• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Chuo kikuu cha Johannesburg cha Afrika Kusini chazindua kituo cha utafiti cha Afrika na China 2018-11-23

    Kituo cha utafiti cha Afrika na China cha chuo kikuu cha Johannesburg cha Afrika Kusini leo kimezinduliwa huko Johannesburg. Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi, mkurugenzi wa kituo hicho upande wa Afrika Kusini Bw. David Monyae amesema, uhusiano kati ya China na Afrika unazidi kuwa karibu, kituo hicho kitafanya juhudi kutafiti uhusiano huo na kuweka kipaumbele katika utafiti wa miradi ya miundombinu, ujenzi wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja", mapinduzi ya nne ya viwanda, mawasiliano ya watu wa China na Afrika na uhusiano kati ya pande mbili.

    • Rais wa Rwanda awakaribisha Wachina kutembelea Rwanda 2018-11-12

    Rais paul Kagame wa Rwanda ametuma salamu kwa Wachina na kuwakaribisha kutembelea nchi hiyo, wakati mauzo ya punguzo kubwa ya tarehe 11/11 ukianza usiku wa kuamkia jumapili.

    • Shirika la Ndege la Ethiopia lazindua tena safari zake za ndege kutoka Addis Ababa hadi Somalia baada ya kusitishwa kwa miaka 41 2018-11-10

    Shirika la ndege la Ethiopia ET jana lilizindua safari tatu za moja kwa moja kwa wiki kati ya Addis Ababa na Mogadishu, baada ya kusitishwa kwa miaka 41, hatua ambayo inaongeza kasi ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.

    • China na Kenya kufanya kongamano la kuhimiza nguvu ushindani kiviwanda 2018-11-09

    Baraza la ushirikiano kuhusu kuhimiza uwezo wa viwanda kati ya China na Kenya litafanyika wiki ijayo mjini Nairobi, ili kuhimiza nguvu ya ushindani kwa uzalishaji wa viwandani nchini Kenya.

    • Benki ya maendeleo ya Afrika yaunga mkono uwekezaji barani Afrika 2018-11-08

    Mkurugenzi wa benki ya maendeleo ya Afrika AfDB Bw. Akinwumi Adesina, amesema mashirika ya fedha yanaunga mkono Afrika wakati bara hilo linajaribu kuvutia uwekezaji na kukabiliana na changamoto zilizopo kuhusu miundombinu.

    • Abiria watatizika kufuatia msako wa matatu Nairobi 2018-11-07
    Abiria wengi wanaendelea kutatizika jijini Nairobi baada ya shughuli za usafiri jijini humo kuathirika tangu siku ya jumatatu kufuatia msako wa magari ya umma unaotekelezwa na maafisa wa trafiki. Matatu (daladala) nyingi zimenaswa na polisi wa trafiki katika msako huo kwa makosa ya kupiga muziki kwa sauti ya juu,mapambo ya rangi nyingi,kukosa mikanda ya usalama,na yale yasiyofaa kuwa barabarani.
    • Rwanda yatarajia kuongeza mauzo kupitia Alibaba 2018-11-02

    Serikali ya Rwanda imesema itatumia fursa ya makubaliano kati yake na kampuni ya Alibaba kuuza bidhaa zaidi kwenye soko la China na hivvyo kusaidia maelfu ya vijana wake kupata ajira.

    • Reli ya SGR imesafirisha abiria milioni 2 nchini Kenya 2018-11-01

    Naibu meneja mkuu wa Kampuni ya operesheni ya reli ya Africa Star inayosimamia uendeshaji wa treni ya abiria ya reli ya SGR Bw. Li Jianfeng, amesema reli ya SGR ya Kenya imesafirisha abiria zaidi ya milioni 2 kati ya Nairobi na Mombasa tangu ilipozinduliwa mwezi wa Mei mwaka jana.

    • Maonesho ya ajira ya KCETA yafanyika jijini Nairobi 2018-10-30

    Nafasi za ajira zaidi ya 1,000 zimetolewa na makampuni ya China yanayoendesha shughuli mbalimbali nchini Kenya kufuatia kuanzishwa kwa maonesho ya kwanza ya ajira ya Chama cha Kiuchumi na Biashara kati ya Kenya na China (KCETA),ya liyondaliwa jana katika jumba la mikutano la KICC jijini Nairobi.

    • Muungano wa utafiti wa Afrika wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja" waanzishwa 2018-10-29

    Muungano wa utafitu wa Afrika wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja" umeanzishwa huko Guangzhou, China, ambapo umefanya kongamano la kwanza la kimataifa.

    • Makampuni ya Kenya yalenga soko la China 2018-10-26

    Maonesho ya kwanza ya uagizaji bidhaa ya kimataifa ya China CIIE yatafanyika huko Shanghai. Makampuni ya nchi mbalimbali ikiwemo Kenya yanataka kutumia fursa hiyo kupata faida katika soko kubwa la China. Kenya ni nchi yenye raslimali nyingi ikiwemo kahawa, chai na chakula, na makampuni ya nchi hiyo yanataka kuwawezesha wachina wengi zaidi kuonja utamu wa bara la Afrika kupitia jukwaa hilo. 

    • SGR, Reli yangu
    Hadithi ya Jeff, afisa wa ngazi ya kati ya SGR
     2018-10-26

    Kwenye makala yetu ya hadithi za SGR leo mwandishi wetu anazungumza na Jeff Muiruri ambaye ni afisa wa ngazi ya kati kwenye mradi wa ujenzi wa reli kati ya Nairobi na Narok.

    • SGR, Reli yangu
    Hadithi ya Sera, abiria wa SGR
     2018-10-25

    Kwenye makala yetu ya hadithi za SGR leo mwandishi wetu anazungumza na abiria wanaofurahia huduma za usafiri kwenye treni mpya ya SGR.
    Ni safari ya kwenda Mombasa kwa kutumia treni mpya ya SGR.
    Umbali wa kilomita 472 kati ya mji mkuu Nairobi na mji wa pwani Mombasa.
    • SGR, Reli yangu
    Hadithi ya Mugo na Sharon, wahudumu wa SGR waliopata mfunzo China
     2018-10-24

    Kwenye makala yetu ya hadithi za SGR leo mwandishi wetu amekutana na Kennedy Mugo na Chelangat Sharon, wahudumu wa wa abiria kwenye treni mpya ya SGR kati ya Nairobi na Mombasa.
    Wawili hao ni miongoni mwa wale waliopata mafunzo nchini China.
    Ni sauti za Kennedy Mugo na Chelangat Sharon ambao ni wahudumu wa ndani ya treni mpya ya kisasa nchini Kenya na wamekuwa wakifanya kazi hapa kwa zaidi mwak mmoja unusu.
    • SGR, Reli yangu
    Hadithi ya Patrick na Rapahel, wajenzi wa SGR
     2018-10-23

    Kwenye makala yetu ya hadithi za SGR leo mwandishi wetu ametuandalia ripoti kuhusu na Kennedy Mugo na Chelangat Sharon, wahudumu wa wa abiria kwenye treni mpya ya SGR kati ya Nairobi na Mombasa.
    Ndio nguvu kazi ya ujenzi wa reli ya kisasa SGR nchini Kenya.
    Vijana kwa wazee.
    Kampuni inayotekeleza mradi huu wa reli imekuwa nchini Kenya kwa zaidi ya miaka 20 ikitekeleza mirafi mingine kama vile barabara.
    • SGR, Reli yangu
    Hadithi ya Diana, meneja wa holeti mjini Mombasa
     2018-10-22

    Kwenye makala yetu ya hadithi za SGR leo mwanidhsi wetu wanaangazi sekta ya hoteli mjini Mombasa.
    Mji wa Mombasa.
    Ni wenye kuvutia watalii kwa wingi kutoka ndani na nje ya nchi.
    Upepo wake ni mwanana bahari na pwani ya kupendeza.
    Lakini katika siku za nyuma ilikuwa ni vigumu kwa watu wengi kufika hapa kwani hakukuwa na njia rahisi ya kusafiri.
    • Viongozi watofautiana kuhusu kura ya maoni ya katiba Kenya 2018-10-08

    Wanasiasa kutoka nchini Kenya wameendelea kushinikiza hoja ya mabadiliko ya katiba ila kwa lengo kupunguza gharama ya serikali. Aliyekuwa waziri mkuu nchini humo Raila Odinga amekuwa akitoa wito wa kura ya maoni ili kuongeza nafasi za uongozi na kuwa na serikali yenye uwakilishi zaidi.

    • Kenya yaanza kuhimiza mafungamano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Internet 2018-09-28

    Kenya imeanzisha kampeni ya kuhimiza mafungamano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia mtandao wa Internet.

    • Ubalozi wa China nchini Kenya waadhimisha miaka 69 ya jamhuri ya watu wa China 2018-09-27
    Ubalozi wa China nchini Kenya umefanya sherehe mjini Nairobi, kuadhimisha miaka 69 tangu kuzinduliwa rasmi kwa Jamhuri ya Watu wa China. Kwenye hotuba aliyotoa kwenye sherehe hiyo, iliyosomwa kwa niaba yake na Bwana Li Xuhang wa ofisi ya mambo ya kigeni, Balozi Sun amesema China imepiga hatua za kuigwa na mataifa mengine duniani, kutokana na juhudi zake za miaka 40 iliyopita
    • Afisa wa Burundi asema ni vigumu kufikia lengo la kuwarudisha wakimbizi elfu 72 wa Burundi 2018-09-26
    Msaidizi wa waziri wa mambo ya ndani wa Burundi Bw. Therence Ntahiraja amesema itakuwa vigumu kufikia lengo la kuwarudisha nyumbani wakimbizi elfu 72 wa Burundi kutoka Tanzania kabla ya mwezi Desemba mwaka huu kama ilivyofikiwa kwenye mkutano wa kurejesha wakimbizi kwa hiari mwezi Machi.
    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako