Tamasha la 11 la sanaa la nchi za Asia ambalo linafanyika katika mji wa Erdos mkoani Mongolia ya Ndani China limeanza tarehe 18 Agosti na litamalizika tarehe 26. Ujumbe ulioongozwa na mawaziri wa utamaduni kutoka nchi 16, maofisa wa tume za nchi 28 nchini China na wasanii wa makundi ya kiserikali kutoka nchi 18 walishiriki kwenye tamasha hilo kwa nia ya kuimarisha maelewano, ushirikiano na kutunza tamaduni za jadi za aina mbalimbali za Asia. |
Ouyang Xiu alikuwa ni mwanasiasa na mwanafasihi mkubwa katika Enzi ya Song Kaskazini ya zama za kale nchini China, na ni mmoja kati ya wanafasihi wakubwa wanane katika enzi za Tang na Song. |
Picha zilizochorwa kwenye sehemu ya ndani ya chupa ni sanaa ya kipekee nchini China, picha hizo zinazochorwa kwenye tabakero kwa ndani ni pamoja na picha za watu, mandhari ya mazingira ya asili, maua, ndege na sanaa ya maandiko ya Kichina. Tabakero ni kichupa kidogo kinachotengenezwa kwa kioo, fuwele au kaharabu. |
Wilaya ya Dangtu iliyoko kwenye ukingo wa Mto Changjiang mkoani Anhui, mashariki mwa China, inasifiwa kuwa ni "Bahari ya Nyimbo za Wenyeji". Nyimbo za Dangtu maana yake ni nyimbo za aina zote za jadi zinazoenea miongoni mwa wenyeji wa wilaya hiyo, mambo yanayoimbwa kwenye nyimbo hizo ni kuhusu maisha kwenye jamii |
Bi. Jia Pengfei ni mwigizaji kijana wa Jumba la Taifa la Opera ya Beijing, katika michezo ya opera ya Beijing anaigiza wahusika wanawake mbalimbali waliojulikana katika hadithi, aliwahi kuigiza mara nyingi mchezo wa opera ya Beijing "Malaika Atawanya Maua" nchini na nje ya China ambao ulitungwa na msanii mkubwa wa opera ya Beijing Bw. Mei Lanfang, kutokana na maigizo yake mazuri na sauti yake nyororo, watu wanamwita "Malaika". |
Maonesho ya 53 ya kimataifa ya sanaa yanayofanyika kila baada ya miaka miwili hivi sasa yanafanyika huko Vinice Italia, hili ni tamasha kubwa linaloshirikisha wasanii 30 wakubwa duniani kufanya maonesho yao binafsi, mmoja kati ya wasanii hao ni mchoraji Liu Zhong ambaye ni mchoraji wa kwanza kabisa kutoka China kushiriki kwenye maonesho hayo. |
Mfasiri Gao Mang mwenye umri wa miaka 83 mwaka huu, alianza kazi ya kutafsiri maandishi ya fasihi ya Russia tokea miaka ya 40 ya karne iliyopita. Katika miongo kadhaa iliyopita amepata mafanikio makubwa katika kazi ya kutafsiri, kuhariri na kufanya utafiti kuhusu fasihi ya Russia. Kutokana na mafanikio hayo alitunukiwa nishani na rais wa Russia. |
Katika mwaka huu wa lugha ya Kirusi nchini China tumeandaa maelezo kuhusu watu mashuhuri wa China waliowahi kusoma Russia, leo tunawajulisha mwimbaji mwenye umri wa miaka 82 Bi. Guo Shuzhen. |
Katika sehemu ya Altay, kaskazini mwa mkoa wa Xinjiang China, wanaishi watu wa kabila la wakhazak, ambapo sanaa ya jadi iitwayo Dastan ya kuimba na kuongea imeenea sana miongoni mwao. Dastan ni fasihi simulizi, hivi sasa imekuwepo kwa miaka zaidi ya elfu moja. Mzee Kazim Alman ni mrithi wa sanaa hiyo, sasa tusikie maelezo kuhusu mzee huyo. |
Mtunzi mkubwa wa muziki wa China Bw. Wu Zuqiang mwenye umri wa miaka 82, amekuwa akiandamana katika maisha yake ya muziki, na masomo aliyopata Russia katika miaka ya 50 ya karne iliyopita yalimwekea msingi imara wa utunzi wa muziki. |
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |