• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Tuna mengi ya kujifunza China, makamu wa Rais wa Tanzania asisitiza 2020-01-21

    MAKAMU wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema nchi hiyo ya Afrika Mashariki ina mambo mengi ya kujifunza kutoka kwa China katika juhudi zake za kuboresha maisha ya watu na kufanya Mageuzi makubwa ya kiuchumi.

    • Balozi Kairuki ashauri namna ya kutatua changamoto za biashara kwa njia ya mtandao 2020-01-17

    HUKU uwekezaji na biashara kati ya China na Tanzania ukiizidi kukua na kuimarika siku hadi siku, Balozi wa Tanzania jijini Beijing Mbelwa Kairuki ameshauri wafanyabiashara wa pande zote mbili kuwa makini hasa katika biashara kwa njia ya mtandao ili kuepuka changamoto za kuibiwa au kutapeliwa.

    • Rais Magufuli aielekeza kampuni ya CRJE ya China kumaliza kazi kwa wakati 2020-01-17

    RAIS wa Tanzania Dkt. John Magufuli Jumamosi, Januari 11, 2020 aliweka jiwe la msingi la shule ya Sekondari ya Mwanakwerekwe iliyopo Zanzibar inayojengwa na Kampuni ya China Railway Jianchang Engineering Company Limited (CRJE).

    • Rais Shein wa Zanzibar afungua shule iliyojengwa na kampuni ya China 2020-01-09

    RAIS wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein Jumatatu, Januari 6, 2019, ameshiriki hafla ya ufunguzi wa shule ya sekondari ya Mwembeshauri iliyojengwa na Kampuni ya Group Six International Limited kutoka China.

    • Balozi Kairuki aanika mikakati kuimarisha ushirikiano China, Tanzania 2020 2019-12-31

    UBALOZI wa Tanzania nchini China umeelezea mipango na mikakati yake ya kuendelea kuvutia wawekezaji na watalii kutoka China pamoja na namna ya kutafuta masoko zaidi kwa bidhaa za Tanzania mwaka 2020

    • Kampuni ya China kujenga makao makuu ya Umoja wa Posta Afrika 2019-12-31

    SERIKALI ya Tanzania imesaini mkataba na kampuni ya Beijing Construction Engineering Group kwa ajili ya ujenzi wa makao makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU).

    • China yaahidi kusaidia kutatua changamoto uendeshwaji reli ya Tazara 2019-12-23

    MIAKA zaidi ya 40 sasa baada ya China kufadhili ujenzi wa reli ya Tazara inayounganisha Tanzania na Zambia, nchi hiyo ya Asia ya Mashariki imeahidi kuwa iko tayari kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili uendeshwaji wa reli hiyo.

    • Rais wa Tanzania azindua ujenzi wa daraja linalojengwa na kampuni za China 2019-12-10

    RAIS wa Tanzania Dkt. John Magufuli Jumamosi, Desemba 7, 2019, aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Kigongo – Busisi linalojengwa na China Civil Engineering Construction Corporation Group na China Railway 15th Bureau Group Co. Ltd za nchini China.

    • Wajasiriamali EAC wafaidika na mafunzo ya biashara China 2019-11-26

    MAONESHO ya wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imewezesha wafanyabiashra hao wadogo kutembelea China kujifunza namna bora ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi.

    • Madaktari bingwa wa moyo kutoka Fuwai Hospital-China kuwasili Tanzania 2019-11-26

    USHIRIKIANO wa China na Tanzania katika sekta ya afya unazidi kuimarika siku baada ya siku huku timu ya madaktari bingwa wa Moyo kutoka Fuwai Hospital ya nchini China wakitarajiwa kuwasili katika nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki Novemba 28, mwaka huu 2019.

    • China kutoa $ 42.6M ujenzi makao makuu ya ulinzi Tanzania 2019-11-26

    SERIKALI ya Jamhuri ya Watu wa China imetenga jumla ya Dola za Kimarekani Milioni 42.6 (Yuan Milioni 300) kwa ajili ya ujenzi wa makao makuu ya ulinzi jijini Dodoma, Tanzania.

    • Wajasiriamali EAC wafaidika na mafunzo ya biashara China 2019-11-25

    MAONESHO ya wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imewezesha wafanyabiashra hao wadogo kutembelea China kujifunza namna bora ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi.

    • Madaktari bingwa wa moyo kutoka Fuwai Hospital-China kuwasili Tanzania 2019-11-25

    USHIRIKIANO wa China na Tanzania katika sekta ya afya unazidi kuimarika siku baada ya siku huku timu ya madaktari bingwa wa Moyo kutoka Fuwai Hospital ya nchini China wakitarajiwa kuwasili katika nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki Novemba 28, mwaka huu 2019.

    • Idadi ya wanafunzi wanaosoma Kichina Chuo Kikuu Cha Dodoma yaongezeka 2019-11-22

    IDADI ya wanafunzi wanaosoma lugha ya Kichina katika Chuo Kikuu cha Dodoma imeongezeka kutoka mwanafunzi mmoja mwaka 2016 kozi hiyo ilipoanzsishwa hadi kufikia zaidi ya 100 mwezi Novemba, mwaka huu, 2019.

    • Madaktari toka China waendesha zoezi la upimaji afya Zanzibar 2019-11-07

    TIMU ya madaktari bingwa kutoka Jamuhuri ya watu wa China, wakishirikiana na madaktari Wazalendo wa Zanzibar wameendesha zoezi la upimaji wa Afya kwa wazee wanaoishi katika nyumba za Wazee Sebleni na Welezo visiwani humo na kutoa huduma za uchunguzi, dawa na ushauri.

    • Rais wa Zanzibar aahidi kuendelea kuthamini uhusiano na China 2019-11-07

    ZANZIBAR itaendelea kuthamini uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na China sambamba na Chama chake cha Kikomunisti cha (CPC).

    • Sera za Tanzania kuhusu China hazijabadilika, Rais Magufuli asisitiza 2019-10-24

    RAIS wa Tanzania Dkt. John Magufuli ameihakikishia Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kuwa sera za nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki kuhusu China hazijabadilika.

    • Miradi ya ujenzi inayotekelezwa na makampuni ya China nchini Tanzania yafika Dola Bilioni 17 2019-10-23

    MAKAMPUNI kutoka China yametekeleza miradi ya ujenzi nchini Tanzania yenye jumla ya Dola za Kimarekani Bilioni 17 (zaidi ya Shilingi Trilioni 39 za Tanzania) na kufanya nchi hiyo ya Asia ya Mashariki kushika nafasi ya kwanza katika kutekeleza miradi ya ujenzi nchini humo.

    • Watanzania waliosoma China waazimia kuvutia wawekezaji 2019-10-23

    JUMUIYA ya Watanzania waliosoma China (CAAT) hivi karibuni kiliazimia kuwa kiunganishi kati ya Tanzania na China -- kushawishi wawekezaji kutoka nchi hiyo ya Asia ya Mashariki kuwekeza Tanzania.

    • China yakabidhi jengo la Dola Milion 22 kwa Serikali ya Tanzania 2019-10-15

    SERIKALI ya Jamhuri ya Watu wa China imekabidhi jengo jipya lenye gharama ya Dola za Kimarekani Milioni 22 (sawa na Shilingi Bilioni 50 za Tanzania) kwa Serikali ya Tanzania.

    • Zanzibar yaahidi kuimarisha ushirikiano na China National Research Institute of Food & Fermentation Industries 2019-10-08

    SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesisitiza kuwa itazidi kupanua wigo wa ushirikiano kati yake na China National Research Institute of Food & Fermentation Industries katika suala la upatikanaji wa mafunzo kwa watendaji wake kupitia sekta tofauti.

    • Rais Magufuli, Museveni wafurahishwa na kampuni ya ujenzi ya China 2019-09-09

    MARAIS wa Tanzania na Uganda Dkt. John Magufuli na Yoweri Museveni wameipongeza kampuni ya China Railway Jianchang Engineering (CRJE--East Africa Ltd) kwa kukamilisha ujenzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa viwango na ubora wa kimataifa.

    • China inavyohimiza ushirikiano wa kiutamaduni kupitia utengenezaji, unywaji wa chai 2019-09-09

    KATIKA jitihada zake za kueneza utamaduni wake barani Afrika, China --nchi yenye idadi kubwa ya watu duniani, imeanza kutangaza na kueneza 'utamaduni wa unywaji chai' nchini Tanzania.

    • Wachina washauriwa kuwekeza zaidi Tanzania kufaidika na fursa EAC, SADC 2019-09-06

    TANZANIA kupitia Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZA) imewakaribisha wawekezaji kutoka China kuwekeza nchini humo wakati huu ambapo Serikali inalenga kufanya nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki kuwa kitovu cha viwanda kutokana na faida iliyo nayo ya kijiografia.

    • Kampuni ya China yazindua kiwanda cha kuchakata betri za magari Tanzania 2019-08-29

    KAMPUNI ya Huatan Investment Group Limited ya nchini China siku ya Jumanne, Agosti 27, 2019, imezindua kiwanda cha kuchakata betri za magari zilizotumika nchini Tanzania.

    • Waandishi wa habari Zanzibar Waadhimisha miaka 70 ya Taifa la China 2019-08-19
    • Afisa ubalozi wa China ashauri vijana Tanzania kushiriki mchezo wa Wushu 2019-08-16

    MSIMAMIZI wa Kituo cha Utamaduni katika Ubalozi wa China nchini Tanzania Bw. Gao Wei ameshauri vijana wa Tanzania kushiriki katika mchezo wa Wushu akieleza kuwa itawasiadia kujijengea uwezo wa kujiamini na kushauri pia vyombo vya ulinzi kutumia mchezo huo kuwaongezea uzoefu zaidi .

    • Tanzania, kampuni mbili za China zatiliana saini mradi wa Daraja Ziwa Victoria 2019-08-05

    SERIKALI ya Tanzania, Jumatatu, Julai 29, 2019 jijini Dar es Salaam imetiliana saini na kampuni za China Civil Engineering Construction Corporation na China Railway 15th Bureau Group kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi katika Ziwa Victoria mkoani Mwanza.

    • Kampuni ya CHICO kujenga barabara ya kuunganisha Tanzania, Kenya 2019-08-01

    KAMPUNI ya ujenzi ya China Henan International Corporation Group Co. Ltd (CHICO) Jumatano, Julai 31, 2019 wilayani Pangani, Mkoa wa Tanga imetiliana saini na Serikali ya Tanzania kutekeleza mradi wa ujenzi wa kipande cha barabara itakayounganisha Tanzania na Kenya.

    • Wafanyabiashara Tanzania kufanya ziara ya mafunzo China 2019-07-29

    HUKU uhusiano wa kibishara na uwekezaji ukizidi kukukua na kuimarika kati ya Tanzania na China, wafanyabiashara kutoka Mkoani Mtwara, kusini mwa nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki, wanatarajia kutembelea China hivi karibuni ili kujifunza fursa mbalimbali za kibiashara zikiwemo za uwekezaji wa viwanda ili kuendana na kasi ya Tanzania ya viwanda.

    1  2  3  4  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako