10. Kanisa la Notre Dame la Paris laungua kufuatia moto mkubwa
Kanisa la Notre Dame la Paris nchini Ufaransa liliungua baada ya moto mkubwa uliotokea tarehe 15 Aprili. Tukio hilo lilisababisha jumuiya ya kimataifa kufuatilia namna ya kuhifadhi, kulinda na kukarabati urithi wa utamaduni duniani. Mwezi Novemba, China na Ufaransa zilisaini nyaraka za ushirikiano hapa Beijing kuhusu wataalamu wa China kushiriki kwenye kazi ya ukarabati wa kanisa hilo. Kwenye mkutano wa 43 wa kamati ya urithi wa dunia uliofanyika mwezi Julai, katibu mkuu wa Shirika la elimu, sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO Bw. Audrey Azoulay amesema, pande mbalimbali zinapaswa kuimarisha ushirikiano na mazungumzo, ili kuhifadhi urithi wa binadamu wote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |