• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • China na Marekani zinaweza kutatua mgogoro wao wa kibiashara kama zikifanya mazungumzo kwa usawa

    Marais wa China na Marekani Jumanne walizungumza kwa njia ya simu, wakisema watakutana tena kwenye mkutano wa wakuu wa kundi la G20 mjini Osaka, Japan. Pia wamekubaliana kudumisha mawasiliano kati ya timu za biashara za pande hizo mbili. Habari hii ilituliza kwa kiasi wasiwasi wa watu na kulipa nguvu soko la hisa duniani.

    • Hakuna vikwazo vitakavyozuia hatua ya China ya kufanya uvumbuzi wa sayansi na teknolojia
    Hivi karibuni mshindi wa Tuzo ya Nobel Bibi Tu Youyou na kikundi chake wametangaza matokeo mapya ya utafiti, na kutoa mpango wa kutatua tatizo la usugu wa vimelea vya malaria dhidi ya dawa ya artemisinin. Huu ni mchango mpya unaotolewa na wanasayansi wa China katika kutatua matatizo ya matibabu ya binadamu. Maelfu ya wanasayansi wa China wanaojihusisha kwa bidii katika utafiti wa sayansi na teknolojia ni siri ya China ya kupata maendeleo katika sekta hiyo.
    • Soko la hisa la China lapiga hatua muhimu katika kufungua mlango na nchi za nje
    Utaratibu wa kuunganisha soko la hisa ya Shanghai na la London, umeanzishwa rasmi leo mjini London, ikiwa ni baada ya maandalizi ya miaka minne. Hii ni hatua muhimu kwa soko la hisa la China kutimiza kufungua mlango kwa nchi za nje, hatua ambayo itachangia maendeleo ya masoko ya hisa ya nchi zote mbili za China na Uingereza, na utaratibu huo wa kivumbuzi umeonesha nia na vitendo halisi kwa soko la hisa la China kupanua ufunguaji mlango kwa dunia.
    • Rais Xi Jinping wa China atoa wito wa kujenga mustakabali mzuri wa Asia na dunia nzima
    Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba muhimu kwenye Mkutano wa tano wa viongozi kuhusu ushirikiano na kujenga uaminifu barani Asia CICA huko Dushanbe, Tajikistan, akitoa mapendekezo na msimamo wa China kuhusu jinsi nchi za Asia zitakavyokabiliana na changamoto za pamoja, kujenga Jumuiya ya Asia yenye mustakabali wa pamoja, na kupata mustakabali mzuri katika siku za baadaye.
    • Kujenga jumuiya yenye mustakabali mzuri ya SCO iliyo na uhusiano wa karibu zaidi
    Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba kwenye Mkutano wa 19 wa Baraza la viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai SCO uliofanyika jana, akitoa wito wa kuijenga jumuiya hiyo iwe jumuiya yenye mustakabali wa pamoja ambayo wanachama wake wanashirikiana na kuaminiana, kukabiliana na changamoto kwa pamoja, kusaidiana na kunufaishana, kusikilizana na kufundishana, na kuwa na uhusiano wa karibu zaidi. Hayo ni mapendekezo yaliyotolewa na rais Xi Jinping wa China kuhusu maendeleo ya jumuiya hiyo baada ya mkutano wa viongozi wa jumuiya hiyo iliyofanyika mwaka jana mjini Qingdao, hatua ambayo imeonesha uungaji mkono wa China kwa jumuiya hiyo.
    • Kuivuruga Hongkong hakutaleta faida yoyote kwa pande zote
    Hivi karibuni baadhi ya wabunge wa Marekani walitaja "Sheria kuhusu haki za binadamu na demokrasia ya Hong kong" ambayo iliwekwa kando, wakiitaka serikali ya Marekani ithibitishe hali ya kujitawala kwa Hong Kong kila mwaka, ili kuamua kama itaendelea kuipa Hong Kong haki maalumu ikiwa eneo huru la ushuru wa forodha kwa kufuata Sheria ya Sera ya Marekani-Hongkong ya mwaka 1992. Kuingilia kwa nguvu kwa baadhi ya wanasiasa mambo ya ndani ya China, kumeonesha vya kutosha jaribio la Marekani la kuzuia maendeleo ya China na kuiwekea vikwazo kwa pande zote. Lakini watu wenye busara wanatambua kwamba, vitendo hivyo havitaleta faida yoyote kwa pande zote.
    • Uhusiano kati ya China na Russia waingia katika zama mpya
    Rais Xi Jinping wa China ambaye yupo Moscow, amesaini taarifa mbili muhimu za pamoja na rais Vladimir Putin wa Russia, wakitangaza kukuza uhusiano wa kiwenzi na ushirikiano wa kimkakati wa pande zote kati ya pande hizo mbili katika zama mpya, na kushirikiana katika kuimarisha utulivu wa kimkakati duniani.
    • Kauli ya Marekani kwamba imepata hasara katika biashara kati yake na China haina msingi
    Wizara ya biashara ya China leo imetangaza ripoti ya utafiti kuhusu faida inayopata Marekani katika ushirikiano wa kibiashara kati yake na China, ikionesha hali halisi na chanzo cha urari mbaya wa biashara kwa Marekani, lakini pia inaonesha kuwa Marekani imepata faida kubwa kutokana na ushirikiano wa biashara kati yake na China, na ingawa China ina urali mzuri wa biashara, lakini pande zote mbili zinanufaika, na kwamba kauli kuwa Marekani ni upande unaopata hasara haina msingi.
    • China yaingia katika zama ya matumizi ya kibiashara ya teknolojia ya 5G kwa njia ya kufungua mlango na kunufaishana
    Wizara ya viwanda na TEHAMA ya China leo imetangaza kutoa leseni kuhusu matumizi ya kibiashara ya teknolojia ya 5G kwa makampuni manne ya mawasiliano ya simu yakiwemo China Mobile, China Telecom, China Unicom na Mtandao wa Matangazo wa China (China Broadcast Network). Hatua hii imeonesha kuwa China imefungua rasmi zama ya matumizi ya kibiashara ya teknolojia ya 5G, na kuwa soko kubwa zaidi la teknolojia hiyo duniani litakalotoa fursa nyingi mpya, kuhimiza mageuzi mapya ya viwanda, kutoa huduma mpya kwa maisha ya wananchi, na kuongoza ukuaji wa uchumi duniani.
    • Mazingira yenye usalama na urafiki ni njia pekee inayowavutia watalii wa China
    Wizara ya mambo ya nje ya China leo imetoa tahadhari ya usalama kuhusu kwenda nchini Marekani ikisema, kutokana na idara za sheria za Marekani kuwasumbua mara nyingi raia wa China kupitia ukaguzi wa kuingia na kutoka nchini humo na mahojiano, hivyo wizara hiyo inawakumbusha raia wa China wanaoenda Marekani na matawi ya mashirika ya China nchini Marekani kuinua kiwango cha wazo la usalama. Wizara ya utamaduni na utalii ya China pia imetoa tahadhari ya kwenda kutalii nchini Marekani ikisema, kutokana na ongezeko la matukio ya ufyatuliaji wa risasi, uporaji na wizi nchini Marekani, wizara hiyo inawakumbusha watalii wa China kutathmini hatari ya kutalii nchini Marekani.
    • Uhusiano kati ya China na Russia kupata maendeleo mapya kwenye kipindi kizuri zaidi katika historia
    Rais Xi Jinping wa China leo ameondoka kwenda Russia kwa ziara rasmi nchini humo na kuhudhuria mkutano wa 23 wa Baraza la Uchumi Duniani la St. Petersburg. Huu ni mwaka wa 70 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kibalozi kati ya China na Russia, pande hizo mbili zimeeleza mara nyingi kuwa, uhusiano kati yao uko katika kipindi kizuri zaidi kwenye historia. Ziara ya rais Xi inayofanyika katika wakati huo muhimu itahimiza uhusiano kati ya pande hizo mbili kwenye kiwango cha juu zaidi na kupata maendeleo makubwa zaidi.
    • China yatoa tahadhari kwa wanafunzi wanaotaka kusoma nchini Marekani

    Wizara ya elimu ya China leo imetoa tahadhari ya kwanza ya mwaka 2019 ikisema, kutokana na kuzuiwa kwa visa za baadhi ya wachina wanaoenda kusoma Marekani, muda wa ukaguzi wa visa kuongezeka, muda wa visa kufupishwa na kiwango cha kukataliwa maombi ya visa kuongezeka, wanafunzi wa China wanaotaka kwenda kusoma nchini Marekani au kumaliza masomo yao nchini humo wanakabiliwa na athari kubwa. Wizara hiyo inawakumbusha wanafunzi na wasomi wengi kuimarisha tathmini ya hatari kabla ya kwenda kusoma nchini Marekani, kuongeza wazo la kujikinga na hatari na kujiandaa vizuriā€¦. Ana maelezo zaidi.

    • Jaribio la kuzuia soko kubwa lenye idadi ya watu bilioni 1.4 kamwe halitafanikiwa
    Hivi karibuni makampuni mengi yametangaza kwa kauli kwamba yamesimamisha ushirikiano na Kampuni ya Huawei ni uvumi, hali ambayo imeonesha kuwa hatua ya Marekani ya kudhibiti uuzaji wa bidhaa wa Kampuni ya Huawei, imeharibu maslahi ya makampuni mengi ya nchi za nje yakiwemo yale ya Marekani, na haiungwi mkono na wananchi wake. Jaribio la baadhi ya wanasiasa wa Marekani la kuwekea vizuizi dhidi ya soko kubwa la China lenye idadi ya watu bilioni 1.4 halitafanikiwa.
    • Hatua ya Marekani ya kuongeza ushuru kwa bidhaa za China haishinikiza makampuni ya kimataifa nchini China
    Hivi karibuni Marekani imesema kutokana na hatua yake ya kuongeza ushuru kwa bidhaa za China, baadhi ya makampuni yatahamisha viwanda vyao kutoka China hadi Vietnam na nchi nyingine barani Asia, na baadhi ya makampuni ya Marekani yatarejea nchini humo. Kauli hizo zimekiuka kanuni za kawaida za uchumi za soko huria, na zimetungwa kwa makusudio na Marekani.
    • Mitaji ya kimataifa ina imani na soko kubwa la China

    Takwimu zinaonesha kuwa kutoka mwezi wa Januari hadi Aprili mwaka huu, China imetumia mitaji ya kigeni ya dola bilioni 44.2 za kimarekani, ambayo inaongezeka kwa asilimia 6.4 ikilinganishwa na mwaka jana. Uwekezaji kutoka vyanzo vikuu vya Korea Kusini, Marekani na Ujerumani umeongezeka kwa asilimia 114.1, 24.3 na 101.1 mtawalia. Vituo vikuu vya kikanda na vituo vya utafiti vya makampuni 27 ya kimataifa vimeanzishwa jijini Shanghai, ambako mitaji ya kigeni iliyotumiwa katika robo ya kwanza ya mwaka huu imeongezeka kwa asilimia 20.3 ikilinganishwa na mwaka jana. Katika mkoa wa Hainan ambayo ni eneo maalumu la kiuchumi lenye eneo kubwa zaidi nchini China, mitaji ya kigeni iliyotumiwa imeongezeka mara 20 hivi kwenye miezi minne ya mwanzo ya mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana.

    • Marekani ni chanzo kikuu cha nakisi duniani

    "Kutoa shutuma zisizo na msingi" ni njia ya kawaida inayotumiwa na Marekani kushambulia washindani wake. Kwa mfano, kabla ya kufanyika kwa duru ya 11 ya mazungumzo ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani, Marekani ilitoa shutuma zisizo na msingi kwamba China imerudi nyuma katika mazungumzo hayo, na kuzitumia kama kisingizio cha kuongeza ushuru dhidi ya bidhaa za China zinazouwa kwa Marekani.

    • China yafanya maandalizi kwa pande zote katika kukabiliana na mgogoro wa kibiashara na Marekani
    Baada ya Marekani kuongeza ushuru dhidi ya bidhaa za China zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 200 zinazouzwa nchini humo kutoka asilimia 10 hadi 25, imetishia tena kuanzisha utaratibu wa kuongeza ushuru kwa asilimia 25 kwa bidhaa nyingine za China zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 325, na kutangaza orodha za bidhaa hizo hivi karibuni. Wakati huo huo, raundi ya 11 ya mazungumzo ya ngazi ya juu ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani imemalizika, na pande mbili zimekubaliana kuendelea na mazungumzo.
    • Hatua ya Marekani ya kuongeza ushuru kwa bidhaa za China yaathiri maslahi ya China na pia kujiharibu
    Marekani imetangaza kuongeza ushuru kwa bidhaa za China zinazouzwa nchini humo zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 200 kutoka asilimia 10 hadi asilimia 25 kuanzia leo saa sita na dakika 1 kwa saa za hapa Beijing, huku China ikitangaza hatua ya kuijibu siku hiyo hiyo saa sita na dakika 3 kwa saa za Beijing.
    • Mazungumzo pamoja na makabiliano huenda yatakuwa hali ya kawaida katika migogoro ya kibiashara kati ya China na Marekani
    Ofisi ya Mwakilishi wa Biashara wa Marekani Jumatano ilitangaza kupanga kuinua kiwango cha ushuru wa forodha dhidi ya bidhaa za China zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 200 hadi asilimia 25 kutoka asilimia 10 ya awali, hatua ambayo itatekelezwa kuanzia Mei 10. Kuhusu uamuzi huo wa Marekani, China imetoa taarifa ikisema kuongeza mgogoro wa kibiashara kati ya pande hizo mbili hakuendani na maslahi ya watu wa nchi hizo mbili na dunia nzima, China imesikitishwa na uamuzi huo, na kama Marekani ikitekeleza hatua hiyo, China italazimika kuchukua hatua za lazima za kujibu.
    • Kujaribu kuibana China kwa suala la Taiwan hakika ni njia isiyopitika
    Baraza la Wawakilishi la Marekani Jumanne tarehe 7 lilipitisha "Sheria ya Uhakikisho ya Taiwan ya Mwaka 2019" na "Kurudia tena ahadi ya Marekani kwa Taiwan na kwa utekelezaji wa 'Sheria ya Uhusiano na Taiwan'". Hii ni mara nyingine kwa Marekani kuingilia ovyo masuala ya ndani ya China kwa kutumia suala la Taiwan, ambayo ni hatua ya kisiasa yenye hatari kubwa inayolenga kuzuia maendeleo ya amani ya China.
    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako