• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Kasri la Potala la Tibet lahifadhiwa vizuri
    Mkoa wa Tibet uko katika uwanda wa juu wa Qinghai-Tibet. Mkoani humo si kama tu kuna mandhari nzuri ya asili, bali pia kuna mabaki mengi ya utamaduni. Tangu mageuzi ya demokrasia yafanyike mwaka 1959 mkoani Tibet, serikali kuu ya China na serikali ya mkoa wa Tibet zimefanya juhudi kubwa za kuhifadhi mabaki ya kale ya utamaduni mkoani humo.
    • Kauli mbiu ya Maonesho ya kimataifa ya Shanghai
    Maonesho ya kimataifa ya mwaka 2010 yatakayofanyika huko Shanghai, mji uliopo mashariki ya China yatafanyika kwa siku 184 kuanzia tarehe 1 Mei hadi tarehe 31 Oktoba,. inakadiriwa kuwa maonesho hayo yatavutia watembezi wapatao milioni 70 kote duniani, na kauli mbiu ya maonesho hayo ni "Miji bora zaidi, maisha bora zaidi". Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa China kuandaa maonesho ya kimataifa, na kauli mbiu hiyo ina umuhimu mkubwa katika hali halisi kwa hivi sasa.
    • Wanakijiji wa Fengdu wapambana na ukame
    Kuanzia kipindi cha majira ya joto mwaka jana, sehemu tano za kusini magharibi mwa China zilikumbwa na maafa ya ukame ambayo hayakutokea hapo awali. Wilaya inayojiendesha ya makabila ya Wamiao na Wabuyi ya Qianxinan mkoani Guizhou ilikumbwa na ukame zaidi, kuanzia mwezi Agosti mwaka 2009 mvua haikunyesha kabisa.
    • Mwanzo mpya wa mtangazaji wa Uingereza nchini China
    Bibi Susan Osman alikuwa mtangazaji mwanamke maarufu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC, hivi sasa anafanya kazi katika Radio China Kimataifa, na kuwa mtangazaji wa kipindi kipya cha habari Beijing Hour.
    • Hali ya wanafunzi wengi wenye umri mdogo kusoma katika nchi za nje yafuatiliwa nchini China
    Mwaka jana wanafunzi wapatao laki 2.3 wa China walikwenda nje kuendelea na masomo yao, idadi ambayo imeongezeka kwa asilimia 30, na kati ya wanafunzi hao wahitimu wa shule za sekondari walichukua asilimia kubwa.
    • Mzee mwenye umri wa miaka 70 aanzisha duka la kushona nguo
    Kutokana na misaada ya "mikopo midogo" na "kituo cha kusaidia biashara" inayotolewa na Shirikisho la wanawake la Tianjin, wanawake wengi mjini Tianjin wamepata ajira na hata wameanzisha shughuli zao kwa mafanikio.
    • Wageni watapata huduma za afya zitakazotolewa na upande wa tatu wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Shanghai
    Kama tujuavyo, maonesho hayo yatakayofunguliwa tarehe 1 Mei yanatazamiwa kuwavutia watalii milioni 70 kutoka nchi mbalimbali duniani. Je, watalii wakikumbwa na ajali au kusumbuliwa na tatizo la kiafya wakati wanapotembelea maonesho ya kimataifa, watasaidiwa vipi? Katika kipindi cha leo, tutawaelezea jinsi huduma za afya zitakazotolewa na upande wa tatu wakati wa maonesho hayo zitakavyowasaidia watalii.
    • Wajumbe wa baraza la mashauriano ya kisiasa watoa mapendekezo kuhusu maendeleo ya uchumi katika sehemu za makabila madogo madogo yenye watu wachache
    Mkutano wa baraza la mashauriano ya kisiasa umefungwa hivi karibuni nchini China. Kwenye mkutano huo wajumbe kutoka sehemu za makabila madogo madogo yenye watu wachache walitoa mapendekezo mbalimbali kuhusu maendeleo ya uchumi katika sehemu hizo. Nchini China kati ya makabila 55 madogo madogo, kuna makabila 22 yenye watu wasiofikia laki moja, na makabila hayo yanajulikana kuwa makabila madogo madogo yenye watu wachache.
    • Wanawake watimiza ndoto za kuanzisha shughuli zao
    Mikopo midogo inatatua suala la fedha kwa wanawake wanaoanzisha shughuli zao, lakini mwanzoni wakati wanaanzisha shughuli zao, huwa wanakabiliwa na changamoto nyingine mbalimbali. Ili kuwasaidia wanawake hao kukabiliana na changamoto hizo, "kituo cha kusaidia biashara" kilianzishwa, ambacho lengo lake ni kuyasaidia makampuni ambayo yako katika hatua ya mwanzo, ili ndoto ya wanawake kuhusu kuanzisha shughuli zao itimizwe.
    • Bibi Wang Ge na ustadi wake wa kukata picha za karatasi
    Katika mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uyghur ulioko kaskazini magharibi mwa China, kuna wakazi wa makabila 13 yakiwemo makabila ya Wauyghur, Wakazakh, Wamongolia, Wahui, Wahan na Waman. Tokea zamani, watu wa makabila hayo tofauti wameishi pamoja kwa urafiki na mshikamano...
    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako