) katika nchi hizo mbili umetimia, ikiashiria kuwa, Mkataba huo wenye umuhimu mkubwa katika kulinda usalama wa dunia umevunjika rasmi kuanzia leo tarehe 2 Agosti. Hatua hii ya Marekani ni kitendo chake kingine cha kutekeleza sera za utaratibu wa upande mmoja, hali itakayopunguza kuaminiana kwa usalama wa kimkakati kati ya nchi kubwa duniani, kuongeza ushindani wa kijeshi, na kuleta matishio mapya kwa utaratibu wa usalama wa dunia.
    • Hadhi ya nchi inayoendelea ya China hairuhusiwi kubatilishwa
    • Uchambuzi: Marekani inakwamisha ushirikiano na maendeleo ya dunia

    Zaidi ya wamarekani mia moja wenye msimamo mkali dhidi ya China, hivi karibuni walimwandikia barua ya pamoja rais Donald Trump wa nchi yao, wakishutumu China kwa kuwashawishi washirika wa Marekani na nchi nyingine kwa mbinu za kiuchumi, ili kupanua ushawishi wake duniani. Ni wazi kuwa kauli hii inakashfu utetezi wa China wa kufanya maendeleo ya uchumi wake kunufaisha dunia nzima, na pia imeonyesha hisia za wivu na chuki ya baadhi ya wamarekani, na ongezeko la nguvu ya kiuchumi ya China. Lakini hali halisi ni kuwa sera ya upande mmoja na ya kujilinda wanayotetea wanasiasa wa Marekani, ndio kizuidi dhidi ya maendeleo ya pamoja kupitia ushirikiano kati ya nchi mbalimbali duniani.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako