• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Nchi za Afrika zafurahia misaada ya China katika kukabiliana na COVID-19
     2020-04-19

    Hivi karibuni, licha ya vikundi vya madaktari vilivyotumwa na China katika nchi za Afrika, misaada ya vifaa vya matibabu dhidi ya ugonjwa wa COVID-19 iliyotolewa na China pia imefurahiwa na nchi za Afrika.

    • Waziri wa mambo ya nje Nigeria: Baadhi ya raia wa Nigeria walioko Guangzhou hawakufuata kanuni ya udhibiti wa virusi vya Corona 2020-04-15

    Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria Geoffrey Onyeama na Balozi wa China nchini humo Zhou Pingjian jana walikutana na waandishi wa habari kwa pamoja, na kufafanua hali halisi kuhusu kile kinachoitwa "Wanigeria kutendewa vibaya mjini Guangzhou", na kutoa taarifa ya hali ilivyo sasa ya raia wa Nigeria waliowekwa karantini huko Guangzhou.

    • Uchambuzi wa kina watolewa na gazeti la Uganda kuhusu tukio lililowahusu raia wa Afrika huko Guangzhou 2020-04-14
    Hivi karibuni, taarifa nyingi zilizagaa kuhusu ubaguzi wa rangi dhidi ya raia wa Afrika mjini Guangzhou, mji wenye idadi kubwa ya Waafrika, wakati China ikizingatia sana kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona kutoka nje.
    • Uchambuzi:Maambukizi ya virusi vya Corona yaathiri vibaya uchumi wa Afrika 2020-04-07

    Nchi mbalimbali za Afrika zimepunguza makadirio ya ongezeko la uchumi la mwaka huu kwa kiasi kikubwa kutokana na athari mbaya ya uenezi wa kasi wa virusi vya Corona kwa uchumi wa Afrika. Wachambuzi wanaona kuwa, mfumo wa afya na matibabu barani Afrika ni dhaifu, muundo wa uchumi ni rahisi na usio na unyumbufu , hivyo maambukizi ya virusi hivyo yataleta changamoto kubwa kwa uchumi wa Afrika.

    • Serikali ya kaunti nchini Kenya yafanya mikakati ya kuimarisha kilimo ili kupambana na atahri hasi za ugonjwa wa Corona 2020-04-06
    Serikali za kaunti nchini Kenya zinachukua hatua mbalimbali za tahadhari ili kukabiliana na athari za maambukizi ya virusi vya Corona. Serikali ya kaunti ya Nandi imezindua matrekta kwa ajili ya wakulima kufanya upanzi ili kuwa na chakula cha kutosha wakati huu wa maambukizi ya virusi vya Corona. Khamis Darwesh anaripoti.
    • Uwezo wa Afrika wa kupambana na virusi wainuka kutokana na michango ya China 2020-04-02

    Vifaa vingi vya matibabu vilivyochangiwa na Mfuko wa Jack Ma na Mfuko wa Alibaba kutoka China, ikiwemo mask, vitendanishi, nguo na miwani ya kujikinga, vinasambazwa kwa nchi zote za Afrika.

    • Sekta ya maua nchini Kenya yapata pigo kufuatia maambukizi ya virusi vya CORONA 2020-03-31

    Sekta ya biashara ya maua nchini Kenya imeathirika kutokana na kukosekana kwa soko la bidhaa hiyo kufuatia mlipuko wa maambukizi ya virusi vya CORONA CORONA.

    • Mradi wa kukarabati hospitali ya kutibu virusi vya Corona ya Zimbabwe uliotekelezwa na kampuni ya China wakamilika 2020-03-31

    Mradi wa kukarabati hospitali ya kutibu virusi vya Corona ya Wilkins ya Zimbabwe uliofadhiliwa na kutekelezwa na kampuni ya China umekamilika na kukabidhiwa rasmi jana Jumatatu.

    • Afrika yapata vifaa vya kupambana na virusi vya Corona kutoka kwa Jack Ma wa China 2020-03-23

    Wakati nchi za Afika zinafunga mipaka kutokana na hofu ya athari ya maambukizi ya virusi vya Corona, bilionea wa China ambaye ni mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Alibaba ya China, Bw. Jack Ma ameahidi kutoa vifaa vya upimaji zaidi ya milioni moja kwa bara hilo.

    • Mbele ya virusi vya corona, Akufaaye wakati wa dhiki ndiye rafiki wa kweli 2020-03-21

    Siku hizi, kuna watoa maoni wengi wametumia methali ya Kiswahili ya "Tembo mbili wakipigana zinazoumia ni nyasi" kueleza wasiwasi wao kuwa kama China na Marekani zinapopambana, nchi za Afrika zitaumia.

    • Nchi 34 za Afrika zaripoti wagonjwa 640 wa COVID-19 2020-03-20
    Habari kutoka kituo cha kinga na udhibiti wa ugonjwa cha Afrika, zinasema kuwa mpaka sasa wagonjwa karibu 640 wameripotiwa katika nchi 34 za Afrika.
    • Tiba ya jadi ya kichina inapata umaarufu barani Afrika wakati wa mlipuko wa COVID-19
     2020-03-19

    Sekta ya afya nchini Namibia imetoa kibali kwa tiba ya jadi ya kichina (TCM) nchini humo. Ilimchukua Peng Wang, raia wa China anayetibu kwa kutumia dawa za asili za China mjini Windhoek, Namibia, miaka mitatu kwa tiba hiyo kusajiliwa na sekta ya afya nchini humo. Machi 6 mwaka huu, Shirikisho la Mfuko wa Msaada wa Afya nchini Namibia lilitoa kibali hicho, na kuifanya Namibia kuwa nchi ya karibuni katika mlolongo wa nchi za Afrika ambazo zinachanganya tiba ya jadi ya kichina katika mfumo wao wa afya. Uamuzi huo umekuja wakati tiba za jadi zikidhihirisha uwezo wake kuwatibu watu walioambukizwa virusi vya korona (COVID-19) nchini China.

    • Balozi wa China nchini Kenya asema China itaziunga mkono kwa juhudi zote nchi za Afrika kupambana na COVID-19 2020-03-18

    Wakati Kenya imethibitisha mtu wa nne kuambukizwa virusi vya Korona, ambaye aliwasili Kenya tarehe 9 Machi kutoka Uingereza, Balozi wa China nchini Kenya Bw. Wu Peng amesema China itachangia uzoefu na vifaa kwa nchi za Afrika katika kupambana na maambukizi ya COVID-19.

    • Nchi za Afrika Kusini mwa Sahara zarekodi maambukizi zaidi ya 100 vya COVID-19 2020-03-17

    Idadi ya maambukizi ya nimonia ya COVID-19 inayosababishwa na virusi vya korona imezidi 100 katika Eneo la Afrika Kusini mwa Sahara, ambako nchi zaidi ya 20, zikiwemo Afrika Kusini, Nigeria na Ethiopia, zimeripoti visa vya maambukizi na kuchukua hatua kupambana na ugonjwa huo.

    • Kenya yathibitisha watu wengine viwili walioambukizwa virusi vya Covid-19, na kutangaza shule kufungwa 2020-03-16

    Rais Uhuru Kenyatta amethibitisha kupatikana kwa visa vingine viwili vya maambukizi ya virusi vya Korona nchini Kenya. Akihutubia Taifa jana Rais Kenyatta amesema watu hao wamethibitishwa baada uchunguzi uliofanywa kwa 27 waliokaribiana na mgonjwa wa kwanza wa virus hivyo nchini Kenya. Rais Kenyatta amesema vikundi vya madaktari vinawafuatilia kwa karibu watu waliokaribiana na mtu huyo.

    • Zimbabwe yajifunza uzoefu wa China katika kukabiliana na COVID-19 2020-03-07

    Wakati dunia inakabiliwa na maambukizi ya ugonjwa wa nimonia inayosababishwa na virusi vipya vya korona COVID-19, uzoefu wa China wa kukinga na kutibu ugonjwa huo umekuwa msaada mkubwa. Waziri wa afya na ustawi wa watoto wa Zimbabwe Bw. Obediah Moyo amesema, nchi hiyo inaiga uzoefu wa China, ili kuzuia ugonjwa wa COVID-19 usienee nchini Zimbabwe.

    • Nchi za Afrika zilizo kusini mwa Sahara zaimarisha nguvu ya kukabiliana na COVID-19 2020-03-06

    Cameroon leo imethibitisha kuwa na kesi ya kwanza ya virusi vya korona (COVID-19), na kuifanya kuwa nchi ya nne baada ya Nigeria, Senegal na Afrika Kusini kuripoti kesi ya ugonjwa huo hii leo katika kanda ya Afrika kusini mwa Sahara.

    • Nchi za Afrika zajitahidi kupambana na COVID-19 2020-03-03

    Maambukizi ya ugonjwa wa nimonia inayosababishwa na virusi vipya vya korona COVID-19 yameanza kuenea katika nchi za Afrika, na jana, Senegal, Morocco na Tunisia kwa nyakati tofauti zimeripoti mgonjwa kwa kwanza wa COVID-19. Nchi za Afrika zinajiandaa kupambana na maambukizi hayo. 

    • Ethiopia yashindana na wakati kudhibiti uvamizi wa nzige 2020-02-27
    Umoja wa Mataifa umeonya kuwa serikali ya Ethiopia inashindana na wakati kudhibiti uvamizi wa nzige wa jangwani unaoendelea, wakati msimu wa mavuno wa kuanzia Februari hadi Mei ukianza.
    • Reli ya SGR nchini Kenya yaendeshwa kwa usalama kwa siku elfu moja 2020-02-26
    Meneja mkuu wa uendeshaji wa reli ya SGR wa kampuni ya Afistar Bw. Li Jiuping, amesema reli ya SGR ya Kenya imeleta manufaa kwa jamii na uchumi wa Kenya.
    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako