• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Wanadiplomasia wanasema FOCAC unaashiria mwamko mpya Afrika 2018-08-24

    Wanadiplomasia wameelezea matumaini yao kuwa ushirikiano kati ya Afrika na China kupitia Jukwaa la Forum on China-Africa Cooperation (FOCAC) utaleta enzi mpya ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

    • Ahadi ya China ya kutekeleza miradi Afrika kupitia mpango wa Ukanda Mmoja na Njia Moja 2018-05-28

    Mpango wa mkanda mmoja njia moja unaadhimisha mwaka mmoja mwezi huu wa Mei tangu kuzinduliwa kwake rasmi kwa ulimwengu katika sherehe iliyofana jijini Beijing mwaka 2017. Halfa hiyo ilihudhuriwa na marais na viongozi wa serikali mbalimbali ambao baadaye waliidhinisha mpango huo na hatimaye kutia saini kuthibitisha uanachama wao katika mpango huo mkuu wa China ya kuunganisha dunia.

    • Vijiji 800 nchini Kenya kufaidika kutokana na mradi wa digitali inayofadhiliwa na China 2018-04-26

    USHIRIKIANO kati ya Kenya na China kwa mara nyingine utahakikisha kuwa jumla ya vijiji 800 kote nchini vitapata kuunganishwa kupitia mradi wa utoaji wa runinga ya kunasa mawimbi ya digitali bila malipo.

    • Uwazi wa China utachochea ufanisi wa kichumi katika mataifa mengi 2018-04-26

    Wakati ulimwengu ulikuwa unakaribisha mwaka wa 2018, Rais wa China Xi Jinping alitoa hotuba muhimu kuhusiana na nchi hiyo kufungua milango yake na kuwa wazi kwa dunia kati ya maswala mengine. Hii ilikuwa ni muhimu sana kwani haikuwa tu inahusu taifa la China bali ililenga binadamu kwa ujumla.

    • China kugeukia washirika mbadala iwapo malumbano ya kibiashara na Marekani yatakithiri 2018-04-12

    Katika dunia nzima, mataifa yanafuatilia kwa karibu matukio yanayoendelea katika nchi mbili yenye chumi kubwa ulimwenguni ambayo huenda yakasababisha malumbano ya kibiashara kati ya Beijing na Washington.

    • Asilimia kubwa ya Wakenya wathamini China kama mshirika mkuu wa maendeleo 2018-04-08

    Asilimia kubwa ya Wakenya wanaamini China ni mshirika mkubwa anayefaidi Kenya. Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na kampuni ya utafiti ya Ipsos, asilimia 34 ya wale waliohojiwa wanaamini kwamba Kenya iko kwenye nafasi nzuri ya kuinuka kiuchumi China ikiwa mshirika wake ikilinganishwa na asilimia 26 ambao wanaamini Marekani ni mshirika mwema kimaendeleo.

    • Mpango wa Mkanda Mmoja Njia Moja yachochea ukuaji wa soko ya mali nchini Kenya 2018-02-16

    KNIGHT Frank sasa inasema soko ya mali isiyohamishika nchini Kenya imefaidika mno kutokana na mpango wa Mkanda Mmoja Njia Moja. Kwa mujibu wa kampuni hiyo ya ushauri wa mali, idadi kubwa ya miradi kwa sasa yanatekelezwa katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki chini ya udhamini wa mfumo huo unaopendekezwa na serikali ya China.

    • Umuhimu wa ziara ya Waziri Wang Yi barani Afrika 2018-01-13

    Kuna msemo maarufu usemao: "Rafiki mpime kwa vitendo". Ama kwa kweli usemi huu unatumika mara nyingi kutilia mkazo vitendo vya watu walio kwenye mahusiano ya karibu. Hakika, ni rahisi kwa mtu binafsi kupima umuhimu wake anapoangalia mambo anayotendewa.

    • Treni za mwendo kasi: China kujenga mtandao mpya wa kilomita 23,000 kufikia 2030 2017-11-24

    Tangu China ilipozindua treni za mwendo kasi mwaka 2008, nchi hiyo imejenga kilomita 22,000 za reli, na kuwa mtandao mkubwa zaidi duniani kwenye masuala ya mfumo huo wa usafiri ikilinganishwa na mataifa mengine. Lakini shughuli hii bado haijakamilika kwani uongozi wa nchi hiyo unapanga kujenga kilimita 23,000 mpya za mtandao wa treni za mwendo kasi na kufikisha jumla ya mtandao huo urefu wa kilomita 38,000 kufikia mwaka wa 2025 na hatimaye kilomita 45,000 mwaka wa 2030.

    • Mfanyabiashara maarufu kutoka China kuanzisha viwanda ndogo ndogo Afrika 2017-11-22

    Mfanyabiashara kutoka China ametangaza mpango wa kupanua biashara zake barani Afrika kwa kuwekeza katika viwanda vidogo vidogo tano kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa za nyumbani za matumizi ya kila siku kama vile betri za tochi, karatasi ya choo na bidhaa za elektroniki.

    • Kampuni ya kutengeneza magari ya umeme kutoka China inapanga kuwekeza zaidi Afrika 2017-11-18

    Serikali ya China inasema kuwa ina nia ya kuondoa magari yote yanayotumia mafuta kwenye barabara zake katika miaka michache ijayo. Badala yake magari yanayotumia nishati ya umeme yatachukua nafasi yao, ambayo Beijing inasema inatokana na mahitaji makubwa nyumbani na nje ya nchi.

    • China yashuhudia ukuaji mkubwa katika sekta ya anga 2017-11-14

    China kwa sasa inajenga mojawapo ya uwanja mkubwa wa ndege duniani. Uwanja huo mpya wa Beijing Daxing Airport inajengwa kwa gharama ya bilioni 12 dola za Marekani na itakuwa uwanja wa ndege wa tatu katika mji mkuu wa China, Beijing.

    • Xi kutumia hadhi yake mpya kushawishi maendeleo Afrika 2017-10-26

    Rais Xi Jinping sasa anasema atatumia hadha aliyotunukiwa katika jamii ya Kichina kuboresha maisha ya wengi katika nchi zinazoendelea. Xi anasema mawazo yake sasa zinatoa mbinu mbadala kupambana na changamoto zinazokabili nchi nyingi.

    • Enzi mpya China na kuongezeka kwa ushawishi wake ulimwenguni 2017-10-23

    Kote duniani, wengi wamekuwa makini na kuelekeza macho Beijing siku za hivi karibuni kutokana na mkutano wa kitaifa wa 19 wa Chama cha Kikomunisti cha China. Bila shaka, viongozi wa dunia na watu kutoka kila ngazi ya maisha wanakodolea jicho tukio hilo linalofanyika mara moja kila baada ya miaka mitano linalofanyika kwenye mji mkuu wa China, ikiwa taarifa ni za kuaminika. Lakini, matokeo ya mkutano huo yatakayowekwa hadharani mwishoni yanasubiriwa kwa hamu na gamu zaidi na wote.

    • China yaahidi mahusiano dhabiti na nchi marafiki baada ya mafanikio yake ya kiuchumi 2017-10-21

    Rais wa China Xi Jinping sasa anasema uchumi wa nchi yake ilistahimili dhoruba kali na kuinuka tena baada ya kipindi ambapo ilisajili utendaji usio wa kuridhisha. Kiongozi huyo wa Kichina alisema hayo huku akisisitiza kuwa Beijing itabaki mwamba wa kiuchumi duniani. Rais huyo alifichua kwamba pato la nchi yake limeongezeka kwa trilioni 4 Dola za Marekani katika miaka mitano iliyopita.

    • China kufadhili utafiti zaidi juu ya Afrika katika juhudi za kuimarisha ushirikiano 2017-10-11

    Serikali ya China sasa inasema itaingiza rasilimali na fedha zaidi katika miradi ya utafiti ili kuelewa mahitaji ya wananchi barani Afrika. Utawala huo wenye makao yake jijini Beijing unasema kuwa ufahamu mwafaka kuhusu bara hilo lilatoa nafasi nzuri kwa taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Asia kutoa mchango wake na msaada dhabiti katika jitihada zake za kusaidia hali ya maisha katika Afrika.

    • China yaadhimisha tamasha la mbalamwezi 2017-10-07

    China inafahamika kwa uaminifu wake kwa mila za tangu jadi. Taifa hilo kubwa zaidi barani Asia kwa kweli imesifika kwa utajiri wa tamaduni. Mila hizi kwa njia nyingi zimezidi zile za nchi nyingine. Sifa mojawapo ya kipekee ya watu wa China, ni kujitolea kwao kuhadhimisha sherehe za mabadiliko ya hali ya hewa. Tamaduni hizi zimekuzwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

    • BRICS yaelekeza macho yake kwa mataifa yanayoendelea Afrika 2017-09-04

    Kenya ni miongoni mwa mataifa yanayoshiriki mkutano wa BRICS unaoendelea Mkoani Fujian, eneo la Xiamen nchini China. Nchi hiyo kutoka Afrika Mashariki ilialikwa kushiriki katika mkutano huo kwa mara ya kwanza kabisa huku ikidhihirika kwamba kongamano hilo linabadili mwelekeo na kutaka kuvutia mataifa yanayoendelea barani Afrika.

    • Hifadhi ya Summer Palace, kivutio cha Utamaduni na Utalii  2017-07-24

    Hifadhi ya Summer Palace mjini Beijing inajumuisha ziwa kubwa bandia, kisiwa na kilima vilivyotengenezwa na binadamu.

    • Taasisi zaungana kuzuia kuenea kwa maradhi ya Ukimwi Afrika 2017-07-14
    Juhudi za kimataifa za kuzuia maambukizi na kuenea kwa maradhi ya ukimwi unashika kasi. Jicho la dunia sasa linaangazia juhudi za kuwashawishi watu wengi iwezekanavyo ili kujua hali zao.
    • China inakuza sekta ya nishati mbadala kupigana na uchafuzi wa mazingira 2017-07-12

    China inazidi kupunguza utegemezi wake juu ya makaa ya mawe kama nguvu ya nishati, badala yake inaendeleza miradi ya vyanzo vya umeme mbadala. Ujenzi wa mitambo ya upepo na umeme wa jua kwa sasa inafanyika katika karibu mikoa yote ya taifa hilo ya mashariki ya mbali. Utegemezi wa nishati inayotokana na makaa ya mawe imetajwa kama moja ya sababu kuu ya uchafuzi wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi kama inavyoshuhudia nchini China. Viwanda vya uzalishaji wa umeme kupitia makaa ya mawe kwa sasa vinapunguzwa kwa kasi kubwa.

    • Inner Mongolia yapanua biashara na Afrika huku China ikitafuta mahusiano zaidi 2017-07-03

    Jimbo la Mongolia ya ndani ipo kaskazini mashariki mwa China katika mpaka wa Mongolia na Urusi. Si mengi yametangazwa kuhusu mkoa huu lakini umesajili maendeleo makubwa tangu kiongozi Deng Xiaoping kuweka mageuzi ya kiuchumi China mwaka 1978.

    • Mafanikio na uzoefu wa China katika kupunguza umaskini 2017-06-20

    "LAZIMA tuondoe umaskini ambao upo katika akili zetu kabla ya kuuondoa ndani ya maeneo tunaotawala, kabla ya kusaidia raia na taifa kutoka kwenye minyororo ya umaskini na kuanza barabara ya mafanikio." Haya ni maneno ya kiongozi wa China Xi Jinping katika kitabu chake maarufu "Kuondokana na Umaskini." Kitabu hiki kinatoa maelezo ya kina kuhusu jinsi yeye alifanikiwa kukabiliana na kushinda vita dhidi ya umaskini kama kiongozi katika Ningde, moja ya sehemu ya Mkoa wa Fujian iliyokuwa na umaskini zaidi katika miaka ya 1980.

    • Maendeleo na ujenzi wa kihistoria China baada ya tetemeko la ardhi 2017-06-16

    JE, utafanya nini iwapo tetemeko la ardhi wenye ukubwa wa 8.0 kwenye Richter utazuka na kufanya uharibifu mkubwa na kuleta pigo mijini na vijijini? Mbaya zaidi, unaweza kufanya nini wakati vitetemeko zaidi vinaendelea kwa maeneo yaliyokaribu kwa miezi kadhaa baada ya tetemeko hilo kuu na kusababisha majeruhi zaidi na uharibifu?

    • China yasema mpango wa Ukanda Mmoja na Njia Moja ni njia rahisi ya kusaidia nchi wanachama 2017-06-15
    Beijing imesisitiza kuwa mpango wa kiuchumi wa karne ya 21 wa Ukanda Mmoja na Njia Moja ni mfumo bora mno ambayo China itatumia kutoa msaada wake kwa nchi zinazoendelea ambazo zimeamua kushirikiana na taifa hilo lenye uchumi mkubwa zaidi barani Asia.
    • Kenya kutafuta fursa ya biashara zaidi na China kupitia mpango wa Mkanda Mmoja Njia Moja 2017-06-09
    Nairobi imetangaza kuwa itaanza kuwinda nafasi za biashara zaidi na Beijing kupitia mpango wa kiuchumi uliozinduliwa karibuni wa Mkanda Mmoja Njia Moja. Waziri wa biashara na viwanda wa Kenya Adan Mohamed anasema mfumo huu unaofuata barabara ya kale ya Silk ambao una mizizi yake China utahusisha matrilioni ya dola ya uwekezaji na miradi mikubwa muhimu katika kila moja ya nchi husika.
    • Makampuni kutoka China yaahidi fursa zaidi Afrika kupitia mfumo wa Mkanda Mmoja Njia Moja 2017-06-06
    Wiki tatu tu baada ya kumalizika kwa kongamano la kwanza kabisa kuhusu Mkanda Mmoja Njia Moja mjini Beijing, makampuni makubwa ya Kichina yameelezea utayari wao wa kuongeza uwekezaji katika nchi ambazo hadi sasa yamejiunga katika mpango huo.
    • Wachina Waadhimisha tamasha la Duanwu 2017-05-31

    Wachina wanaadhimisha sherehe ya siku tatu kwa kuandaa tamasha la Duanwu maarufu kama Dragon Boat Festival. Tamasha hili linaandaliwa kukumbuka mshairi mkubwa tajika ambaye alipigana dhidi ya mateso ya raia maelfu ya miaka iliyopita.

    • Mchango wa dola milioni 20 kutoka China wa Uhifadhi Mazingira na Wanyamapori Afrika 2017-05-26

    Serikali ya China imedhihirisha nia yake kubwa ya kuhifadhi mazingira na wanyamapori kwa kuongeza fedha kwa sekta hii Afrika kwa dola milioni 20 za Marekani. Toleo hili ni mara mbili ya kiasi cha fedha zilizoahidiwa mwaka wa 2014 na nchi hiyo yenye uchumi mkubwa zaidi barani Asia.

    • Waziri wa Usafiri Kenya asema matunda ya Mkanda Mmoja Njia Moja tayari yanaonekana 2017-05-22

    Mwezi Mei, duniani yote ilielekeza macho yake kuelekea Mjini Beijing kwa sababu ya tukio kubwa ya kihistoria iliyokuwa ikiendelea katika mji huo mkuu wa China. Serikali mbalimbali na mashirika ya kimataifa yalikuwa hapa kushuhudia kuzaliwa kwa mpango wa maendeleo wa Mkanda Mmoja Njia Moja.

    1  2  3  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako