• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • China kutekeleza hatua 20 za kuvutia uwekezaji wa nje
     10-30 16:29

    Baraza la Serikali la China hivi karibuni limepitisha "pendekezo la namna ya kutumia vizuri uwekezaji wa nje". Kwa mujibu wa pendekezo hilo, China itatekeleza hatua 20 za kufungua mlango zaidi, kuongeza nguvu ya kuhamasisha uwekezaji wa nje, kukuza mageuzi ya kurahisisha uwekezaji, na kuimarisha ulinzi wa maslahi halali ya wawekezaji wa nje.

    • Nchi zaidi ya 170 kushiriki katika Maonesho ya pili ya kimataifa ya bidhaa zinazoagizwa na China
     10-29 19:11

    Maonesho ya pili ya kimataifa ya bidhaa zinazoagizwa na China yatafanyika kuanzia tarehe tano hadi 10 mwezi ujao mjini Shanghai, China. Watu kutoka nchi zaidi ya 170 na mashirika mbalimbali ya kimataifa wanatarajiwa kushiriki katika maonyesho hayo.

    • Rais wa China apongeza mkutano wa kilele wa wanasayansi vijana duniani
     10-26 18:11

    • Rais wa China atoa wito wa amani na urafiki katika michezo ya kimataifa ya majeshi 10-18 20:41

    Rais Xi Jinping wa China leo amekutana na viongozi wa idara za ulinzi na majeshi ya nchi zinazoshiriki kwenye michezo ya kimataifa ya majeshi, na maofisa wa Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Majeshi, kabla ya kuanza rasmi kwa michezo hiyo.

    • Pato la taifa la China laongezeka kwa asilimia 6.2 katika robo tatu za mwanzo mwaka huu
     10-18 18:56

    Takwimu zilizotolewa leo na Idara Kuu ya Takwimu ya China zinaonesha kuwa, katika robo tatu za mwanzo mwaka huu, pato la taifa la China GDP limezidi dola za kimarekani trilioni 9.87, na kuongezeka kwa asilimia 6.2 ikilinganishwa na mwaka jana kipindi kama hiki.

    • China yawahamisha watu kutoka sehemu zenye hali duni ili waondokane na umaskini
     10-17 19:02

    Leo tarehe 17 Oktoba ni Siku ya Kupambana na Umaskini Duniani, na pia ni Siku ya kuondoa Umaskini ya China. Hadi sasa China imepiga hatua kubwa katika ujenzi wa makazi kwa watu waliohamishwa kutoka sehemu zenye hali dunia ili waondokane na umaskini, na watu hao watapata makazi mapya kabla ya mwishoni mwa mwaka 2019.

    • Bw. Jack Ma sasa kuangalia elimu, ujasiriamali na Afrika baada ya kustaafu 10-16 08:32

    Mwanzilishi wa kampuni ya Alibaba Bw. Jack Ma amesema kazi yake kubwa kwa sasa baada ya kustaafu ni kuangalia ni vipi elimu inaweza kutolewa kwa njia tofauti na kuwawezesha wajasiriamali vijana barani Afrika.

    • Rais wa China asisitiza umuhimu wa kuhifadhi mazingira ya kiikolojia ya Mto Huanghe 10-15 16:48

    Jarida la Qiushi la China kesho litatoa makala muhimu ya rais Xi Jinping wa China ya "Hotuba kwenye semina kuhusu uhifadhi wa mazingira ya kiikolojia ya Mto Huanghe na maendeleo yenye sifa nzuri".

    • China yatoa waraka kuhusu usalama wa chakula 10-14 17:37

    Ofisi ya habari ya Baraza la Serikali la China leo imetoa waraka kuhusu usalama wa chakula. Waraka huo umeeleza mafanikio ya kihistoria iliyopata China katika kuleta usalama wa chakula, kuangalia kwa kina mfululizo wa sera na hatua za China katika kulinda usalama wa chakula baada ya mwaka 1996, haswa kufanyika kwa mkutano mkuu wa 19 wa Chama cha Kikomunisti cha China, kufafanua kanuni na msimamo wa China katika kufungua mlango na kufanya ushirikiano wa kimataifa kuhusu soko la chakula pamoja na utetezi wa sera wa China katika suala la chakula kwa siku za baadaye.

    • Ofisa wa Umoja wa Mataifa azungumzia uhusiano wake na China 10-11 09:00

    Huu ni mwaka wa 70 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China. Hivi karibuni mkurugenzi wa idara ya mambo ya Afrika ya kituo cha mali za urithi cha Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa Bw. Edmond Moukala, alipohojiwa na mwanahabari wa Shirika Kuu la Utangazaji la China CMG, ameeleza mambo yake yanayohusika na China.

    • Baba wa taifa la Zambia asema China ni rafiki mwaminifu wa Afrika
     10-09 09:37

    Baba wa Taifa la Zambia Bw. Kenneth Kaunda ni rafiki mkubwa wa China. China yake Zambia ilipata uhuru tarehe 24 Oktoba mwaka 1964 kutokana na juhudi zake na wananchi wenzake, na siku moja baadaye ilianzisha uhusiano wa kibalozi na Jamhuri ya Watu wa China. Bw. Kaunda kwa muda mrefu amehimiza maendeleo ya uhusiano wa kirafiki kati ya nchi yake na China na kati ya Afrika na China.

    • Wachina watalii katika sikukuu ya siku ya taifa
     10-07 08:46

    Mapumziko ya siku ya taifa huwa msimu wa utalii nchini China. Takwimu zilitolewa leo zinaonesha kuwa, katika siku nne za kwanza za mapumziko za sikukuu hiyo, idadi ya Wachina waliotalii ndani ya nchi ilifikia bilioni 542, ambalo ni ongezeko la asilimia zaidi ya nane ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huu, na pato la utalii lilizidi dola za kimarekani bilioni 63.75, na kuongezeka kwa asilimia 8.58.

    • Wachina wavutiwa na maonesho ya kiutamaduni katika siku za mapumziko
     10-03 17:08

    Wachina wako kwenye mapumziko ya wiki moja kutokana na sikukuu ya Siku ya Taifa, na wengi wao wamevutiwa na aina mbalimbali za maonesho ya kiutamaduni.
    • Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China limefanyika Beijing 10-01 21:45
    Tamasha kubwa la kusherehekea Miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China limefanyika Beijing
    Rais Xi Jinping na viongozi wengine wa Chama na serikali wamefika kwenye jukwaa la viongozi lililoko kwenye roshani ya Tian An Men, wakisherehekea pamoja na wananchi usiku wa sikukuu ya taifa
    • Viongozi wa China waweka vikapu vya maua kwa mashujaa waliojitoa mhanga
     09-30 17:22

    Leo tarehe 30 Septemba ni siku ya kuwakumbuka mashujaa wa China waliojitoa mhanga kwa ajili ya nchi na watu wa China. Hafla ya kuweka mashada ya maua kwa mashujaa hao imefanyika kwenye Uwanja wa Tian'anmen mjini Beijing, na kuhudhuriwa na viongozi wa China pamoja na zaidi ya wajumbe 4,000 wa ngazi mbalimbali, wakiwemo askari wa zamani, maofisa wandamizi wastaafu, jamaa wa washujaa waliojitoa mhanga, watu waliopewa medali ya kitaifa, wanafunzi na watoto.

    • Miaka 70 -- tumeipita kwa kusaidiana na kushirikiana – ripoti maalumu ya kuadhimsha miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China 09-30 09:25

    Huu ni mwaka wa 70 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China. Katika miaka 70 iliyopita, China imetekeleza sera ya kidiplomasia ya amani na kujiamulia, na kwa kufuata utaratibu wa kimsingi wa uhusiano wa kimataifa ambao kiini chake ni kanuni tano za kuishi kwa pamoja kwa amani。China imeshirikiana na nchi zinazoendelea kwa msimamo thabiti, ili kujitahidi kujenga utaratibu mpya wa kimataifa ulio wa haki na usawa zaidi, na kuhimiza amani, masikilizano na maendeleo ya dunia. Katika mchakato huo, China imedumisha urafiki mkubwa na nchi za Afrika, ambapo pande hizo mbili zimefanikiwa kujenga uhusiano wa wenzi wa kimkakati katika zama mpya, na zinajitahidi kujenga jumuiya yenye mustakbali wa pamoja, ili kusukuma mbele zaidi uhusiano kati yao. Maendeleo ya uhusiano kati ya China na Afrika ni utendaji wa ujenzi wa pamoja wa China na nchi nyingine wa jumuiya yenye hatma ya pamoja, na pia yameonesha uhai mkubwa wa mawazo ya sera ya kidiplomasia ya China.

    • Uwekezaji mkubwa wa China kwenye elimu waandaa watu wenye uwezo wa kuhimiza maendeleo ya ngazi ya juu 09-28 20:45
    Wakati Jamhuri ya Watu wa China ilipoanzishwa, asilimia 80 ya watu walikuwa hawajapata elimu ya shule. Baada ya miongo saba, China imekuwa na walimu zaidi ya milioni 16, elimu ya lazima ya miaka tisa imefika karibu sehemu zote za nchi.
    • CMG yaanzisha marekebisho ya maendeleo yenye sifa ya juu kwa pande zote 09-26 18:41
    Mhusika mkuu wa CMG amesema, marekebisho hayo ya pande zote yanalenga kutekeleza mwongozo uliotolewa na rais Xi Jinping wa China kwa kazi za kituo kikuu hicho, kuharakisha hatua muhimu za kuhimiza maendeleo ya kina ya muungano wa vyombo vya habari vya aina tofauti, na kujenga vyombo vikuu vya habari vya kiwango cha juu cha kimataifa, ambayo pia ni ukaguzi wa kufanikisha kuripoti sherehe ya siku ya taifa kwa nguvu zote.
    • Uwanja mpya wa ndege wa Daxing utakuwa injini mpya ya maendeleo ya China katika kuhimiza mawasiliano na dunia 09-25 18:08
    "Natangaza, uwanja wa ndege wa kimataifa wa Daxing wa Beijing umezinduliwa rasmi." Ni sauti yake rais Xi Jinping wa China akitangaza kuzinduliwa rasmi kwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Daxing alipohudhuria hafla ya uzinduzi wa uwanja huo wa ndege iliyofanyika sehemu ya Daxing hapa Beijing. Katika siku za baadaye, uwanja wa ndege wa kimataifa wa Daxing wa Beijing utakuwa alama mpya ya ujenzi na uendeshaji wa kituo cha safari za anga cha kimataifa na injini mpya ya kuhimiza maendeleo ya pamoja ya sehemu ya Beijing, Tianjing na Hebei. Uwanja huo unawekezwa dola bilioni 63.2 za kimarekani, na safari za ndege zinaenea sehemu 112 duniani. Inakadiriwa kuwa, idadi ya abiria kwa mwaka itafikia milioni 100 na ndege laki 8 zitaruka na kutua katika uwanja huo.
    • Wanajeshi elfu 15 kushiriki kwenye Gwaride la Siku ya Taifa la China 09-25 08:30

    Gwaride kubwa la kijeshi kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya taifa la China litakalofanyika Oktoba Mosi mjini Beijing, litashirikisha wanajeshi wapatao elfu 15. Kwa mujibu wa ofisi ya uongozi wa gwaride hilo litakalofanyika katika mtaa wa Chang'an katikati ya mji wa Beijing kwa dakika 80, gwaride hilo litakuwa kubwa zaidi kufanyika katika miaka ya karibuni, ambapo jumla ya vikosi 59 na bendi moja ya kijeshi, ndege zaidi ya 160 na vifaa 580 vya kijeshi vya aina mbalimbali vitashiriki.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako