9. Eneo la biashara huria la Afrika AfCFTA lazinduliwa
Mkutano maalumu wa eneo la biashara huria la Afrika AfCFTA la Umoja wa Afrika ulifanyika tarehe 7 Julai huko Niamey, Niger, na kutangaza kuzinduliwa kwa eneo hilo ambalo litaanza kufanya kazi rasmi mwezi Julai mwaka kesho. Kuzinduliwa kwa eneo hilo kunaonyesha maendeleo makubwa ya mchakato wa mafungamano ya Afrika. Eneo la AfCFTA litasaidia kuhimiza uwezo wa kujiendeleza kwa Afrika, kujenga soko kubwa lenye GDP kiasi cha kimarekani trilioni 2.5 ambalo litanufaisha watu bilioni 1.3, kuisaidia Afrika kuboresha mazingira ya maendeleo, na kutimiza mapema maendeleo ya viwanda na maendeleo endelevu ya kujitegemea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |