• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • Kiwango cha kurejea kwa uzalishaji nchini China chafikia asilimia 90 isipokuwa mikoa michache
     03-17 17:47

    Kamati ya Maendeleo na Mageuzi ya China imesema kiwango cha kurejea kwa uzalishaji nchini humo kimefikia zaidi ya asilimia 90 isipokuwa mikoa michache ukiwemo Hubei, na shughuli za uzalishaji za kampuni za nje pia zinarudi katika hali ya kawaida.

    • Rais Xi Jinping asema China itatuma wataalamu zaidi wa matibabu nchini Italia 03-17 09:29

    Rais Xi Jinping wa China amesema, China itatuma wataalamu zaidi wa matibabu nchini Italia, pia itafanya juhudi kadiri iwezekanavyo kutoa vifaa vya matibabu na misaada mingine kwa Italia.

    • Ripoti ya ukiukwaji wa haki za binamu wa Marekani kwa mwaka 2019 03-13 17:01

    Ofisi ya Habari ya Baraza la Serikali la Jamhuri ya Watu wa China

    Machi, 2020

    • China yasisitiza ari ya kuondoa umaskini kwa wakati uliopangwa licha ya athari ya COVID-19 03-12 17:34

    Mkurugenzi wa ofisi ya kupambana na umasikini iliyo chini ya Baraza la Serikali la China Bw. Liu Yongfu leo amesema, baada ya juhudi za zaidi ya miaka minne, wilaya zenye umaskini uliokithiri nchini China imepungua na kufikia 52 kutoka 832 mwishoni mwa mwaka 2012. Amesisitiza kuwa, maambukizi ya COVID-19 hayataathiri vigezo, muda na kazi ya kuondoa umaskini, pia hayatabadilisha imani na nia ya China ya kutimiza lengo hilo kwa wakati uliopangwa.

    • China kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuondoa umaskini kwa sifa ya juu 03-10 18:55

    China imepanga kukamilisha kazi ya kuondoa umasikini katika maeneo ya vijijini mwaka huu wa 2020, na hiyo ni ahadi iliyotolewa na Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China, ambayo ni lazima itimizwe kwa wakati uliopangwa. Katika semina ya kuondoa umaskini, rais Xi Jinping wa China ametoa amri mpya ya kupata ushindi katika mapambano dhidi ya umaskini.

    • Vijana wa Wuhan wachangia kazi ya kukabiliana na maambukizi 03-05 17:57

    Leo tarehe 5 Machi ni siku ya vijana wanaojitolea nchini China. Katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya korona, mbali na madaktari na wauguzi, vijana wa Wuhan, mji ulioathiriwa vibaya na maambukizi hayo, pia wamejitolea kuchangia katika mapambano hayo.

    • Maelfu ya watu wanaojitolea wafanya kazi katika mapambano dhidi ya virusi vya Korona 03-04 18:25

    Wakati madaktari wanajitahidi kuokoa wagonjwa wanaoambukizwa COVID-19, watu wa sekta mbalimbali pia wanasaidia katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo mjini Wuhan. Kuanzia misaada ya matibabu, chakula na bidhaa, na msaada wa kisaikolojia, usafirishaji na huduma za kijamii, maelfu ya watu wanaojitolea wanajibu kwa haraka na kwa makini baada ya Wuhan kufungwa ili kupunguza kuenea kwa virusi hiyo.

    • Wataalamu wa WHO wasema hatua za China za kupambana na COVID-19 zimepata mafanikio 02-25 09:07
    Baada ya kufanya ukaguzi nchini China kwa siku 9, jopo la wataalamu wa China na shirika la afya duniani WHO, jana lilifanya mkutano na waandishi wa habari hapa Beijing. Kiongozi wa watalaamu wa nchi za nje Bw. Bruce Aylward amesema baada ya kufanya ukaguzi kwa makini na kwa pande mbalimbali, watalaamu wanaona hatua zilizochukuliwa na China kupambana na virusi hiyo, zimezuia kwa ufanisi hali ya kuenea kwa virusi hivyo kwa kasi.
    • Maambukizi ya virusi vya korona hayatabadili maendeleo ya muda mrefu ya biashara ya China na nje
     02-24 17:18

    Wizara ya Biashara ya China imesema maambukizi ya virusi vya korona COVIC-19 hayatabadili mwelekeo wa maendeleo ya muda mrefu ya biashara ya China na nchi za nje na nguvu ya ushindani ya China katika kuvutia fedha za kigeni, na China itaendelea kuwa sehemu inayowekezwa zaidi na kampuni za kimataifa.

    • Mradi wa kujitolea kupambana na virusi vya korona mjini Wuhan wavutia zaidi ya watu elfu 10 02-24 10:01

    Mradi wa kujitolea umewavutia watu zaidi ya elfu 10 katika mji wa Wuhan, ambao ni kiini cha maambukizi ya virusi vipya ya korona vinavyosababisha nimonia (COVID-19), mkoani Hubei, China, muda mfupi tu baada kuanzishwa.

    • Afrika haipaswi kuchukuliwa na Marekani kuwa uwanja wa vita dhidi ya China
     02-23 19:55

    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo hivi karibuni alimaliza ziara nchini Senegal, Angola na Ethiopia na katika Umoja wa Afrika. Hii ni mara yake ya kwanza kufanya ziara katika nchi za Afrika zilizoko kusini mwa Sahara, katika karibu miaka miwili iliyopita, tangu ateuliwe kuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani.

    • China yajitahidi kutibu wagonjwa wa COVID-19 wakati idadi ya vitanda vya hospitali katika kiini cha mlipuko inazidi elfu 40 02-20 09:10

    China inafanya juhudi zote kuwatibu wagonjwa wa nimonia ya COVID-19 inayosababishwa na virusi vya korona katika mji wa Wuhan ambao ndio kiini cha mlipuko wa virusi hivyo, wakati idadi ya vitanda vya hospitali kwa ajili ya wagonjwa wa COVID-19 imeongezeka na kuzidi elfu 40, huku idadi ya wafanyakazi wa afya waliojitolea kutoka nje ya mkoa, ikizidi elfu 30.

    • Chombo cha anga ya juu cha Chang'e-4 chaanza kazi tena siku ya 15 ya mwandamo wa mwezi 02-19 18:10

    Chombo cha anga ya juu cha China kinachoitwa Chang'e kimeanza tena kazi yake ya uchunguzi kwa siku ya 15 ya mwandamo baada ya kulala wakati wa usiku wa baridi kali.

    • Kushinda COVID-19 kwa niaba ya jumuiya yenye hatma ya pamoja 02-19 17:26

    Tangu kutokea kwa maambukizi ya virusi vipya ya korona vinavyosababisha nimonia (COVID-19), watu wa nchi mbalimbali duniani wameeleza kuiunga mkono China.

    • Mtaalam wasisitiza kutumia dawa ya jadi ya kichina katika kupambana na virusi vya korona 02-19 09:20
    Mtaalamu wa magonjwa kwenye mfumo wa kupumua Bw. Zhong Nanshan amesisitiza utafiti wa dawa ya jadi ya kichina TCM kwenye mapambano dhidi ya nimonia ya COVID-19 inayosababishwa na virusi vya korona.
    • China yaitaka Marekani kuacha vitendo vya uchochezi 02-18 18:45

    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang amesema, China inahimiza Marekani kushughulikia kwa haki kampuni za China na ushirikiano wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili na kuacha vitendo vya uchochezi.

    • Adui mkubwa zaidi sio virusi vya korona, bali ni habari za kupotosha zinazoweza kuwatenga watu 02-18 18:36

    China bado inajitahidi kupambana na maambukizi ya virusi vipya vya korona vinavyosababisha nimonia (COVID-19). Wakati huohuo, badala ya kutoa misaada, baadhi ya nchi za magharibi zinapaka matope China kutokana na ugonjwa huo. Shirika Kuu la Utangazaji la China limetoa tahariri inayouliza, "Adui mkubwa zaidi kuliko virusi ni nini".

    • Dawa za malaria zathibitishwa kuwa na ufanisi wa kutibu nimonia ya COVID-19 02-18 09:17

    Wataalamu wa China wamethibitisha kuwa dawa ya malaria aina ya Chloroquine Phosphate ina ufanisi wa kutibu ugonjwa wa nimonia unaosababishwa na virusi vya korona COVID-19.

    • China yatoa wito wa ushirikiano wa kimataifa dhidi ya COVID-19 02-14 19:18

    Mjumbe wa Baraza la Taifa la China ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya nje ya China Bw. Wang Yi amesema virusi havina mipaka, na jumuiya ya kimataifa inapaswa kufanya kazi kwa pamoja kupigana na virusi vipya vya korona (COVID-19).

    • Rais wa China aagiza kupeleka madaktari wengine 2,600 wa jeshi katika mji wa Wuhan unaokumbwa na maambukizi 02-13 18:25

    Rais Xi Jinping wa China ameagiza madaktari wengine 2,600 wa kijeshi kupelekwa wametumwa mjini Wuhan, ambao umeathirika zaidi na maambukizi ya virusi vipya ya korona COVID-19.

    prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 next
    SearchYYMMDD  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako