• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Huawei yachukua hatua kali kujibu vikwazo ilivyowekewa na Marekani 05-19 19:07
    • Marekani yapoteza uaminifu kufuatia vitendo vyake
     05-17 17:12

    Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Mataifa inasema, ikiwa nchi ya pili inayolipa ada zaidi kwa Umoja wa Mataifa, China imelipa ada zote za asilimia 12.01 ya bajeti ya umoja huo. Msemaji wa katibu mkuu wa umoja huo Bw. Stefan Dujarric ameishukuru China kwenye Twitter akitumia neno la kichina "Xiexie", lenye maana ya asante. Kwa upande wa Marekani, hadi tarehe mosi Januari mwaka huu, imechelewa kulipa ada ya kawaida ya Umoja wa Mataifa ambayo ni dola za kimarekani milioni 381, na ada ya kijeshi dola milioni 776.

    • China si adui wa kweli wa Marekani 05-16 19:48

    Hivi karibuni Steve Bannon aliyekuwa mshauri wa juu wa kimkakati wa rais wa Marekani alitunga makala ndefu, akisema China imekuwa adui mkuu wa Marekani, na kutaka serikali ya Marekani isirudi nyuma katika vita vya kiuchumi na China. Lakini Makala hiyo ikichambuliwa kwa undani, ni wazi kuwa haina msingi na mantiki sahihi. Wanasiasa wa mrengo wa kulia wanachochea migongano kati ya Marekani na nchi nyingine, na hao ndio maadui wa kweli wa Marekani.

    • Rais wa China ahutubia ufunguzi wa mazungumzo ya ustaarabu ya Asia
     05-15 20:04

    Mazungumzo ya ustaarabu ya Asia leo yamefunguliwa hapa Beijing. Rais Xi Jinping wa China amehudhuria ufunguzi huo na kutoa hotuba ya "kuzidisha mawasiliano ya ustaarabu, na kujenga jumuiya ya Asia yenye hatma ya pamoja".

    • Marekani yajidanganya kwa kusema inaibiwa
     05-15 20:03

    Hivi karibuni baadhi ya wanasiasa wa Marekani wanadai kuwa nchi hiyo ni kama sanduku la kuhifadhi pesa, na nchi nyingine zote ikiwemo China zinaiba pesa kutoka kwake, jambo linalodhihirisha kuwa wanaosema hivyo hawana ufahamu mpana kuhusu masuala ya uchumi.

    • Tahariri ya CMG yafafanua nia na nguvu ya China katika vita vya kibiashara na Marekani 05-14 20:22

    Tahariri iliyotolewa jana na televisheni ya Shirika kuu la Utangazaji la China CGM. Tahariri hiyo inayozungumzia vita vya kibiashara vilivyochochewa na Marekani na msimamo wa China imefuatiliwa sana na watazamaji wa China.

    • Skinner wa Marekani ahimizwa kutopaka matope ustaarabu
     05-14 16:45

    Mkurugenzi wa ofisi ya mambo ya mipango ya sera ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani Bibi Kiron Skinner hivi karibuni alisema, ushindani kati ya Marekani na China ni mgongano kati ya staarabu tofauti. Kauli hiyo imewashangaza wamarekani na dunia nzima, na wengi wanaona kuwa, kauli hiyo inapaka matope ustaarabu, na kuifanya wizara ya mambo ya nje ya Marekani iwe kama mchekeshaji.

    • Bei za hisa katika Soko la hisa la New York zaporomoka kutokana na mgogoro wa kibiashara kati ya China na Marekani 05-14 10:39
    • Rais wa China ahimiza mazungumzo ya ustaarabu ya Asia
     05-13 18:39

    Miaka mitano iliyopita, rais Xi Jinping wa China alipendekeza kufanyika kwa mazungumzo ya ustaarabu ya Asia, na tarehe 15 pendekezo hilo litatimizwa. Wajumbe kutoka nchi 47 za Asia pamoja na wasomi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa watakutana hapa Beijing, na kufanya mazungumzo yenye kauli mbiu ya "kuwasiliana na kuigana katika mambo ya ustaarabu, na jumuiya yenye hatma ya pamoja".

    • UCHAMBUZI: Kutilia maanani yanayofuatiliwa na kila upande ni msingi wa kutatua mikwaruzano ya kiuchumi na kibiashara 05-11 10:36
    Mazungumzo ya duru ya 11 ya mambo ya kiuchumi na kibiashara kati ya China na Marekani yalimalizika Ijumaa huko Washington. Mwakilishi wa China katika mazungumzo hayo Bw Liu He aliwaambia wanahabari kuwa, mazungumzo hayakuvunjika ila tu yalikumbwa na matatizo madogo, hali ambayo ni kawaida na isiyoepukika katika mazungumzo. Aliongeza kuwa, China ina imani na mazungumzo ya siku za usoni.
    • Kujaribu kuibana China kwa suala la Taiwan hakika ni njia isiyopitika 05-09 14:54

    Baraza la Wawakilishi la Marekani Jumanne tarehe 7 lilipitisha "Sheria ya Uhakikisho ya Taiwan ya Mwaka 2019" na "Kurudia tena ahadi ya Marekani kwa Taiwan na kwa utekelezaji wa 'Sheria ya Uhusiano na Taiwan'". Hii ni mara nyingine kwa Marekani kuingilia ovyo masuala ya ndani ya China kwa kutumia suala la Taiwan, ambayo ni hatua ya kisiasa yenye hatari kubwa inayolenga kuzuia maendeleo ya amani ya China.

    • Kundi la Uchumi la "Ukanda Mmoja, Njia Moja" limekuwa kundi kubwa la pili la uchumi duniani 05-08 18:26
    Tokea mwezi Mei mwaka huu, ripoti mbili za utafiti kuhusu Ujenzi wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" zimefuatiliwa sana na watu. Moja ni Ripoti ya vigezo vya uwekezaji wa biashara wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" iliyotolewa na washauri mabingwa wa China na wa nchi za nje wanaoongozwa na Kituo cha mawasiliano ya uchumi cha kimataifa cha China
    • Mkutano wa pili wa viongozi wa Ujenzi wa teknolojia ya dijitali wa China wafunguliwa mjini Fuzhou 05-07 19:40
    Mkutano wa Pili wa Ujenzi wa teknolojia ya dijitali wa China umefunguliwa mjini Fuzhou, mkoani Fujian, na umeshirikisha makampuni kutoka mikoa na miji 31, ikiwemo Mikoa ya utawala maalumu ya Hong Kong, Macao na Taiwan, na kuonesha maendeleo yaliyopatikana nchini China katika ujenzi wa teknolojia ya dijitali.
    • China kuanzisha na kukamilisha mfumo wa maendeleo ya pamoja ya miji na vijiji 05-06 19:35
    Mkurugenzi wa Idara ya mikakati na mipango ya maendeleo iliyo chini ya Kamati ya Maendeleo na Mageuzi ya China Bw. Chen Yajun amesema, maendeleo ya pamoja ya miji na vijiji ni injini yenye nguvu ya China katika kupanua maeneo ya maendeleo. Hivi sasa China inapanga kuanzisha mfumo kamili wa maendeleo ya pamoja ya miji na vijiji hadi ifikapo mwaka 2022, ili kuhimiza uchumi na jamii kupata maendeleo endelevu.
    • Wachina watalii katika mapumziko ya sikukuu ya Mei Mosi 05-01 18:08

    Mapumziko ya sikukuu ya Mei Mosi ya mwaka huu yamerefushwa na kuwa siku nne kutoka siku tatu, na kuwawezesha wachina wengi zaidi kutalii.

    • Rais wa China ahamasisha vijana wa China kwenye hotuba yake ya kuadhimisha Siku ya Vijana
     04-30 17:21

    Kabla ya kufika kwa Siku ya Vijana ya China ambayo ni tarehe 4, Mei, mkutano mkubwa wa hadhara umefanyika leo hapa Beijing, ili kuadhimisha miaka 100 tangu kufanyika kwa Harakati ya Tarehe 4, Mei. Rais Xi Jinping wa China amehutubia mkutano huo akiwahamasisha vijana wawe na uzalendo na upendo kwa familia na binadamu wote, pia amewataka wafanye juhudi ili kutimiza ustawishaji mpya wa taifa la China, na ujenzi wa jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja.

    • Ujenzi wenye sifa nzuri wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" kuleta manufaa mengi
     04-29 16:57

    Mkutano wa pili wa kilele wa ushirikiano wa kimataifa wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" umefungwa hapa Beijing, na makubaliano zaidi ya 280 yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 640 yamefikiwa. Wataalam wanaona kuwa, ujenzi wa pamoja wenye sifa nzuri wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" utaweza kutimiza lengo la kuunganisha ufanisi wa uchumi, jamii na uhifadhi wa mazingira.

    • Rais Xi Jinping wa China apendekeza kujenga kwa pamoja "maskani mazuri ya binadamu duniani" 04-28 17:59

    Maonyesho ya kimataifa ya kilimo cha maua ya mwaka 2019 yatafanyika hapa Beijing, na kushirikiwa na nchi 86 na mashirika 24 ya kimataifa. Rais Xi Jinping wa China kwa nyakati tofauti alifafanua sera ya China ya kujiendeleza bila kuchafua mazingira, na kutoa kipaumbele katika kuhifadhi mfumo wa ikolojia, na kueleza nia ya China ya kushirikiana nchi mbalimbali kujenga kwa pamoja "maskani mazuri ya binadamu duniani".

    • "Ukanda mmoja, njia moja" Pendekezo muhimu kwa dunia iliyo wazi zaidi 04-28 09:53

    Mkutano wa pili wa baraza la kimataifa la "ukanda mmoja, njia moja" umefungwa jana hapa Beijing, na baadaye taarifa ya pamoja kutolewa baada ya mkutano wa majadiliano wa viongozi.

    • Mkutano wa wakuu wa Baraza la ushirikiano wa kimataifa la "Ukanda Mmoja, Njia Moja" wafanyika 04-27 13:10

    Mkutano wa kilele wa baraza la wakuu la ushirikiano wa kimataifa la "Ukanda Mmoja, Njia Moja" umefanyika leo asubuhi, na kuhudhuriwa na viongozi 37 wa nchi, maofisa wa Umoja wa Mataifa na wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako