• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Nchi zalenga kupanua uhusiano wa kibiashara na China kupitia maonyesho ya Shanghai 2020-11-03

    Katika kile kinachoonyesha hali tofauti kabisa na hali ya mambo katika maeneo mengine ya dunia, China inajipanga kuandaa maonyesho ya kila mwaka ya China International Import Expo, kuashiria kurejea kwa hali ya kawaida katika taifa hilo lenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani.

    • Kenya na China zasisitiza haja ya ushirikiano wa kimataifa 2020-09-28

    Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake wa China Xi Jinping wameelezea wasiwasi wao kuhusu kudhoofika kwa ushirikiano wa Kimataifa, hatua ambayo wamesema utaacha ulimwengu katika hali hafifu hasa kutokana kwa shinikizo zinazohatarisha utulivu wake.

    • Hatua madhubuti za China za kukomesha matumizi mabaya ya data 2020-09-11

    Juhudi za kimataifa za kuwalinda watumiaji wa teknolojia ya kidijitali pamoja na juhudi za kusitisha matumizi mabaya ya data, yalipigwa jeki wiki hii baada ya China kuzindua mwongozo inayokusudiwa kuhakikisha usalama wa habari na uendelezaji wa uchumi wa kidijitali ambao unaendelea kupanuka kila uchao.

    • China yahimiza ushirikiano wa kimataifa kukabiliana na mgogoro wa kiafya na kiuchumi 2020-05-30

    Janga la virusi vya Corona, kwa sasa, limeibuka kuwa changamoto kubwa zaidi ambalo wanadamu wamekumbana nalo tangu vita vikuu vya dunia. Ugonjwa huo wa kuambikiza umesambaa hadi karibu kila kona ya dunia. Hadi sasa, nchi 213 na maeneo kote duniani yameathirika.

    • Ahadi ya China kwa washirika wa kiuchumi ni habari njema hasa kwa Afrika 2020-05-26

    Dunia kwa sasa inapambana vurugu inayotokana na janga la chamuko la homa ya Corona. Waangalizi wengi wanashikilia mtazamo kwamba janga hili litavuruga uchumi wa dunia kwa kiwango ambacho kamwe haijawahi kutokea. Hata ingawa ukubwa kamili wa athari zake haujadhihirika kwa sasa, siku za baadaye kwa nchi nyingi hasa katika mataifa yanayoendelea yamejaa mashaka.

    Ili kustahimili dhoruba ya janga hili, mataifa lazima yapigane na ugonjwa huu kwa pamoja. Katika vita hivi, mimi, kama wengine wengi walivyohoji, kwa maoni yangu, hakuna yeyote anayefaa kuachwa nyuma. Huu si wakati wa mwenye nguvu mpishe bali hii ni safari ambapo mwenye nguvu lazima amsaidia aliye dhaifu.

    • China imeipa kipaumbele ustawi wa raia wake na hali njema duniani 2020-05-23

    Macho yote kwa sasa yameelekezewa China wakati huu ambapo viongozi na wabunge nchini humo wanakutana tena kwa mkutano wa bunge wa mwaka, jijini Beijing. Hii hasa inatokana na kuzuka kwa maradhi ya covid-19 ambayo imeyumbisha uchumi wa dunia kwa kiwango ambacho kamwe haijawahi kushuhudiwa.

    • Ujasiri wa uongozi wa China kwenye vita dhidi ya janga la COVID-19 2020-04-01

    Uwezo wa uongozi wowote popote huonekana katika nyakati za migogoro. Ama kwa hakika, ni katika nyakati za dhiki ndipo serikali zinaimarishwa au kusambaratishwa. Hali kama hii pia inaonekana katika taasisi mbali mbali, ziwe za kisiasa, kiuchumi au kijamii.

    • Jumuiya ya kimatiafa yahitaji mshikamano ili kushinda mlipuko wa virusi vya Korona 2020-02-08

    Kitabu kitakatifu kinasema "Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake" ……."wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kuyakusanya mawe pamoja. Wakati wa kukumbatia na wakati wa kujizuia kukumbatia ... wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa vita na wakati wa amani."

    • China yathibitisha kuwa ni mshirika wa karibu wa Kenya kufuatia mkasa wa maporomoko ya ardhi 2019-12-23

    Mwezi mmoja uliopita, kaunti ya Pokot Magharibi iliyoko katika mkoa wa Bonde la Ufa nchini Kenya iligonga vichwa vya habari baada ya kukumbwa na mkasa wa maporomoko ya ardhi. Janga hili lilisababishwa na mvua kubwa iliyokuwa ikushuhidiwa katika sehemu hiyo.

    • Juhudi za kampuni moja za kupambana na umaskini zazaa matunda Kusini Magharibi mwa China 2019-09-27

    Kwa miaka mingi, umaskini uliokithiri ulidhihiri hali mbaya ya kiuchumi ya maeneo kadhaa ya kusini magharibi mwa China. Jimbo la Guizhou lililojaa milima, kwa mfano, limekuwa nyumbani mwa mamilioni ya watu masikini.

    • China yasisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kwenye mpango wa Mkanda Mmoja Njia Moja 2019-09-18

    Kongamano la jukwaa la mtandao wa habari la Mkanda Mmoja Njia Moja maarufu kama Belt and Road News Network (BRNN) lilingoa nanga katika mji mkuu wa China, Beijing, tarehe 16 Septemba, 2019, na kuwavutia waandishi wa habari 50 wanaowakilisha vyombo vya habari maarufu 46 kutoka nchi 26 mbalimbali kutoka bara Afrika na Amerika ya Kusini.

    • Mwekezaji kutoka China atangaza nia ya kufufua kiwanda cha mshubiri nchini Kenya 2019-09-10

    Mwaka 2004, kiwanda kilichogharimu mamilioni ya pesa cha aloe vera au mshubiri kilianzishwa katika eneo la Baringo. Jamii inayoishi sehemu hiyo iliona hatua hii kama baraka kwani hii ingewasaidia kujikwamua kutoka minyororo ya ufukara uliokithiri katika asilimia kubwa ya sehemu hiyo.

    • Pato la kigeni la Kenya kuongezeka baada ya nchi hiyo kufanya makubaliano na China kuhusu chai ya zambarau 2019-09-06

    China imefungua milango yake kwa bidhaa zaidi za kilimo kutoka Kenya. Kuanzia sasa kwenda mbele, wakulima wa chai ya rangi ya zambarau katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki wataanza kusafirisha chai maalumu kwa soko la China baada ya makampuni mawili kutoka nchi hiyo ya bara Asia kufanya makubaliano ya kutangaza mpango wa kusambaza zao hilo nchini China.

    • China yaahidi kuisaidia Kenya katika utoaji wa huduma za afya kwa wasiojiweza 2019-07-01

    China imetoa ahadi ya kusaidia juhudi za Kenya za kutoa na kuchukua huduma za afya karibu na raia katika sehemu zote za nchi. Balozi wa China nchini Kenya Wu Peng alizungumzia kujitolea kwa Beijing kutimiza ahadi yake ya kuhakikisha kwamba pande zote zinanufaika wakati mahusiano baina ya nchi hizo mbili zinaendelea kunawiri.

    • Balozi Wu akutana na Odinga na kujadili njia za kuimarisha mahusiano kati ya Kenya na China 2019-06-27

    Kiongozi wa upinzani wa Kenya Raila Odinga alikuwa mwenyeji wa balozi wa China nchini Kenya Wu Peng katika ofisi yake ya Capitol Hill jijini Nairobi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kitengo cha habari cha Odinga, wawili hao walibadilishana mawazo juu ya kuimarisha mahusiano yaliyomo kati ya Nairobi na Beijing.

    • Kuibuka kwa teknolojia kutoka China barani Afrika kumekumbatiwa pakubwa 2019-06-24

    Uwekezaji wa Wachina katika miundombinu ya teknolojia katika Afrika unaendelea kushika kasi kote barani. Bila ufahamu wa mamilioni ya watumiaji, teknolojia kutoka Beijing sasa inatumika kama uti wa mgongo wa mtandao wa miundombinu katika nchi kadhaa za Afrika.

    • Licha ya marufuku kutoka Marekani, itakuwa vigumu kumaliza mahusiano katika ya Huawei na Afrika 2019-06-17

    Serikali ya Marekani hivi karibuni ilitangaza vikwazo dhidi ya kampuni ya Huawei na kuzuia kampuni hiyo kutumia programu mbalimbali za kampuni ya Google.

    • Wakulima wa Kenya hatimaye wapata miche ya aina ya parachichi iliyoruhusiwa kuingia soko la China 2019-05-27

    Wakulima wadogo wadogo kutoka Kenya wamo mbioni kufaidi kutokana na uamuzi wa China kufungua soko lake kwa bidhaa za kilimo kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki. Miongoni mwa mimea mengine, Beijing iliingia makubaliano na Nairobi mwezi Novemba mwaka jana ambapo mazao ya maembe, korosho na parachichi zitaingia katika soko la China kwa mara ya kwanza.

    • Wakulima wa Kenya hatimaye wapata miche ya aina ya parachichi iliyoruhusiwa kuingia soko la China 2019-05-27
    Wakulima wadogo wadogo kutoka Kenya wamo mbioni kufaidi kutokana na uamuzi wa China kufungua soko lake kwa bidhaa za kilimo kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki. Miongoni mwa mimea mengine, Beijing iliingia makubaliano na Nairobi mwezi Novemba mwaka jana ambapo mazao ya maembe, korosho na parachichi zitaingia katika soko la China kwa mara ya kwanza.
    • Makampuni ya Kichina nchini Kenya yaahidi kuyapa kipaumbele ustawi wa wafanyakazi wao 2019-05-02

    Makampuni ya Kichina yanayoendesha shughuli yao nchini Kenya yameahidi kuzingatia zaidi ustawi wa wafanyakazi wao wa ndani. Yakiongozwa na kampuni ya China Road and Bridges Corporation (CRBC), makampuni hayo yalisisitiza haja ya kusaidia kupunguza mzigo kwa wafanyakazi wao hasa wale wanaopeleka watoto wao shuleni.

    • Dhamira na malengo ya Ukanda Mmoja Njia Moja yatoa msukumo kwa mataifa yanayoendelea kuukumbatia mpango huo 2019-04-26

    Mwaka 2017 iliashiria hatua ya kihistoria ya uhusiano wa China na ulimwengu. Aidha, mwaka huo ulikuwa wenye matukio mahsusi hasa kwa uhusiano kati ya China na Afrika. Utaratibu mpya wa dunia uliibuka.

    • Wakenya katika makampuni ya Kichina wasifu ushirikiano kati ya Kenya na China 2019-04-19

    Baadhi ya wafanyakazi bora wa Kenya katika makampuni ya Kichina yanayoendesha shughuli zao nchini humo walitunukiwa nafasi ya kihistoria ya kuzuru China baada ya makampuni hizo kugharamia ziara hiyo kwa asilimia mia moja.

    • Juhudi za Kenya za kuuza parachichi kwenye soko la China zashika kasi huku wakaguzi kutoka Beijing wakitua Nairobi 2019-04-03
    • Afisa wa ngazi ya juu wa UM asifu miradi ya China Afrika huku akiomba Beijing kusaidia kuangamiza jinamizi la ufisadi barani 2019-03-28

    Katibu Mkuu wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na maendeleo, UNCTAD, Dkt. Mukhisa Kituyi ametoa wito kwa serikali ya China kusaidia Afrika kushinda vita dhidi ya rushwa iwapo bara hilo linataka kufanikisha ajenda yake ya maendeleo.

    • Ajenda ya China ya usalama Afrika inashika kasi huku bara hilo likiendeleza juhudi za amani kwa ajili ya maendeleo 2019-03-24
    Muda mfupi baada ya kuchukua hatamu za uongozi mwaka 2013, Rais wa China Xi Jinping alishinikiza kuwepo kwa sera dhabiti kuhusiana na mataifa ya kigeni na kusababisha viongozi wengi barani Afrika kuvutiwa na uhusiano wa karibu na Beijing, si tu katika ulimwengu wa biashara na mahusiano ya kiuchumi lakini katika masuala ya usalama pia.
    • Afrika yapaswa kufwatilia kwa karibu matukio katika mikutano miwili ya kisiasa nchini China 2019-03-04

    Kila mwaka, vyombo vikuu vya kisheria nchini China huitisha mikutano kwa kile ambacho ni kongamano lenye shughuli nyingi hasa katika kuweka ajenda ya mwaka unaofuata. Hii ni pamoja na ajenda ya Rais kwa China na ulimwengu.

    • Makampuni ya Kichina yanadhamini masomo ya wanafunzi kutoka familia maskini nchini Kenya 2019-01-14

    Enzi mpya ya urafiki na ushirikiano kati ya China na Afrika inaendelea kushuhudiwa barani humo. Pande zote mbili yanapiga hatua muhimu katika mahusiano ya kibiashara pamoja na ubadilishanaji wa utamaduni na mahusiano ya watu kwa watu.

    • Makampuni kutoka China sasa yanatoa fursa zaidi za ajira kwa Wakenya kupitia maonyesho ya kazi 2018-10-30

    Makampuni ya Kichina yanayofanya kazi nchini Kenya yamefungua milango ya nafasi zaidi za ajira kwa wenyeji. Makampuni haya yalitangaza kuwepo kwa nafasi za ajira wakati Muungano wa uchumi na biashara kati ya China na Kenya ulipozindua rasmi maonyesho ya kazi kwenye jumba la KICC jijini Nairobi.

    • Chama tawala nchini Kenya kimetangaza nia ya kufuata nyayo za Chama cha Kikomunisti cha China 2018-10-22

    Chama cha Jubilee cha Kenya kimeanza mchakato wa kuratibu mfumo na sera zake na kuweka msingi imara wa kisiasa. Wakati ambapo mahusiano baina Nairobi na Beijing yanaendelea kumawiri, viongozi wa chama hicho tawala nchini Kenya wameweka wazi nia yao ya kufuata nyayo za Chama cha Kikomunisti cha China huu ukiashiria sura mpya ya ushirikiano wa kisiasa.

    • Hatua kwa hatua China imekuwa kipenzi cha wanafunzi wanaotafuta masomo ya juu kutoka Afrika 2018-09-25

    Mwenendo wa hivi karibuni unaonyesha kuwa China imekuwa eneo la kuvutia kwa Waafrika wanaotafuta masomo zaidi. Kufikia mwaka jana, inakadiriwa kuwa asilimia 14 ya wanafunzi wote wa kigeni katika China wanatoka Afrika. Huu ni ukuaji wa haraka mno kwani mwaka 2003 ni asilimia 2 pekee ya wanafunzi kutoka Afrika waliotafuta masomo China.

    1  2  3  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako