Mwishoni mwa mwaka 2009 Jumba la Makumbusho la Historia ya Maneno ya Kichina lilizinduliwa rasmi huko Anyang mkoani Henan, ambao ni mji maarufu kwa kuwa chimbuko la maandishi ya asili kabisa ya Kichina yaliyoandikwa kwenye magamba ya kobe na mifupa. |
Mji wa Zhengzhou uliopo katikati ya China ni moja kati ya miji mikubwa minane ya kale nchini China, katika mji huo kuna sehemu 26 za mabaki ya kale ya ngazi ya taifa. Kutokana na ugunduzi mkubwa uliofanywa na wataalamu wa mambo ya kale, mji huo umekuwa unavutia kutokana na utamaduni mkubwa wa kale. Bw. Yu Xiaoxing ni moja kati ya wataalamu hao wa kale ambaye ni wa kizazi cha kwanza kabisa tangu Jamhuri ya watu wa China ianzishwe. |
Maonesho makubwa mawili yanafanyika kwa pamoja katika Jumba la Makumbusho la Beijing, maonesho ya kwanza ni kuhusu historia ya mmisionari Matteo Ricci wa Italia alipokuwa nchini China kueneza utamaduni wa Ulaya zaidi ya miaka 400 iliyopita, na mengine ni maonesho ya vyombo vya kauri vya China vilivyokuwa vinauzwa katika nchi za Ulaya katika karne ya 18. Maonesho hayo mawili yanayofanywa kwa pamoja yanaonesha wazi hali nzuri ya maingiliano ya utamaduni kati ya China na Ulaya katika zama za kale. |
Katika sikukuu ya Mwaka Mpya wa jadi wa China au "Sikukuu ya Spring", watu wa makabila yote ya China hufanya shamrashamra za kila aina na kufanya matambiko kwa miungu na mababu zao wakikaribisha mwaka mpya na kuomba mavuno mazuri. Utamaduni huo pia unafuatwa na watu wa makabila mengi madogo madogo mkoani Yunnan kusini magharibi mwa China. |
Taa za Mapambo ambazo pia zinaitwa Taa za Sikukuu zimekuwa na historia ya zaidi ya miaka 1,800 nchini China, na ni mapambo muhimu yanayochangia mazingira ya sherehe za sikukuu. Mchana, taa hizo zinazotundikwa mbele ya milango zinaleta mazingira ya furaha, na usiku, taa hizo zinazowaka zinaleta mazingira ya kifahari. |
Opera ya Huangmei ni moja kati ya opera tano muhimu nchini China. Hapo awali, opera hiyo ilitokea katika wilaya ya Huangmei mkoani Hubei, na ilikuwa inaitwa "nyimbo za Huangmei" au "nyimbo za kuchuma chai", lakini hivi leo opera hiyo imeenea zaidi katika mji wa Anqing mkoani Anhui na wilayani Huangmei mkoani Hubei. |
Taa za Mapambo ambazo pia zinaitwa Taa za Sikukuu zimekuwa na historia ya zaidi ya miaka 1,800 nchini China, na ni mapambo muhimu yanayochangia mazingira ya sherehe za sikukuu. Mchana, taa hizo zinazotundikwa mbele ya milango zinaleta mazingira ya furaha, na usiku, taa hizo zinazowaka zinaleta mazingira ya kifahari. |
Katika mji wa Urumqi, mkoani Xinjiang China, kuna bustani moja iliyowekwa sanamu zaidi ya 60. Kati ya sanamu hizo inayovutia zaidi ni sanamu yenye mtindo wa utamaduni wa kikabila mkoani humo, hii ni sanamu iliyopewa jina la "Dansi ya Batamaji", ambayo ilichongwa na Bw. Zhang Xinmin, ambaye ni mkurugenzi wa Shirikisho la Wachongaji la Mkoa wa Xinjiang. |
Katika mji wa Huangshi wa mkoa wa Hubei, katikati ya China, kila mwaka kabla ya siku ya tarehe 5 ya mwezi wa 5 kwa kalenda ya kilimo ya China, hufanyika Tamasha la Mashua ya Dragoni Yenye Sanamu za Miungu. Hili ni tamasha linalofanyika kwa ajili ya kuomba Mungu awabariki watu wa sehemu hiyo na kuwapa amani na afya njema |
Mji mdogo Guanhu mkoani Jiangsu China unajulikana kwa maendeleo ya kasi kiuchumi na usanii wa kutengeneza vichwa vya Simba kwa karatasi. Kutokana na usanii huo kuwa na historia ndefu, serikali imeuweka katika orodha ya urithi wa utamaduni usioonekana wa China, na Bw. Shi Rongsheng ambaye ana ujuzi mkubwa wa usanii huo amechaguliwa kuwa mrithi wa usanii huo. |
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |