• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Tanzania yapokea watalii 120 toka Hong Kong, China 2019-08-01

    SEKTA ya utalii nchini Tanzania inazidi kukua baada ya kupokea watalii 120 kutoka Hong kong, China kuwasili nchini kwa ajili ya kutembelea hifadhi mbalimbali za Taifa na maeneo mbalimbali yenye vivutio vya utalii nchini.

    • Chama cha Waajiri Tanzania watoa elimu Sheria za Kazi na Ajira kwa Wafanyabiashara toka China 2019-07-30

    Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) wamefanya mkutano na wafanyabiashara toka China kwa lengo la kujadili fursa za uwekezaji nchini pamoja na sheria ya kazi na ajira pamoja na kujadili changamoto za kibiashara wanazokutana katika uwekezaji wao.

    • Wafanyabiashara Tanzania kufanya ziara ya mafunzo China 2019-07-29

    HUKU uhusiano wa kibishara na uwekezaji ukizidi kukukua na kuimarika kati ya Tanzania na China, wafanyabiashara kutoka Mkoani Mtwara, kusini mwa nchi hiyo ya Afrika ya Mashariki, wanatarajia kutembelea China hivi karibuni ili kujifunza fursa mbalimbali za kibiashara zikiwemo za uwekezaji wa viwanda ili kuendana na kasi ya Tanzania ya viwanda.

    • China yawezesha Tanzania kuwa ya kwanza Afrika Mashariki kutibu moyo unaokwenda mbio kwa kuipatia mashine yenye thamani ya Shilingi milioni 500 2019-07-29

    CHINA imewezesha Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki kutibu wagonjwa wa moyo ambao unakwenda mbio baada ya mfumo wa umeme wa moyo kuharibika, tatizo ambalo wagonjwa walikua wakipelekwa nje kupata matibabu .

    • Balozi mdogo wa China Zanzibar asema Misaada ya China Zanzibar inalenga kuimarisha uchumi na huduma za jamii kwa wananchi 2019-07-29

    SERIKALI ya Jamhuri ya Watu wa China imesema misaada yake inayotoa inalenga katika kuimarisha uchumi na huduma za jamii kwa wananchi wa Zanzibar.

    • Tanzania yaanza kutumia mbinu ya kutokomeza Malaria iliyotumika China kutokomeza ugonjwa huo mikoa ya Kusini 2019-07-27
    TANZANIA imeanza kutekeleza mradi wa kutokomeza malaria kwenye mikoa ya kusini kwa kutumia mbinu iliyotumika kuutokomeza nchini China.
    • Rais Magufuli ahaidi kuboresha utendaji kazi wa Reli ya kihistoria Ushirikiano Afrika na China ya TAZARA 2019-07-27
    RAIS John Magufuli amesema Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) halitakufa kwa sababu wazo la shirika hilo ni la kihistoria baina ya nchi husika.
    • Kampuni ya China yasaini mkataba kuongeza watalii na uwekezaji Zanzibar 2019-07-23

    WIZARA ya habari Utalii na Mambo ya kale imetiliana saini makubaliano ya kuimarisha uhusiano katika sekta ya utalii na kampuni ya kimataifa ya touchroad kutoka jimbo la Zhejiang ya China yenye lengo la kuongeza idadi ya wa watalii wanaokuja zanzibar kutoka nchi hiyo.

    • Wafanyabiashara 25, kutoka Kampuni 15 za Jimbo la Zhejiang China kufanya ziara ya siku tatu kusaka fursa za biashara Tanzania 2019-07-22

    UWEKEZAJI wa China kwa anzania mwaka jana umefikia dola za Marekani Bilioni saba na kufanya nchi hiyo kuendelea kuongoza kwa uwekezaji nchini kwa kuwa na kampuni 200 zilizowekeza na kutoa huduma nchini hadi sasa,ambazo wawakilishi wake walipata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo.

    • Xinhua, TSN wakubaliana kudumisha ushirikiano na kukuza Kiswahili 2019-07-22

    USHIRIKIANO baina ya Vyombo vya habari China na Tanzania unazidi kushika kasi baada ya Shirika la Habari la China, Xinhua na Kampuni ya Magazeti ya Serikali Daily News, Habari Leo (TSN), zimezidi kudumisha ushirikano ikiwa ni pamoja na kuendeleza programu ya lugha ya Kiswahili kwa Wachina.

    • Sekta ya Utalii China inavyobebwa na Wachina Wenyewe 2019-07-16

    UTALII nchini China ni sekta muhimu kwa maendeleo ,unaochangiwa na raia wenyewe wa nchi hiyo kutokana na kuwa na vivutio vya kila aina ikiwemo maeneo ya historia mbalimbali kuanzia dini,siasa,maendeleo ukuaji wa miji na mengineo imekuwa vivutio katika miji mbalimbali nchini humo huku idadi kubwa ya watalii wakiwa ni kutoka ndani ya nchi hiyo tofauti na nchi nyingine.

    • Wanafunzi wa kidato cha nne katika sekondari 16 Tanzania kufanya mtihani wa taifa wa somo la lugha ya kichina mwaka huu 2019-07-15

    KATIKA kuhaikikisha Tanzania inakuwa na wataalamu katika lugha ya kichina kwa wananchi wake kwa mara ya kwanza mwaka huu, wanafunzi wa shule 16 za Sekondari nchini wanatarajia kulifanyia mtihani wa taifa wa kidato cha nne wa somo hilo baada ya kufundisha miaka

    • DIT kuzalisha wataalamu wa Teknolojia na Ufundi kwa kushirikiana na Chuo Cha Teknolojia na Ufundi cha Nanning China 2019-07-12

    TANZANIA kupitia Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) imesaini makubaliano ya ushirikiano katika nyanja mbalimbali za utoaji wa elimu na Chuo cha Teknolojia na Ufundi 'Nanning' kutoka nchini China kusaidia kuzalisha wataalam wenye weledi wa kutosha katika fani zote zinazofundishwa katika taasisi hiyo.

    • Tanzania na China kushirikiana kuendeleza utamaduni wa nchi hizo 2019-07-12

    SERIKALI ya Tanzania imehaidi itaendelea kutambua mchango wa China na kushirikiana nao katika kukuza utamaduni na sanaa nchini.

    • China yawapatia wanawake wa mikoa sita Tanzania vyerehani 330 na kutoa vifaa 380 kwa watu wenye ulemavu 2019-07-01

    CHINA imetoa msaada wa vyerehani 330 kwa vikundi vya wanawake katika mikoa sita na vifaa 380 vya watu wenye ulemavu vyote vikiwa na thamani ya Dola za Marekani 51,617 (takribani Sh milioni 121.3).

    • Wakandarasi China kukamilisha gati bandari ya Mtwara mwisho wa mwaka 2019-06-18

    WAKANDARASI wa kampuni toka nchini China, China Railway Construction Engineering Group (CRCEG) na China Railway Major Bridge Engineering Group Co. Ltd (CRMBEG) wanaojenga gati namba mbili katika bandari ya Mtwara watakamilisha ujenzi mwishoni mwa mwaka huu.

    • Tanzania kushiriki michuano ya vijana chini ya miaka 11 China 2019-06-18

    Tanzania ni kati ya nchi nne Afrika zitakazopeleka timu za vijana walio na umri wa chini ya miaka 11 katika mashindano yatakayofanyika nchini China kuanzia Juni 23 hadi 30 mwaka huu.

    • UDSM na Chuo Kikuu cha Beijing kushirikiana utoaji mafunzo katika sheria 2019-06-11

    UHUSIANO baina ya China na Tanzania unazidi kukua katika sekta mbalimbali hivyo kuimarisha ushirikiano wa nchi hizo wenye historia ya takribani miaka 55 iliyopita bila kuwa na changamoto mbalimbali.

    • Kampuni ya Magazeti ya serikali Tanzania (TSN) yatuzwa na gazeti la China Daily kwa ushirikiano China 2019-06-11

    KAMPUNI ya Magazeti ya Serikali (TSN), imepongezwa kwa ushirikiano wake kwa vyombo vya habari vya kimataifa, likiwemo gazeti la China Daily linalochapishwa kila siku nchini China.

    • Watalii 343 toka China watembelea vivutio vya utalii Tanzania na kuvitangaza nchini mwao kupitia mkakati wa 'Tour Africa New Horizon' 2019-05-14

    VIVUTIO vya Utalii nchini Tanzania ,vitaanza kutangazwa nchini China baada watalii 343 kuwasiliTanzania kutoka China ikiwa ni matokeo ya uzinduzi wa mkakati unaojulikana kama 'Tour Africa New Horizon'.

    • Watalii 343 toka China watembelea vivutio vya utalii Tanzania na kuvitangaza nchini mwao  kupitia  mkakati wa "Tour Africa New Horizon" 2019-05-14

    VIVUTIO vya Utalii nchini Tanzania ,vitaanza kutangazwa nchini China baada watalii 343 kuwasiliTanzania kutoka China ikiwa ni matokeo ya uzinduzi wa mkakati unaojulikana kama "Tour Africa New Horizon".

    • Tanzania kujifunza katika jimbo la Hebei China kutangaza rasilimali zilizopo kuvutia watalii 2019-05-07

    TANZANIA na Jimbo la Hebei lililopo nchini China wamekutana kubadilishana uzoefu kuhusu namna ya kuongeza idadi ya watalii wa pande hizo mbili .

    • Wataalamu China wakamata ajira zaidi ya 100,000 EAC, Tanzania, Kenya zaongoza 2019-05-05

    NCHI za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zimekuwa fursa kubwa ya ajira kwa wataalamu wa taifa la China, baada ya kutoa ajira zaidi ya 123,524. Ajira hizo ni kupitia kandarasi za miradi mbalimbali ya miundombinu ya barabara, viwanda na nishati.

    • Uhusiano wa Kidplomasia China na Tanzania wafikia miaka 55 kwa mafanikio lukuki 2019-04-26

    TANZANIA na China zimeadhimisha miaka 55 ya ushirikiano wa kidiplomasia na kuhakikisha kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

    • Biashara kati ya China na Tanzania yazidi kukua yafikia dola bilioni nne kwa mwaka 2019-04-19

    UHUSIANO wa China na Tanzania kiuchumi na kidplomasia unazidi kukua kila mwaka kutokana na mwaka jana biashara baina ya China na Tanzania kufikia dola za Marekani bilioni 3.976 ikiwa ni ukuaji kwa asilimia 15.

    • China tayari kusaidia fedha uboreshaji reli ya Tazara, kulinda historia na Afrika 2019-04-11
    • Tanzania yaadhimisha "Qingming Festival" kwa kuwakumbuka raia wa China waliofariki wakati wa ujenzi wa TAZARA 2019-04-07

    Ijumaa April 5, mwaka huu Tanzania iliungana na China kuadhimisho sikukuu za kijadi ijulikanayo kama "Qingming Festival" pia inatambulika kama siku ya kufagia makaburi na kukumbuka watu mbalimbali waliokufa.

    • Tanzania kufungua ubalozi mdogo Guangzhou, China 2019-04-07

    Urafiki na ushirikiano wa miaka mingi baina ya China na Tanzania umeendelea kuimarika kila kukicha kwa kuwepo ushirikiano wa masuala ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

    • China kupambana na watengenezaji na wasafirishaji bidhaa zisizo na Ubora yakubaliana na Tanzania kuweka mikakati ya pamoja kuwanasa 2019-03-19

    BIDHAA zisizo na ubora imekuwa changamoto kubwa kwa nchi mbalimbali duniani hususan katika ukanda wa Afrika kwa kiasi fulani bidhaa hizo zimekuwa zikiingia au kutengenezwa kwa wingi.

    • Watalii 10,000 wakiwemo watu mashuhuri toka China kutembelea Tanzania mwaka huu 2019-03-14

    MWAKA huu China na Tanzania zinaadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kibalozi huku uhusiano huo ukiwa umedumu kwa amani na kusaidia katika Uhusiano katika sekta mbalimbali ikiwemo kifedha, Kibiashara, Utamaduni, miundombinu, utalii na mengineyo.

    1  2  3  4  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako