• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • China yatangaza fursa ya vijana wa Tanzania kupata uzoefu wa maandiko ya biashara ili kujiajiri 2020-01-17

    CHINA imetangaza fursa kwa vijana wa Tanzania kwenda nchini China kuongeza uzoefu maandiko ya kibiashara ili waweze kujiajiri kuliko kutegemea kuajiriwa na Serikali.

    • Madaktari toka China watoa msaada wa dawa na vifaa tiba vyenye thamani ya milioni 15 kwa Taasisi ya Moyo JKCI 2019-12-30

    MADAKTARI toka china wanaofanya kazi nchini Tanzania wametoa msaada wa vifaa tiba na dawa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

    • Mashirika yasiyo ya kiserikali ya Tanzania na China yasaini mkataba kushirikiana kuondoa umasikini 2019-12-30

    MASHIRIKA yasiyo ya kiserikali saba kwa kila nchi kutoka Tanzania na China yamesaini mkataba wa ushirikiano katika nyanja tofauti kwa lengo la kuondoa umasikini.

    • Kampuni toka China kuwasili Februari mwakani kusaka bidhaa za nyama na ngozi Tanzania 2019-12-23

    KAMPUNI ya serikali ya China inayojishughulisha na bidhaa za Nyama na Ngozi inatarajia kuwasili nchini Tanzania mwezi February Mwakani ili kuangalia namna ya kukamata soko la bidhaa hizo nchini.

    • China yaipa Zanzibar misaada ya Sh bilioni 306 katika miaka tisa 2019-12-23

    SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kipindi cha miaka tisa imefaidika na misaada mbalimbali ya kuleta maendeleo inayotolewa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China yenye gharama ya Sh Bilioni 306 iliyosaidia kuleta maendeleo na kukuza uchumi na ustawi wa wananchi wake.

    • Hospitali ya Bugando yaokoa bilioni 1 kwa kununua kontena sita zenye vifaa tiba, madawa na vitendea kazi toka China 2019-12-17

    HOSPITALI ya Rufaa ya Kanda, Bugando Medical Centre (BMC) imeokoa Sh. Bilioni moja baada ya kuagiza vifaa tiba, madawa na vitendea kazi kutoka nchini China.

    • Mtanzania ashinda tuzo China kwa kubuni chakula cha samaki cha gharama nafuu 2019-12-10

    MWANAFUNZI wa Kitanzania Amos Benjamin aliyepata ufadhili toka serikali ya China mwaka 2017 na kuhitimu Chuo Kikuu cha Kilimo China mwezi uliopita ametunukiwa tuzo kutokana na ubunifu wa teknolojia ya ufugaji samaki maarufu "2019 UNLEASH Award for Innovative Fish Farming Technology" katika Shindano lililofanyika Shenzhen China.

    • China yatoa Sh. Bilioni 19.4 kujenga chuo cha ufundi Kagera 2019-12-02

    SERIKALI imezindua ujenzi wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma cha mkoani Kagera kilichofadhiliwa na Jamhuri ya Watu wa China kwa Shilingi bilioni 19.4.

    • Watanzania 17000 wanajifunza lugha ya Kichina 2019-11-26

    VIJANA wa Tanzania 1700 wanajifunza lugha ya kichina nchini huku wachina 10 kila mwaka wakijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kusoma lugha ya Kiswahili.

    • Watanzania 1700 wanajifunza lugha ya Kichina 2019-11-25
    VIJANA wa Tanzania 1700 wanajifunza lugha ya kichina nchini huku wachina 10 kila mwaka wakijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kusoma lugha ya Kiswahili.
    • Taifa la China halikwepeki katika maendeleo -Spika Ndugai 2019-11-22

    SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amesema katika dunia ya sasa Taifa la China halikwepeki katika masuala ya ushirikiano wa kiuchumi, hivyo akaishauri Serikali ya Tanzania kutumia fursa hiyo kunufaika kiuchumi.

    • China yaipa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) magari 12 2019-11-13

    CHINA imeahidi kuipa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) magari 12 yenye thamani ya dola za Marekani US$400,000 ili kutumika katika programu mbalimbali za kuwajengea jamii uwezo.

    • China yawapa wanakijiji mbegu kompyuta 2019-11-11

    BALOZI wa China nchini Tanzania Bibi Wang Ke amekabidhi msaada wa mbegu za Alizeti, Choroko na Mahindi zenye uzito wa kilo 4800 ambazo zitagaiwa kwa wananchi wa kijiji Mhenda kilicho jirani na Hifadhi ya Taifa Mikumi mkoani Morogoro.

    • Tanzania inathamini mchango wa China-Balozi Mahiga 2019-10-24

    WAZIRI wa Katiba na Sheria, Balozi Augustine Mahiga amesema Tanzania itaendelea kuthamini mchango unaotolewa na Jamhuri ya Watu wa China huku akisisitiza kuwa masuala yanayoendelea hivi sasa ambapo Hong Kong inataka kujitenga, yanapaswa kushughulikiwa na China yenyewe.

    • Ujumbe toka jimbo la Hebei China kuwekeza mkoani Pwani 2019-10-24

    UJUMBE kutoka China ukishirikisha wawekezaji na maofisa wa serikali uMEwasili mkoani Pwani kusaka maeneo ya uwekezaji huku wakitembelea maonesho ya viwanda yanayoendelea mkoani hapa.

    • China Academy of Building Research yaanza upembuzi yakinifu mradi wa upanuzi Taasisi ya Moyo ya JKCI Mloganzila 2019-09-17

    UJUMBE wa wawakilishi kutoka China Academy of Building Research wamefika nchini kwa ajili ya kupata taarifa zinazohusiana na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa upanuzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), awamu ya pili katika eneo la Mloganzila Jijini Dar es Salaam.

    • Jeshi China lamkabidhi Rais Magufuli magari 40 ya JWTZ 2019-09-16

    JESHI la Ukombozi wa watu wa China (PLA) limekabidhi Jeshi la Ulinzi la wananachi wa Tanzania (JWTZ) magari 40.

    • UDSM yajivunia uhusiano Tanzania na China kuleta manufaa ya kielimu 2019-09-16

    CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimejivunia manufaa ya kielimu waliyopata kutokana na wahadhili na wanafunzi wake kwenda kusoma nchini China katika fani mblimbali.

    • China yatoa mafunzo ya Upishi na ukarimu Zanzibar 2019-09-16
    • Kampuni ya Kimataifa ya Hongwei toka China yaajiri vijana 514 kuchakata mazao ya misitu Mufindi 2019-08-30
    • Madaktari bingwa waliosoma China Wafanya kampeni ya  upimaji magonjwa yasiyoambukiza Kisarawe 2019-08-30
    WAKAZI wa Kisarawe mkoani Pwani, takribani 1,000 watanufaika na kambi ya kwanza ya kampeni ya uchunguzi na matibabu dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza, inayotolewa na madaktari bingwa wa Jumuiya ya Watanzania Waliosoma China (DCAT).
    Mwenyekiti wa DCAT, Dk. Liggyle Vumilia anasema katika siku hizo tatu, watachunguza afya watu 600 hadi 1,000 wa magonjwa ya saratani, moyo, kisukari na mengineyo.
    • Vijana 20 Tanzania wajiunga na sanaa ya Wing Chun toka China 2019-08-30

    VIJANA 20 kutoka eneo la Murieti jijini Arusha wamejiunga katika Sanaa mpya ya mapigano iliyoanzishwa ijulikanayo Kama 'Wing Chun'.

    Mwanzilishi na mkufunzi was Sanaa hiyo Rashid Said amesema kuwa ni mchezo mpya umeingia kwa Kasi nchini kutokana na vijana kuuelewa haraka.

    Alisema asili ya Wing Chun ni nchini China na unaendelea kusambaa maeneo mbalimbali ni miongoni mwa michezo ambayo inafundishwa kihalali na umesashasajiliwa.

    • China yaweka rekodi kwa kutokuwa na maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwa miaka mitatu 2019-08-23

    China, nchi inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu duniani, ikiwa na watu zaidi ya bilioni 1.4, huku ikiwa nchi ya pili kwa uchumi mkubwa duniani, imefanikiwa kwa miaka mitatu kuhakikisha hakuna maambukizi ya malaria nchini humo, na itafikia malengo ya milenia ya kutokomeza maambukizi ya ugonjwa huo hadi kufikia mwaka 2020.

    • China yaongeza ufadhili kwa wanafunzi wa fani mbalimbali Tanzania kufikia 259 kwa mwaka 2019-08-22

    UFADHILI kutoka nchini China kwa wanafunzi wa Tanzania wanaosoma fani mbalimbali nchini humo imeongezeka mara mbili zaidi mwaka huu kutoka wanafunzi 120 mpaka 259 mwaka jana .

    • Balozi wa China nchini Tanzania ataka taasisi za Confucius kufundisha Kiswahili 2019-08-22

    LUGHA ni muhimu katika mawasiliano ikiwemo kubadilishana tamaduni za aina mbalimbali,biashara,utalii na muingiliano wa watu katika dunia hii ambayo kwa sasa imekuwa kama kijiji kwa mtu wa eneo moja kwenda kuishi au kufanya shughuli mbalimbali katika eneo lingine.

    • China yatoa samani za Ofisini kwa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) huku Balozi wake akipongeza serikali kuboresha mazingira ya uwekezaji 2019-08-19

    BALOZI wa China nchini Wang Ke amepongeza jitihada za serikali katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini na kueleza kuwa mwaka huu mambo mengi yamefanyiwa kazi hivyo anatarajia wawekezaji zaidi nchini hususan kutoka nchini China.

    • Vigae "Tiles" za Tanzania zinazozalishwa na mwekezaji toka China zakamata soko Afrika Mashariki 2019-08-16

    KIWANDA cha kutengeneza vigae "Tiles" nchini cha Goodwill Tanzania Ceramic Limited kilichopo katika Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani,kinachomilikiwa na mwekezaji toka China kimeshika soko katika ukanda wa Afrika Mashariki.

    • China yaipa Tanzania Milioni 217 kusaidia shughuli za kiofisi wakati wa mkutano wa SADC 2019-08-16

    CHINA imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ofisini vyenye thamani ya zaidi ya milioni 217 kwa ajili ya shughuli mbalimbali za ofisini wakati wa mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa afrika (SADC).

    • Zanzibar yanunua meli mpya ya Mafuta iliyowasili kutoka Shanghai China 2019-08-09

    SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imetimiza ahadi yake kwa wananchi wake ya kununua meli mpya ya mafuta MT Mkombozi II, baada ya meli hiyo kuwasili katika Bandari ya Zanzibar ikitokea Shanghai nchini China.

    • Kampuni ya CHICO kutoka China yasaini mkataba ujenzi barabara Tanga-Pangani 2019-08-05

    KAMPUNI ya China Henan International Company Limited (CHICO) imesaini mkataba wa ujenzi sehemu ya barabara ya Tanga- Pangani yenye urefu wa kilometa 50.

    1  2  3  4  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako