• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • China yailaani Marekani kwa kukiuka kanuni ya kuwepo kwa China moja duniani 05-20 17:03
    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo leo ametoa salamu za kumpongeza Tsai Ing-wen kuapishwa kuwa kiongozi wa Taiwan, akimwita rais wa Taiwan, na kupongeza "uhusiano wa kiwenzi" kati ya Marekani na Taiwan. Maofisa na wanasiasa wengine wa Marekani pia wametoa salamu za kumpongeza Tsai Ing-wen. Wizara ya mambo ya nje ya China imetoa taarifa, ikisema kitendo hicho cha Marekani kimekiuka kanuni ya kuwepo kwa China moja duniani, na taarifa tatu za pamoja zilizotolewa na China na Marekani, na kuingilia kati mambo ya ndani ya China
    • Wanasayansi wa China na Marekani waungana kutafuta chanzo cha virusi vya Corona
     04-30 18:06

    Wanasayansi kutoka Marekani wanashirikiana na wenzao wa China katika kutafuta chanzo cha virusi vya Corona, licha ya baadhi ya wanasiasa wa Marekani kueneza uvumi kwamba virusi hivyo vilitengenezwa katika maabara mjini Wuhan.

    • China na Afrika zashirikiana kwenye mapambano dhidi ya COVID-19
     04-29 17:58

    Nchi nyingi za Afrika zikiwemo Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Benin na Angola, zimeimarisha hatua zao za kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona yanayoenea kwa kasi barani Afrika. China ikiwa ni mwenzi wa nchi za Afrika, imetoa misaada kwa bara hilo kupitia njia mbalimbali.

    • Rais wa China awataka wananchi washirikiane kukabiliana kwa pamoja na janga la virusi vya Corona 04-25 19:21
    • China yaharakisha ujenzi wa nchi yenye nguvu kubwa ya hakimiliki za ubunifu
     04-23 17:08

    Mkuu wa Idara ya Hakimiliki za Ubunifu ya China Shen Changyu leo amesema, mwaka jana idadi ya biashara ya hataza nchini China ilizidi elfu 3, na thamani ya biashara hizo ilizidi dola bilioni 131 za Kimarekani. Wakati huohuo, ushirikiano wa kimataifa katika hakimiliki za ubunifu pia umeimarika.

    • Kiwango cha kupona kwa wagonjwa wa COVID-19 chafikia asilimia 94 nchini China
     04-22 19:10

    Ofisi ya Kamati ya Afya ya Taifa ya China leo imefanya mkutano na waandishi wa habari uliohusu kukabiliana na virusi vya Corona, na kusema mbali na hali ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona kuboreka ndani ya nchi, China itaimarisha kazi ya kuzuia virusi kuingia nchini katika miji inayopakana na nchi za nje.

    • China yachukua hatua za kupunguza ukosefu wa ajira unaotokana na virusi vya Corona
     04-21 19:32

    Msemaji wa Wizara ya Rasilimali Watu na Huduma za Kijamii ya China Lu Aihong leo hapa Beijing amesema katika robo ya kwanza ya mwaka huu, China imetoa hatua mfululizo za sera za kudhibiti maambukizi ya virusi vya Corona, pia imetoa huduma za kijamii na kupunguza ukosefu wa ajira unaotokana na virusi hivyo. Aidha, imepanga kai za kutoa elimu ya ufundi stadi kwenye mtandao wa internet, jambo ambalo limeonesha ufanisi wake wa mwanzo.

    • Viashiria mbalimbali vya uchumi wa China vyaboreka mwezi Machi
     04-20 17:08

    Kamati ya Maendeleo na Mageuzi ya China imesema, toka mwezi Machi, viashiria mbalimbali vya uchumi wa China vimeboreka, shughuli za kiuchumi zinarudi kwenye hali ya kawaida na kampuni za Marekani na Japan zilizopo China zimeongeza sana uwekezaji wao ikilinganishwa na mwezi Februari.

    • Pato la taifa la China lapungua kwa asilimia 6.8 katika robo ya kwanza ya mwaka kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona 04-17 20:16

    Pato la ndani la China (GDP) limefikia dola za kimarekani trilioni 2.91 katika robo ya kwanza ya mwaka huu, ikiwa ni chini kwa asilimia 6.8 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huo kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona.

    • Msaidizi wa waziri wa mambo ya nje wa China akutana na mabalozi wa nchi za Afrika 04-14 18:20

    Jana Jumatatu, msaidizi wa waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Chen Xiaodong alikutana na mabalozi wa nchi zaidi ya 20 za Afrika nchini China kwa wakati mmoja, na kubadilishana nao maoni kuhusu hali ya kinga na udhibiti wa maambukizi ya virusi vya Corona inayohusu waafrika walioko mkoani Guangdong.

    • China yaimarisha hatua za kuzuia kuingia kwa virusi vya Corona kutoka nje kwa raia wote bila tofauti 04-13 17:59

    China yaimarisha hatua za kuzuia kuingia kwa virusi vya Corona kutoka nje kwa raia wote bila tofauti. Taratibu zinazochukuliwa na China za kupambana na virusi vya Corona zina lengo moja tu, yaani kulinda usalama wa watu wote

    • China yahimiza ushirikiano wa kimataifa kukabiliana na COVID-19 04-08 19:53
    Tangu kutokea kwa maambukizi ya virusi vya Corona, kwa kufuata mawazo ya jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja, na msimamo wa kuwajibika, China imetoa taarifa wazi na kwa wakati kuhusu maambukizi ya virusi hivyo, wakati huo huo imeshirikiana na jamii ya kimataifa, na kutoa misaada kwa nchi zinazohitaji.
    • Kipindi maalum cha kujadili changamoto ya virusi vya Corona katika Siku ya Qingming 04-04 07:43

    Tarehe 4, Aprili kwa mwaka huu ni Siku ya Qingming hapa China. Hii ni siku maalum ambayo inatengwa na China kila mwaka kuwakumbuka marehemu. Katika siku hii wachina wote wanapewa mapumziko ya siku moja ili kufanya shughuli za kuwakumbuka marehemu wao wapendwa, mashujaa na watu wengine.

    • Biashara kati ya China na nchi za nje yaanza kufufuka 04-03 10:45
    Wakati biashara ya kimataifa inaathiriwa vibaya na maambukizi ya virusi vya corona, uchukuzi wa mizigo wa reli kati ya Wuhan na miji ya Ulaya umerejeshwa katika hali ya kawaida, huku matunda kutoka nchi za Kusini Mashariki mwa Asia yanasafirishwa kuja kwenye soko la China kwa njia ya reli.
    • Ukarabati wa reli waendelea baada ya treni kuacha njia yake katikati ya China 03-31 09:31
    Ukarabati wa reli unaendelea baada ya treni moja kuacha njia yake kwenye mji wa Chenzhou, mkoani Hunan, katikati ya China, na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine 127 kujeruhiwa.
    • China yatuliza uchumi wa dunia kwa hatua halisi
     03-30 19:53

    Rais Xi Jinping wa China jana alikagua bandari ya Zhoushan mkoani Zhejiang, ambayo inashika nafasi ya kwanza duniani kwa kupokea na kusafirisha mizigo, na wakati dunia ikikabiliwa na maambukizi ya virusi vya COrona, China imetoa ishara ya kujitahidi kulinda utulivu wa mnyororo wa ugavi duniani.

    • Nia ya rais wa Marekani kutenganisha Marekani na China yaleta matokeo mabaya
     03-30 19:49

    Jarida la the Atlantic la Marekani limechapisha makala iliyoandikwa na Profesa Peter Beinart wa Chuo Kikuu cha Mji wa New York, ikisema kitendo cha rais Donald Trump wa Marekani kutenganisha nchi yake na China kimeleta matokeo mabaya.

    • China yaimarisha kwa pande zote hatua za kutuliza ajira zinazokabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona 03-25 18:29

    Baraza la Serikali la China limesema, ili kukabiliana na athari ya maambukizi ya virusi vya Corona, China imetekeleza hatua za kinga na udhibiti kwa usahihi, kuharakisha makampuni kuanza tena uzalishaji, kuwaongoza wafanyakazi vibarua kupata ajira kwa usalama na utaratibu, pia kuongeza nafasi za ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu, ili kuhakikisha utulivu wa jumla wa ajira.

    • China kuadhibu vikali vitendo vinavyokiuka sheria za ukaguzi wa afya katika forodha 03-24 20:06

    Kutokana na hali mbaya ya kuenea kwa virusi vya Corona duniani, China imetoa kipaumbele katika kukinga maambukizi ya nje katika kukabiliana na ugonjwa huo. Hivi karibuni mahakama kuu, idara kuu ya uendeshaji wa mashtaka, wizara ya usalama wa umma, wizara ya sheria na idara kuu ya forodha nchini China zimetoa kwa pamoja mapendekezo kuhusu uhalifu dhidi ya ukaguzi wa afya katika vituo vya forodha.

    • Nusu ya wagonjwa wa COVID-19 watoka hospitali ya Leishenshan ya Wuhan baada ya kupona 03-18 09:26

    Naibu mkurugenzi wa hospitali ya Leishenshan ya Wuhan Bw. Yuan Yufeng jana kwenye mkutano na waandishi wa habari amesema, karibu nusu ya wagonjwa wa COVID-19 waliopewa matibabu kwenye hospitali hiyo wameruhusiwa kutoka baada ya kupona.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako