8. Mkutano wa hali ya hewa wa Madrid waweka msingi wa kufikia makubaliano
Takwimu mpya zilizotolewa mwezi Desemba na Shirika la Hali ya Hewa Duniani WMO zinaonyesha kuwa, kiasi cha gesi ya ukaa GHG katika hewa ya dunia kimefikia kiwango cha juu zaidi, na matukio ya dhoruba, ukame, mafuriko, moto wa misituni yanayosababishwa na hali hiyo yanatokea mara kwa mara. Mkutano wa 25 wa pande zilizosaini mkataba wa Umoja wa mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi uliofanyika mjini Madrid, Hispania, na kupitisha maamuzi zaidi 30 na kuweka mpango kwa ajili ya utekelezaji wa taratibu za kisoko katika mkataba wa Paris. Ingawa matokeo ya mkutano huo hayakufikia malengo yaliyotarajiwa, lakini yameweka msingi kwa pande mbalimbali kufikia makubaliano katika kipindi kijacho.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |