Rais Xi Jinping wa China jana mjini Cairo alitoa hotuba kwenye makao makuu ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na kueleza sera ya China kuhusu Mashariki ya Kati. Akiwahutubia viongozi mbalimbali wa mashirika na nchi za Mashariki ya Kati akiwemo katibu mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu Bw. Nabil el-Araby jana kwenye makao makuu ya Jumuiya hiyo.
Ziara ya rais wa China Mashariki ya Kati kulenga mchango wa China katika amani ya kanda hiyo Rais Xi Jinping wa China leo anaanza ziara ya siku tano katika nchi tatu za Mashariki ya Kati, itakayomfikisha Saudi Arabia, Misri na Iran. Mbali na mambo ya ushirikiano kati ya pande mbili, ziara yake pia inatarajiwa kuangalia mchango wa China katika kuhimiza amani na maendeleo katika eneo la Mashariki ya Kati.