• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Mgonjwa wa kwanza wa Ebola mjini Goma DRC afariki dunia 2019-07-17

    Mgonjwa wa kwanza wa Ebola mjini Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) amefariki dunia. Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Carly Nzanzu amesema, mtu huyu alifariki jana njiani wakati akipelekwa Butembo kwa matibabu kwenye kituo cha matibabu ya Ebola.

    • China na Afrika zashirikiana kutoa pendekezo la "kuhimiza na kulinda haki za binadamu kwenye maendeleo" 2019-07-10
    Mkutano wa 41 wa baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa umefanyika hivi karibuni ambapo wajumbe wa kudumu wa China na wa nchi za Afrika walikutana kando ya mkutano huo na kupendekeza kwa pamoja wazo la "kuhimiza na kulinda haki za binadamu kwenye maendeleo".
    • Rais Kenyatta azindua Taasisi ya mafunzo ya baharini mjini Mombasa 2019-07-09

    Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta jumatatu alizindua Chuo cha Mafunzo ya Baharini mjini Mombasa kwa lengo la kukidhi mahitaji ya mabaharia nchini humo. Chuo hicho cha Bandari cha mafunzo ya masuala ya baharini kinatoa mafunzo ya kipekee ya ubaharia, na kimeanzishwa kama sehemu ya mageuzi ya sekta ya usafiri wa baharini. Kupitia chuo hicho, serikali ya Kenya inatarajia kuziba pengo kubwa lauhaba wa mabaharia waliohitimu nchini Kenya na katika kanda ili kukidhi mahitaji ya sekta inayoibuka ya uchumi wa majini. Pia chuo hicho kitatoa elimu ya juu na mafunzo kwa wanafunzi watakaofuzu vizuri, ambao watapata shahada za diploma na vyeti.

    • Umoja wa Afrika kutoa heshima kwa rais wa zamani wa Zambia Kaunda kwenye mkutano wa kilele wa mwaka 2020 2019-07-02

    Umoja wa Afrika unapanga kutoa heshima kwa rais wa kwanza wa Zambia, Kenneth Kaunda, kwenye mkutano wa kilele wa Umoja huo utakaofanyika mwezi Februari mwaka 2020.

    • Tanzania yakaribisha kampuni za China kuwekeza nchini humo 2019-06-29

    Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania Bw. Palamagamba John Kabudi, amesema Tanzania inakaribisha kampuni za China kuwekeza nchini humo, na kushirikiana katika kutekeleza pendekezo la "Ukanda Mmoja, Njia Moja".

    • China itatimiza ahadi zote ilizotoa kwa Afrika 2019-06-28

    Rais Xi Jinping wa China amesema nchi yake itatimiza ahadi zote ilizotoa kwa Afrika kwa kushikilia kanuni za udhati, matokeo halisi, udugu na nia njema pamoja na wazo sahihi la thamani kuhusu urafiki, haki na maslahi ya pamoja katika uhusiano kati ya pande hizo mbili.

    • Rwanda yapokea toka Ulaya faru weusi watano walio hatarini kutoweka
     2019-06-24

    Faru watano walio kwenye hatari kubwa ya kutoweka wamepokelewa na Rwanda kutoka Ulaya. Kwa mujibu wa Bodi ya maendeleo ya Rwanda faru hao watatunzwa katika mbuga ya taifa ya Akagera, iliyoko mashariki mwa Rwanda.

    • Kenya kutuma maafisa wa ngazi ya juu kwenye maonesho ya Changasha 2019-06-19
    Waziri wa biashara wa Kenya Peter Munya amasema ataongoza ujumbe wan chi hiyo kushiriki kweye maonesho ya kwanza ya kiuchumi na biashara kati ya China na Afrika yatakayofanyika mjini Changsha katika mkoa wa Hunan nchini China.
    • Rais wa Zimbabwe aipongeza kampuni ya China kwa kufikia hatua nzuri kwenye ujenzi wa jengo jipya la bunge 2019-06-14

    Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ametembelea jengo jipya la Bunge linalojengwa na kampuni ya ujenzi ya China ya Shanghai Construction Group, na kueleza kuridhishwa na hatua nzuri iliyofikiwa hadi sasa.

    • Uganda yawahakikishia watalii licha ya kugunduliwa kwa ugonjwa wa Ebola
     2019-06-12

    Serikali ya Uganda imewahakikishia watalii kuwa hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kufuatia mlipuko wa homa ya Ebola kuripotiwa nchini Uganda.

    • China yatoa msaada wa dharura wa chakula kwa Kenya
     2019-06-11

    Balozi wa China nchini Kenya Bw. Wu Peng jana alitangaza kuwa, serikali ya China imetoa msaada wa chakula wenye thamani ya dola milioni 11.6 za kimarekani kwa Kenya, ili kuisaidia nchi hiyo kukabiliana na ukame ambao ni mbaya zaidi tangu miaka 38 iliyopita.

    • China yakabidhi rasmi hospitali ya Rufaa ya Chuo Kikuu cha Kenyatta kwa serikali ya Kenya 2019-05-27

    Hospitali ya Mafunzo, Rufaa na Utafiti, ya Chuo Kikuu cha Kenyatta ilikabidhiwa rasmi kwa serikali ya Kenya mnamo ijumaa tarehe 25 Mei.

    • Wanahabari wa Uganda wachukua hatua kuokoa mazingira, Uganda 2019-05-14

    Sasa tuelekee Magahribi mwa Uganda amabako wandishi wa habari katika aneo la Bunyoro wameamua kuchukua hataua ya kivitendo kuchagiza juhudi za serikali za uhifadhi nwa mazingira ambazo pia zimethaminiwa katika Malengo ya Maendelleo Endelevu (SDGS).

    • Chama tawala cha ANC cha Afrika Kusini chashinda katika uchaguzi mkuu 2019-05-12

    Tume huru ya uchaguzi ya Afrika Kusini imetangaza matokeo ya upigaji kura, na chama tawala cha ANC kimeshinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2019.

    • Zoezi la kuhesabu kura Afrika Kusini laendelea huku ANC kikiongoza kwa asilimia 57 2019-05-11

    Hadi kufikia Ijumaa mchana asilimia 91 ya kura zilikuwa zimeshahesabiwa Afrika Kusini huku chama tawala ANC kikiongoza mbio hizo za uchaguzi kwa asilimia 57.56 ya kura.

    • Mradi wa China wa mfumo wa televisheni wa digitali wanufaisha wananchi wa Uganda 2019-05-02
    Takriban nchi 16 barani Afrika zinaripotiwa kukamilisha mradi wa serikali ya China wa kuhakikisha kwamba vijiji 10,000 barani Afrika vinafaidika na uhamiaji kutoka mfumo wa runinga wa analogia kwenda digitali bure bila malipo.
    • Wananchi wa Uganda wanufaika na msaada wa madaktari kutoka China 2019-04-30
    Msaada wa matibabu wa China barani Afrika una historia ndefu.Mwaka 1963 China ilituma madaktari 100 nchini Algeria baada ya kupata uhuru kutoka kwa Ufaransa. Hata hivyo kiwango cha misaada ya kimatibabu kimekuwa kikiongezeka katika nchi mbalimbali kadri siku zinavyosonga. Uganda ni mojawapo ya nchi zinazonufaika na msaada wa madaktari kutoka China kwa zaidi ya miongo mitatu sasa. Msaada huu umewawezesha maelfu ya wananchi wa Uganda kupata matibabu maalum kutoka kwa wataalamu wa magonjwa mbalimbali kutoka China.
    • Rais Xi Jinping wa China akutana na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta 2019-04-27
    Katika mkutano wao rais Xi amesema hii ni mara ya tatu kukutana na rais Kenyatta ndani ya mwaka mmoja, ambayo inaonyesha uhusiano wa kimkakati wenye kiwango cha juu kati ya nchi mbili. Amesema China inampongeza rais Kenyatta kwa kupinga shutuma zisizo na msingi wowote juu ya ushirikiano wa China na Afrika ikiwemo Kenya.
    • Vifaa na teknolojia ya China vyarahisisha kazi za utafiti wa maji na samaki Tanzania 2019-04-26
    Katika mfululizo wetu wa ripoti za ushirikiano wa wasomi wa China na Afrika leo tunaelekea kule nchini Tanzania ambapo taasisi ya jiografia na limnolojia ya Nanjing kutoka China imesaidia ile ya utafiti wa uvuvi nchini humo kwa vifaa vya maabara na hiyo kuendeleza uchunguzaji wa ubora wa maji na samaki. Ronald Mutie anaripoti.
    • Ushirikiano wa China na Tanzania katika utunzaji wa ziwa Tanganyika 2019-04-25

    Kwenye mfululizo wetu wa ripoti kuhusu ushirikiano wa China na Tanzania mwandishi wetu Ronald Mutie anaripoti kuhusu ushirikiano kati ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi ya Tanzania Tafiri na taasisi ya jigrafia na nimnolojia ya China (Niglas).

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako