![]() Rais Xi Jinping wa China ametuma barua ya pongezi kwa mkutano wa mwaka 2019 wa Jukwaa la Maendeleo ya Tibet uliofunguliwa leo katika mji mkuu wa mkoa huo, Lhasa. |
Uwekezaji kutoka nje waendelea kuongezeka nchini China 06-13 19:47 Takwimu zilizotolewa leo na wizara ya biashara ya China zinaonesha kuwa, katika miezi mitano ya kwanza ya mwaka huu, China imetumia kihalisi uwekezaji kutoka nje wenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 53.5, ambalo ni ongezeko la asilimia 6.8 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huu. Hali hii inaonesha kuwa China bado inavutia uwekezaji kutoka nje, na kauli ya Marekani ya kusema hatua yake ya kuongeza ushuru wa bidhaa za China inafanya makampuni ya nje yaondoke China haina msingi wowote. |
Jimmy Carter apewa tuzo kutokana na mchango wake kwa uhusiano kati ya Marekani na China 06-13 17:06 |
![]() Tarehe 12 mwezi Juni baada ya ujenzi wa zaidi siku 220, utandikaji wa njia ya reli ya kasi kati ya Beijing na Zhangjiakou umekamilika. Kumalizika ujenzi huo umeweka msingi thabiti wa majaribio na marekebisho ya reli hiyo katika mwezi Septemba mwaka huu, na kuanza usafiri mwishoni mwa mwaka huu. Baada ya kuanza safari, muda wa kusafiri kati ya Beijing na Zhangjiakou utapungua kutoka saa 3 kwa sasa hadi ndani ya saa 1. |
Urari mbaya wa biashara ya huduma wa China wapungua 06-12 16:32 Takwimu zilizotolewa leo na wizara ya biashara ya China zinaonesha kuwa, kuanzia mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu, thamani ya biashara ya huduma kati ya China na nchi za nje ilizidi dola bilioni 253 za kimarekani, ambalo ni ongezeko la asilimia 4.1 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huu, na urari mbaya wa biashara ya huduma ulipungua kwa asilimia 9.7. |
![]() Wizara ya usafiri ya China imesema vijiji vyote vya China vinatarajiwa kuwa na huduma ya usafiri wa mabasi kabla ya kufikiwa mwezi Septemba mwaka 2020. |
Marekani haipaswi kuhusisha mambo yote na usalama wake 06-11 19:24 Marekani imeweka alama ya "matishio ya usalama" ya nchi hiyo kwa bidhaa za chuma, aluminum, magari na vipuri vya magari kutoka nchi za nje, uwekezaji wa nje, wanafunzi na wasomi wa kigeni na hata akaunti za mitandao ya kijamii ya watu wanaoomba visa ya Marekani. Inaonekana kuwa Marekani inaweza kuhusisha mambo yoyote na usalama wake. |
![]() Kituo cha kushughulikia na kuratibu matukio ya dharura ya mtandao wa kompyuta cha China, hivi karibuni kimetoa ripoti ya mwaka 2018 kuhusu hali ya jumla ya usalama wa mtandao wa Internet ya China. Takwimu zinaonyesha kuwa, mashambulizi mengi ya kimtandao dhidi ya China yanatoka Marekani, na mashambulizi hayo bado yanaongezeka. |
Uchumi wa China waendelea vizuri licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali 06-10 19:52 Takwimu zilizotolewa leo na idara kuu ya forodha ya China zinaonesha kuwa, katika miezi mitano iliyopita mwaka huu, thamani ya biashara kati ya China na nchi za nje imefikia karibu dola za kimarekani trilioni 1.76, ambalo ni ongezeko la asilimia 4.1 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huu. |
Rais wa China kufanya ziara katika Asia ya kati na kuhudhuria mkutano wa SCO na mkutano wa CICA 06-10 17:00 Rais Xi Jinping wa China atafanya ziara rasmi nchini Kyrgyzstan na Tajikistan kuanzia tarehe 12 hadi 16, na kuhuduria mikutana kadhaa mikubwa itakayofanyika katika nchi hizo ukiwemo mkutano wa 19 wa kamati ya utendaji ya viongozi ya Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai SCO. Naibu waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Zhang Hanhui amesema, ziara hiyo itasukuma mbele uhusiano kati ya China na nchi hizo mbili za Asia ya kati. |
![]() Takwimu zilizotolewa na Idara Kuu ya Takwimu ya China zinaonesha kuwa, alama ya usimamizi wa manunuzi PMI nchini China kwa mwezi Mei imeshuka na kuwa asilimia 49.4, lakini uchumi wa China bado umedumisha maendeleo tulivu. |
![]() 05-30 16:34 Rais Xi Jinping wa China atafanya ziara rasmi nchini Russia kuanzia tarehe 5 hadi 7 mwezi ujao, ambapo anatarajiwa kuhudhuria Kongamano la 23 la St. Petersburg la Uchumi wa Dunia. Wizara ya mambo ya nje ya China imesema ziara hiyo itafungua ukurasa mpya wa uhusiano kati ya nchi hizo mbili. |
Marekani haipaswi kuwa na wasiwasi kwamba China itachukua nafasi yake 05-29 19:52 Baadhi ya wanasiasa wa Marekani hivi karibuni wamesema, uchumi wa China unakua kwa haraka, na China itakuwa na nguvu kubwa zaidi kuliko Marekani. Lakini ukweli ni kwamba, China haiwezi kuchukua nafasi ya Marekani kuwa lengo lake la maendeleo. |
![]() 05-29 16:49 Mkutano wa kilele wa makampuni 500 makubwa zaidi duniani umefanyika jana hapa Beijing. Wajumbe kutoka makampuni ya nje wanaona kuwa, China ina nafasi kubwa ya kuendeleza biashara ya huduma, kwani serikali ya nchi hiyo inaendeleza sera ya kufungua mlango kwa nia thabiti. |
![]() Katibu mkuu wa kamati ya chama cha kikomunisti cha China mkoani Hebei, Bw. Wang Dongfeng, leo amesema tangu China mpya kuanzishwa miaka 70 iliyopita, mkoa wa Hebei umepata maendeleo makubwa katika mambo mbalimbali. |
Mitaji ya kimataifa yapiga kura ya ndiyo kwa uchumi wa China 05-28 19:51 Shirika la Morgan Stanley Capital International Index leo limeinua kiwango cha nafasi ya soko la hisa la China kwenye alama yake ya kimataifa ya hisa. Hii ni mara nyingine kwa mitaji ya kimataifa kupiga kura ya ndiyo kwa maendeleo ya uchumi wa China. |
![]() 05-27 16:48 Rais Xi Jinping wa China hivi karibuni alipofanya ukaguzi mkoani Jiangxi, aliweka maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya safari ndefu ya Jeshi Jekundu la China, na kusisitiza kuwa moyo wa "safari ndefu" utang'aa daima. |
Wakuu wa majimbo ya Marekani wakosoa sera ya biashara ya nchi hiyo 05-24 10:25 Wakati Marekani inapoongeza mvutano wa biashara na China, kongamano la 5 la wakuu wa majimbo ya China na Marekani linafanyika mjini Lexington, Marekani. Maofisa waandamizi wa majimbo ya Marekani wamesema sera ya biashara ya nchi hiyo imeleta utatanishi, na inaumiza kampuni za nchi hiyo. |
Marekani inajiumiza kwa kutumia "fimbo ya ushuru" 05-23 09:58 Hivi karibuni baadhi ya watu wa Marekani wamesema, nchi hiyo imepata hasara kubwa kutokana na urari mbaya katika biashara na China, ambapo mamilioni ya ajira zimepotea. Wataalamu wa China wanaona kuwa, ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya nchi hizo mbili unanufaisha pande zote, kauli ya Marekani haina msingi wowote, na Marekani itajiumiza kwa kutumia ovyo "fimbo ya ushuru". |
![]() Baada ya kuweka vikwazo dhidi ya kampuni ya Huawei ya China, Marekani hivi karibuni imeikashifu kampuni ya DJI ya China, kuwa ndege zisizo na rubani zinazotengenezwa na kampuni hiyo zina hatari inayowezekana kuwepo na kutishia kuamua kama kuweka kampuni ya kutengeneza vifaa vya video vya usimamizi ya Hikvision ya China katika orodha ya marufuku na kuizuia kununua teknolojia kutoka makampuni za Marekani au la katika wiki kadhaa zijazo. Kabla ya hapo, wanasiasa wachache wa Marekani hata walidai kuwa kampuni ya CRRC ya China kushinda zabuni ya ubunifu wa subway mpya ya mji wa New York kutaleta tishio kwa usalama wa taifa wa Marekani. … ana maelezo zaidi. |
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |